Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 29
  • Je, Ninapaswa Kusali kwa Watakatifu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Ninapaswa Kusali kwa Watakatifu?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu la Biblia
  • Je, Tunapaswa Kusali kwa Watakatifu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Tunapaswa Kusali kwa Yesu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kumukaribia Mungu Karibu Katika Sala
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 29

Je, Ninapaswa Kusali kwa Watakatifu?

Jibu la Biblia

Hapana. Biblia inaonyesha kwamba tunapaswa kusali kwa Mungu pekee, katika jina la Yesu. Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Basi ombeni hivi: Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe.” (Mathayo 6:9, La Sainte Bible en swahili de la R.D Congo) Yesu hakuwafundisha hata kidogo wanafunzi wake kusali kwa watakatifu, malaika, ao mutu mwengine yeyote isipokuwa Mungu.

Yesu pia aliwaambia wafuasi wake hivi: “Mimi ni njia na kweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba, asipopita kwangu.” (Yohana 14:6, Verbum Bible) Yesu pekee ndiye amepewa daraka la kutusemea kwa Mungu.—Waebrania 7:25.

Kuna ubaya gani ikiwa ninasali kwa Mungu na vilevile kwa watakatifu?

Moja kati ya Sheria Kumi inasema hivi: “Mimi, Bwana Mungu wako, mimi ni Mungu mwenye wivu.” (Kutoka 20:5, Verbum Bible) Mungu ni “mwenye wivu” katika maana gani? Maelezo katika tafsiri ya New American Bible yanaonyesha kwamba Mungu ‘anaomba watu wajitoe kwake yeye pekee.’ Mungu anapenda ibada—kutia ndani sala—itolewe kwake tu.—Isaya 48:11.

Tunamukosea Mungu tunaposali kwa mutu mwengine yeyote, hata tunaposali kwa watakatifu ao malaika watakatifu. Mutume Yohana alipotaka kumuabudu malaika, malaika huyo alimuzuia kufanya hivyo kwa kumuambia hivi: “Usifanye hivi; Mimi ni mutumishi mwenzako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Abudu Mungu.”—Ufunuo 19:10, La Sainte Bible en swahili de la R.D Congo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine