Nahumu
1 Tangazo juu ya Ninawi:+ Kitabu cha maono ya Nahumu* Mwelkoshi:
2 Yehova ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu+ na ni mwenye kulipiza kisasi;
Yehova analipiza kisasi na iko* tayari kuonyesha kasirani yake.+
Yehova analipiza kisasi juu ya wapinzani wake,
Na anawekea maadui wake kasirani kali.
3 Yehova hakasirike haraka+ na ni mwenye nguvu nyingi,+
Lakini Yehova hatakosa hata kidogo kutoa azabu yenye kustahili.+
Njia yake iko katika upepo wenye kuharibu na katika zoruba,
Na mawingu ni vumbi ya miguu yake.+
Bashani na Karmeli zinakauka,+
Na maua ya Lebanoni yanakauka.
5 Milima inatetemeka kwa sababu yake,
Na vilima vinayeyuka.+
Dunia itainuka kwa sababu ya uso wake,
Pamoja na inchi na wale wote wenye kukaa ndani yake.+
6 Ni nani mwenye anaweza kusimama mbele ya kasirani yake kali?+
Ni nani mwenye anaweza kuvumilia joto la hasira yake?+
Atamwanga kasirani yake kama moto,
Na miamba itapasuka vipande-vipande kwa sababu yake.
7 Yehova ni mwema,+ naye ni ngome katika siku ya taabu.+
Hasahau* wenye wanatafuta kimbilio katika yeye.+
8 Kupitia mafuriko yenye kufagia ataharibu mahali pake kwa ukamili,*
Na giza litafuatilia maadui wake.
9 Mutafanya mupango gani mubaya juu ya Yehova?
Yeye ataleta uharibifu kamili.
Taabu haitatokea tena mara ya pili.+
10 Kwa sababu wamesukwa kama miiba,
Na wako kama watu wenye kulewa pombe;*
Lakini watateketea kwa moto kama nyasi yenye kukauka.
11 Katikati yenu atatokea mutu mwenye kupanga uovu juu ya Yehova,
Mwenye kutoa mashauri yenye hayana mafaa yoyote.
12 Yehova anasema hivi:
“Hata kama walikuwa na nguvu nyingi na walikuwa wengi,
Hata katika hali hiyo watakatwa na kupotea kabisa.*
Nimekutesa,* lakini sitaendelea kukutesa.
13 Na sasa nitavunja nira yake na kuiondoa juu yako,+
Na nitakata pingu zako vipande mbili.
14 Yehova ameamuru hivi juu yako:*
‘Jina lako halitaendelezwa tena.
Nitaharibu sanamu za kuchongwa na sanamu za metali* zenye kuwa katika nyumba ya* miungu yako.
Nitakuchimbia kaburi, kwa sababu wewe ni mwenye kuchukiza sana.’
Ufanye sikukuu zako,+ Ee Yuda, utimize naziri zako,
Kwa sababu mutu mwenye hana mafaa yoyote hatapita katikati yenu tena hata siku moja.
Ataharibiwa kabisa.”