Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/01 uku. 1
  • Nyinyi Ni “Kitu cha Kutazamwa”!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Nyinyi Ni “Kitu cha Kutazamwa”!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Iga Mufano wa Malaika Waaminifu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Namna Gani Malaika Wanaweza Kukusaidia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 8/01 uku. 1

Nyinyi Ni “Kitu cha Kutazamwa”!

1 Mtume Paulo aliandika: “Tumekuwa kitu cha kutazamwa mahali pa michezo kwa ulimwengu, na kwa malaika, na kwa wanadamu.” (1 Kor. 4:9) Hilo linamaanisha nini, nalo linapaswa kuwa na uvutano gani juu yetu katika huduma yetu leo?

2 Kwa Mkorintho, yaelekea maneno “kitu cha kutazamwa mahali pa michezo” yalikumbusha tukio la mwisho la shindano la Kiroma la kupigana na wanyama, tukio ambalo katika hilo watu waliohukumiwa walionyeshwa mbele ya maelfu ya watazamaji kabla ya kuchinjwa kikatili. Vivyo hivyo, kikundi kikubwa cha watazamaji​​—wanadamu na malaika​​—waliona mateso yaliyowapata Wakristo wa karne ya kwanza kwa sababu ya kutoa ushahidi kuhusu Ufalme. (Ebr. 10:​32, 33) Mwendo wao wa kulinda uaminifu ulikuwa na uvutano juu ya watazamaji wengi, kama vile tu uvumilivu wetu unavyokuwa na uvutano katika uwanja wa michezo wa kisasa. Ni kwa nani sisi tuko kitu cha kutazamwa?

3 Kwa Ulimwengu na kwa Wanadamu: Nyakati nyingine vyombo vya habari hutangaza ripoti kuhusu utendaji mbalimbali wa watu wa Yehova. Ingawa tunathamini ripoti zenye kupatana na kweli na zenye unyofu katika kushughulika na kazi yetu, tunatazamia pia mara kwa mara ripoti mbaya zienezwe na wale wanaosema vibaya juu yetu. Hata hivyo, tunapaswa kuendelea kujipendekeza wenyewe kuwa wahudumu wa Mungu “kupitia ripoti mbaya na ripoti njema.” (2 Kor. 6:​4, 8) Kwa watazamaji wanyofu, inakuwa wazi kwamba sisi ndio wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo.

4 Kwa Malaika: Viumbe vya kiroho pia hututazama sisi. Ibilisi na mashetani wake hutazama, lakini wakiwa na “hasira kubwa,” wakitafuta kusimamisha “kazi ya kutoa ushahidi kuhusu Yesu.” (Ufu. 12:​9, 12, 17) Malaika waaminifu wa Mungu hutazama na kushangilia wakati hata mtenda-dhambi mmoja anapotubu. (Luka 15:10) Tunapaswa kutiwa nguvu kwa kujua kwamba malaika huona kazi yetu kuwa ndiyo kazi ya haraka zaidi na yenye manufaa zaidi inayofanywa duniani leo!​​—Ufu. 14:​6, 7.

5 Wakati unapokabiliana na upinzani au unapofikiri kwamba huduma yako haipati matokeo, kumbuka kwamba wewe unatazamwa na ulimwengu mzima. Uvumilivu wako mwaminifu unasema mengi. Mwishowe, ‘pigano lako bora la imani’ litafanya iwezekane kwako ‘kushika imara uhai udumuo milele.’​​—1 Tim. 6:​12.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine