Tujitoe Kwa Moyo Wa Kujipendea
1 Mtunga zaburi Daudi alitabiri kwamba watu wa Yehova ‘wangejitoa wenyewe kwa moyo wa kujipendea,’ ni kusema wangekubali “haraka kwa kujipendea.” (Zab. 110:3, nota) Ni yale bila shaka yanayotimia katika ushirika wa ulimwenguni pote wa akina ndugu. Muda wa kila moja ya miaka minne ya nyuma ya utumishi, watu wa Yehova waliweza kufanya zaidi ya bilioni moja ya saa katika kujulisha habari njema ya Ufalme. Kwa upande mwingine, zaidi ya kazi ya kuhubiri na ile ya kufanya wanafunzi tunao uwezekano mwingi wa sisi kujitoa kwa moyo wa kujipendea ili kumsaidia jirani yetu.
2 Mambo Katika Hayo Tunaweza Kujitoa kwa Moyo wa Kujipendea: Inawezekana kwamba washiriki fulani wa kutaniko wako na lazima ya msaada ili kujielekeza kwenye mikutano. Kwa nini kutokuwaomba kwenda pamoja nasi? Wengine labda ni wagonjwa, vilema au wenye kulazwa hospitalini. Je! tunaweza kuchukua mipango ili kuwatembelea au kuwasaidia kwa namna moja au nyingine? Ndugu au dada, au tena familia, anahitaji labda vitia moyo. Je! tulifikiria kumwalika kujiunga kwenye funzo letu la familia wakati fulani fulani? Painia au mhubiri anahitaji labda kwamba mtu fulani amshindikize katika mahubiri. Kwa nini kutokumuomba kujiunga naye katika utumishi? Tazama mambo fulani katika hayo tunaweza kutenda kwa kujipendea yaliyo mema kuelekea wale walio jamaa zetu katika imani.—Gal. 6:10.
3 Ndugu wanaweza kuonyesha nia yao ya kutumiwa katika tengenezo la Yehova kwa kujikaza kutimiza matakwa yanayoombwa kwa wazee na watumishi wa huduma. (1 Tim. 3:2-10, 12, 13; Tito 1:5-9) Kwa kuwa sisi ni wengi zaidi na zaidi, tuna lazima ya ndugu wenye kustahili ambao ni tayari kutoa kielelezo katika kazi ya kuhubiri na kufundisha, na pia katika utendaji wa uchungaji wa makutaniko.—1 Tim. 3:1.
4 Wamoja kati yetu labda wana uwezekano wa kujitoa zaidi katika utumishi wa Yehova kwa kuwa mapainia wasaidizi mara kwa mara. Au tena, kwa kuleta mabadiliko yenye kufaa katika matumizi yetu ya wakati, labda tunaweza kuwa mapainia wasaidizi kwa ukawaida au mapainia wa kawaidia. Je! hali yetu ingetuwezesha kwenda katika eneo ambako uhitaji ni mwingi zaidi? Je! tunaweza kuwa tayari kutumikia Betheli na kuchangia hivyo moja kwa moja kuendeleza kazi ya ulimwenguni pote? Kazi kubwa inatimizwa kuhusiana na ujenzi wa Majumba ya Ufalme, Majumba ya makusanyiko na Betheli ulimwenguni, na hilo linahitaji hesabu kubwa ya wafanyakazi wa kujipendea. Wale wanaojitoa kwa moyo wa kujipendea ili kushiriki katika utendaji huo mbalimbali wanathaminiwa sana na wanabarikiwa kwa uwingi.—Lu. 6:38.
5 Tunaishi kipindi chenye kusisimua. Kwa njia ya roho yake, Yehova anatimiza kazi ya ajabu duniani kupitia watumishi wake wa kujipendea! Kila mara, kupitia tengenezo lake, Yehova anapotualika kujitoa zaidi katika utendaji wa Ufalme, tungetenda vema kujiuliza: ‘Je! ninajitoa sikuzote kwa moyo wa kujipendea?’ Kisha tungepaswa kuchunguza katika sala moyo wetu na hali yetu. Ushikamanifu wetu kwa Mungu utatusukuma kufanya yote tuwezayo katika utumishi mtakatifu, tukifurahisha hivyo kikamilifu moyo wa Yehova.—Sef. 3:17.