Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ‘Kile Unachoweka Naziri, Timiza’
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2017 | Mwezi wa 4
    • 7. (a) Hana alifanya naziri gani, na sababu gani? Hilo lilikuwa na matokeo gani? (b) Naziri ya Hana ilimaanisha nini kwa Samweli? (Ona maelezo ya chini.)

      7 Hana pia alifanya naziri kwa Yehova wakati alikuwa na mahangaiko katika maisha yake. Alikuwa na huzuni kwa sababu hakukuwa na watoto, na alikuwa anateswa na kuzarauliwa kwa sababu ya jambo hilo. (1 Samweli 1:4-7, 10, 16) Aliambia Yehova namna alikuwa anajisikia, na akatoa ahadi hii: ‘Ee Yehova wa majeshi, ikiwa hakika utayaona mateso ya kijakazi wako, nawe kwa kweli unikumbuke, na ikiwa hautamusahau kijakazi wako na kwa kweli umupe kijakazi wako uzao wa kiume, mimi nitamutoa kwa Yehova siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita juu ya kichwa chake.’a (Soma maelezo ya chini.) (1 Samweli 1:11) Yehova alisikiliza sala ya Hana, na mwaka wenye ulifuata alizaa mutoto mwanaume, Samweli. Hana alifurahi sana! Lakini hakusahau naziri yenye alimutolea Mungu. Wakati mutoto wake mwanaume alizaliwa, alisema hivi: ‘Nimemuomba kutoka kwa Yehova.’—1 Samweli 1:20.

  • ‘Kile Unachoweka Naziri, Timiza’
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2017 | Mwezi wa 4
    • a Hana alimuahidi Yehova kama ikiwa angezaa mutoto mwanaume, mutoto huyo angekuwa Munaziri maisha yake yote. Hilo lilimaanisha kama mutoto wake mwanaume angetolewa kwa Mungu na kutiwa pembeni kwa ajili ya kazi ya Yehova.—Hesabu 6:2, 5, 8.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine