Hosea
3 Lakini mimi ndiye nilimufundisha Efraimu kutembea,+ nikiwakamata katika mikono yangu;+
Na hawakutambua kama nilikuwa nimewaponyesha.
4 Niliendelea kuwakokota kwa kamba za wanadamu,* ndiyo, kwa kamba za upendo;+
Na nilikuwa kwao kama mutu mwenye kutosha nira kwenye mataya* yao,
Na kwa upole nililetea kila mumoja chakula.
5 Hawatarudia katika inchi ya Misri, lakini Ashuru atakuwa mufalme wao,+
Kwa sababu walikataa kurudia kwangu.+
6 Na upanga utazunguka-zunguka juu ya miji yake+
Na kuharibu mapingo* yake na kumeza miji yake kwa sababu ya mipango yao ya mubaya.+
7 Watu wangu wako na muelekeo wa kukosa uaminifu kwangu.+
Hata kama waliwaita kuelekea juu,* hakuna mutu yeyote mwenye anasimama.
8 Namna gani ninaweza kukuacha, Ee Efraimu?+
Namna gani ninaweza kukutoa, Ee Israeli?
Namna gani ninaweza kukutendea kama Adma?
Namna gani ninaweza kukufanya ukuwe kama Seboimu?+
9 Sitaonyesha kasirani yangu yenye kuwaka.
Sitaharibu tena Efraimu,+
Kwa maana mimi ni Mungu, siko mwanadamu,
Mutakatifu mwenye kuwa katikati yenu;
Na sitakuja kwenu kwa kasirani kali.
10 Watamufuata Yehova, na atanguruma kama simba;+
Wakati atanguruma, wana wake watakuja wakitetemeka kutoka mangaribi.+
11 Watatetemeka kama ndege wakati watakuja kutoka Misri,
Kama njiwa kutoka inchi ya Ashuru;+
Na nitawafanya wakae katika nyumba zao,” ni vile Yehova anasema.+
12 “Efraimu amenizunguka kwa maneno ya uongo,
Na nyumba ya Israeli kwa udanganyifu.+