Mikutano Ya Utumishi Ya Januari
Juma Toka Januari 6
Wimbo 134
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15: “Nani Atasikiliza Ujumbe Wetu?” Kwa maulizo na majibu. Tia ndani mawazo yanayotokana na Amkeni! ya Machi 8, 1988, uku. 5, kwa kuonyesha katika hali gani ujumbe wetu ni wenye kuvutia.
Dak. 20: “Neno la Mungu Linatuongoza.” (Maf. 1-6) Fanya utangulizi wa kipindi kwa msaada wa mafungu 1-2. (Tumia pia kitabu Kutoa Sababu, uku. 40-1, ili kukazia kwa kifupi nne ya “Sababu za Kutufanya Tuichunguze Biblia.”) Onyesho la vielelezo vinavyopendekezwa katika mafungu 3-6 na wahubiri wenye uwezo. Uliza wasikilizaji kusema (1) jinsi maulizo yanayoulizwa yanavyoamsha kupendezwa, (2) ni katika njia gani maandiko yanayotumiwa yalilingana na habari iliyozungumziwa, (3) jinsi ulizo la michango lilivyotajwa, (4) ni katika njia gani ziara ya kurudia ilikuwa mfuatio wenye kupangwa vizuri kiakili wa mazungumzo ya kwanza na (5) jinsi funzo lilivyotolewa.
Wimbo 75 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 13
Wimbo 100
Dak. 5: Matangazo. Hali ya akaunti.
Dak. 20: “Msaada Katika Wakati Ufaao.” Kwa maulizo na majibu. Toa mawazo ya lazima ya kila kimoja cha vichapo vipya.
Dak. 20: “Neno la Mungu Linatuongoza.” (Maf. 7-9). Eleza kichwa kidogo cha habari “Uhitaji wa Mwongozo” katika Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1993, uku. 3. Sema kwa nini utoaji wetu habari ungepaswa kukazia umuhimu wa kutafuta msaada wa mtu aliye juu zaidi: Mungu. Omba mhubiri mmoja kutoa kwa njia ya onyesho vielelezo vya mafungu 7-8. Tia mkazo kwamba kusudi letu la mwisho lingepaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia kwa msaada wa kitabu Ujuzi.
Wimbo 197 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 20
Wimbo 209
Dak. 10: Matangazo. “Mikutano ya Hali ya Juu.” (Maf. 1-12) Mazungumzo pamoja na wasikilizaji.
Dak. 15: “Tujitoe kwa Moyo wa Kujipendea.” Kwa maulizo na majibu. Toa maelezo fulani kutokana na Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1984, uku. 17.
Dak. 20: “Tufurahie Ongezeko Ambalo Mungu Anatutolea.” Hotuba yenye shauku inayotolewa na mzee. Kwa msaada wa Vitabu-Mwaka vya mwisho mwisho, taja mambo yaliyoonwa au toa shuhuda za ongezeko katika nchi zinazozungumziwa ndani.
Wimbo 41 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 27
Wimbo 223
Dak. 10: Matangazo. “Mikutano ya Hali ya Juu.” (Maf. 13-18)
Dak. 20: “Tushiriki Katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.” Hotuba inayotolewa na mwangalizi wa shule. Onyesha hesabu ya wanaojiandikisha na tia moyo wote wale wanaoweza kushiriki shule kujiandisha. Kuhusu vipindi vya wanafunzi, chunguza maagizo yanayopatikana katika “Programu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1997.”
Dak. 15: Vichapo tutakavyotolea mnamo Februari. Tutatolea kitabu chochote cha kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1984. Ikiwa kutaniko halina navyo katika stoki, tumieni kitabu Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. Sema ni vitabu gani kutaniko lilivyo navyo. Chagua viwili au vitatu ambavyo vitafaa kwa eneo lenu. Kwa msaada wa kitabu Kutoa Sababu, kur. 9-15, chunguzeni kwa kifupi matangulizi yanayofaa kwa kila kitabu. Tayarisheni onyosho moja au mawili.
Wimbo 166 na sala ya mwisho.