Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 5 uku. 4-5
  • Ukweli Kuhusu Malaika

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ukweli Kuhusu Malaika
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Malaika
    Amuka!—2017
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Namna Gani Malaika Wanaweza Kukusaidia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Iga Mufano wa Malaika Waaminifu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 5 uku. 4-5
Malaika mukuu pamoja na malaika wengine wengi

HABARI KUBWA | MALAIKA​—WAKO KABISA? SABABU GANI TUFIKIRIE JAMBO HILO?

Ukweli Kuhusu Malaika

Utapenda kujua ukweli kuhusu malaika​—wao ni nani, walitoka wapi, na wanafanya nini? Hakuna nafasi ingine ya muzuri kwenye tunaweza kupata majibu, isipokuwa tu katika Neno lenye liliongozwa na roho ya Mungu, Biblia. (2 Timotheo 3:16) Biblia inatufundisha nini?

  • Kama vile tu Mungu ni Roho, malaika pia ni roho wenye hawaonekane wenye ‘hawana nyama na mifupa.’ Malaika waaminifu wanaishi mbinguni na wanamuona Mungu moja kwa moja.​—Luka 24:39; Mathayo 18:10; Yohana 4:24.

  • Wakati fulani, malaika walitokea katika umbo la mwanadamu ili kufanya kazi zenye Mungu aliwapatia hapa duniani na kisha kumaliza kazi zao, walivaa tena miili ya kiroho.​—Waamuzi 6:11-23; 13:15-20.

  • Hata kama Biblia inaonyesha malaika wakiwa wanaume na walitokea katika umbo la wanaume, hakuna malaika mwanaume wala mwanamuke. Hawaoane wala kuzaa malaika wengine. Zaidi ya hilo, hawakuishi kwanza duniani wakiwa wanadamu​—ikuwe kama watoto ao watu wazima. Malaika waliumbwa na Yehova; ndiyo sababu Biblia inawaita “wana wa Mungu wa kweli.”​—Ayubu 1:6; Zaburi 148:2, 5.

  • Biblia inataja ‘luga za wanadamu na za malaika,’ ili kuonyesha kwamba watu wa kiroho wako na luga na namna yao ya kusema. Hata kama Mungu alitumikisha malaika ili kuzungumuza na wanadamu, hakuturuhusu kuwaabudu ao kusali kwao.​—1 Wakorintho 13:1; Ufunuo 22:8, 9.

  • Kuko malaika wengi sana, pengine mamiliare.a​—Danieli 7:10; Ufunuo 5:11.

  • Malaika wako na “uwezo katika nguvu,” ni kusema, wako na nguvu zaidi kuliko mwanadamu, na wako na akili ya juu kuliko ya mwanadamu. Ni wazi kwamba, wanaweza kufanya safari kwa mwendo wa ajabu sana, kuliko namna tunaweza kuwazia.​—Zaburi 103:20; Danieli 9:20-23.

  • Hata kama wako na akili ya juu na nguvu za kiroho, malaika wako na mipaka, na kuko mambo fulani yenye hawajue.​—Mathayo 24:36; 1 Petro 1:12.

  • Malaika waliumbwa na utu mbalimbali, sifa zenye kufanana na sifa za Mungu, na uhuru wa kuchagua. Kwa hiyo, kama vile wanadamu, malaika wanaweza kuchagua kufanya mema ao mabaya. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, malaika fulani walichagua kumuasi Mungu.​—Yuda 6.

a Neno la zamani la Kigiriki lenye kutumiwa katika andiko la Ufunuo 5:11 linamaanisha “makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu.” Hilo linafanya tufikiri kwamba kunaweza kuwa mamia ya milioni, ao hata mamiliare ya viumbe wa roho!

Malaika wa Mungu Wanapangwa Namna Gani?

Malaika mukuu, Mikaeli, katika uwezo na mamlaka, yeye ni mukuu kuliko malaika wengine. Maandiko yanaonyesha waziwazi kwamba Mikaeli ni jina lingine la Yesu Kristo.​—1 Wathesalonike 4:16; Yuda 9.

Maserafi wako na cheo cha juu sana kati ya malaika kuhusu pendeleo na heshima, na wanatumikia kwenye kiti cha Ufalme cha Mungu.​—Isaya 6:1-3.

Makerubi pia wako na cheo cha juu na wanahangaikia madaraka ya pekee yenye kuwa na uhusiano na Mweza-Yote mwenye kuwa na utukufu mukubwa. Mara nyingi wanaonyeshwa wakiwa wenye kumutumikia.​—Mwanzo 3:24; Ezekieli 9:3; 11:22.

Makumi ya maelfu ya malaika wenye kutoa ujumbe wanatumika kama wawakilishi wa Aliye Juu Zaidi katika kutimiza mapenzi ya Mungu.b​—Waebrania 1:7, 14.

b Ili kupata habari zaidi kuhusu malaika, ona sura ya 10 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? na pia nyongeza kuhusu habari hiyo yenye kichwa “Malaika Mukubwa Anayeitwa Mikaeli Ni Nani?” Kitabu hicho kimechapishwa na Mashahidi wa Yehova. Kinapatikana pia kwenye www.jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine