‘Hekima Inapaaza Sauti’ Unaweza Kuisikia?
‘Je, hekima haiendelee kupaaza sauti, na utambuzi hauendelee kutoa sauti yake? Inasimama juu ya vilele, kando ya njia, kwenye makutano ya barabara. Kwenye kiingilio cha malango inaendelea kulia kwa sauti kubwa.’ —METHALI 8:1-3.
HEKIMA ni ya maana sana. Ikiwa hatuna hekima, tunaweza kuendelea kufanya makosa ya kipumbavu. Lakini tunaweza kupata wapi hekima ya kweli? Muandikaji wa kitabu cha Biblia cha Methali alijua kwamba Muumbaji wetu ana hekima ya juu sana. Zaidi ya hayo, wanadamu karibu wote wanaweza kupata hekima yake kupitia kitabu cha pekee sana, ni kusema, Biblia. Fikiria mambo haya:
Kitabu kimoja kinasema hivi: Biblia ni “kitabu chenye kimegawanywa sana katika historia. Kimetafsiriwa mara nyingi na katika luga nyingi kuliko kitabu kingine chochote.” (The World Book Encyclopedia) Biblia inapatikana sasa katika luga karibu 2600, ikiwa nzima ao kwa sehemu, na hilo linafanya watu zaidi ya 90 juu ya 100 katika dunia waipate.
Hekima ‘inaendelea kulia kwa sauti kubwa’ kwa njia ya kwelikweli. Katika andiko la Mathayo 24:14, tunasoma hivi: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho [wa ulimwengu huu] utakapokuja.”
“Habari njema” hiyo ni hekima ya kweli kwa sababu inaonyesha njia ya hekima yenye Mungu atatumia ili kushugulikia matatizo ya wanadamu, njia hiyo ni Ufalme wake. Ufalme huo ni serikali ya Mungu itakayotawala dunia yote, kutakuwa dunia moja na utawala moja. (Danieli 2:44; 7:13, 14) Ndiyo sababu Yesu Kristo alisali hivi: “Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.”—Mathayo 6:9, 10.
Mashahidi wa Yehova wanaona kuwa ni pendeleo kubwa kutangaza Ufalme wa Mungu katika inchi 239! Kwa kweli, hekima, hekima ya Mungu, ‘inapaaza sauti’ kabisa hata “kwenye kiingilio cha malango.” Unaweza kuisikia?