Utasema nini kwa Mbuddha?
1 Katika nchi fulani, zaidi ya nusu ya wale wanaobatizwa ni wenye kutokana na malezi ya Kibuddha. Ni nini kinachovuta watu hao kwenye kweli? Unawezaje kueleza habari njema kwa Mbuddha?
2 Onyesha kupendezwa kwa kweli: Wengi waliokuwa Wabuddha walisema kwamba si kufikiri kwenye kina kirefu ndiko kuliwavuta kwenye kweli. Badala yake, waliguswa na kule kupendezwa binafsi kwa kweli ambako walionyeshwa. Mwanamke mmoja Mwasia anayeishi katika Amerika aliguswa sana na hali yenye urafiki ya dada aliyemtembelea hivi kwamba alikubali funzo. Hangeweza kusema Kiingereza vizuri, lakini dada alikuwa mvumilivu. Wakati mwanamke huyo alipokuwa mwenye kuchoka au alipokuwa hawezi kujifunza, dada yule alikuwa tu akimtembelea kirafiki na kufanya mipango kwa ajili ya kipindi cha funzo kitakachofuata. Mwishowe mwanamke huyo, wana wake wawili, na mama yake mzee-mzee walibatizwa. Yeye alirudi katika nchi alikozaliwa na alisaidia wengine wengi kujifunza kweli. Mmoja wa wana wake sasa ni mwenye kutumikia kwenye ofisi ya tawi. Ni baraka kama nini zilizotokana na kuonyesha sifa za Yehova, yaani ‘fadhili na upendo kwa ajili ya binadamu’!—Tito 3:4.
3 Wazo la Kibuddha: Kwa kawaida Wabuddha hukubali mawazo mengine, lakini hawaoni kuwa jambo la lazima kushikamana na imani moja yenye kujulikana. Kwa hiyo, imani zao hutofautiana. Kichwa cha habari cha kawaida katika sehemu moja ya fundisho la Kibuddha ni kwamba maisha ni yenye kujaa mateso, lakini kupitia mwangaza wa elimu, mtu anaweza kusimamisha ule mzunguko wenye kuendelea wa kuzaliwa upya katika maisha yasiyotosheleza. Wanasema kwamba ili kuwekwa huru kutoka mzunguko huo, mtu anapaswa kufikia Nirvana, yaani hali ambayo haiwezi kuelezwa kwa kuwa hiyo si mahali au tukio lakini, badala yake, ni mahali palipo tupu ambapo hakuna mateso wala maovu. (Ona Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?, kurasa 9-10.) Jambo hilo linatujulisha nini? Kwamba kuingiza watu katika shindano la maneno juu ya falsafa ya Kibuddha kungekuwa jambo lenye kuzuia matokeo mazuri. Badala yake, zungumzieni matatizo ya kawaida yanayosumbua watu wote.
4 Kazia mambo yenye kupendeza wote: Kwa kuwa Wabuddha kwa kawaida huona maisha duniani kuwa ni mateso, wazo la uhai udumuo milele duniani lingeonekana kwao kuwa lisilo na maana. Hata hivyo, sisi sote tunayo ile tamaa ya kuwa na maisha ya familia yenye furaha, kuona mateso yakimalizwa, na kujua maana ya uhai. Ona jinsi mahitaji hayo ya watu wote yanavyoweza kuelezwa.
5 Unaweza kujaribu utangulizi ufuatao:
◼ “Leo tunaishi katika ulimwengu ambamo watu wengi wasio na kosa lolote huteseka. Je, unaamini kwamba kutakuwako mwisho wa mateso na taabu kwa ajili ya watu wote? [Acha mtu ajibu.] Kuna ahadi ya zamani ambayo hunifariji sana. [Soma Ufunuo 21:4.] Bila shaka, wakati huo haujakuja bado, lakini huo utakapofika, sisi tungetaka kuuona, sivyo?” Kisha, tolea mtu kichapo kinachofasiria jinsi mateso yatakavyokwisha.
6 Kwa mtu mzee-mzee, unaweza kusema:
◼ “Labda wewe ni mwenye kuhangaishwa kama mimi kuhusu wingi wa mawazo yenye kushusha na matokeo ambayo hayo ni yenye kuwa nayo juu ya watoto wetu. Kwa nini kuna ongezeko kama hilo la ukosefu wa adili kati ya vijana? [Acha mtu ajibu.] Je, ulijua kwamba jambo hilo lilitabiriwa katika kitabu kilichoanza kuandikwa wakati mrefu kabla ya dini za Kiislamu, Kikristo na Kihindu kuanzishwa? [Soma 2 Timotheo 3:1-3.] Ona kwamba hali hizo ni zenye kuenea pote ijapokuwa watu wana elimu nyingi. [Soma mstari 7.] Kichapo hiki kilinisaidia kuelewa kweli ambayo watu wengi zaidi hawajifunzi kamwe. Je, ungetaka kukisoma?” Tolea mtu kichapo au broshua yenye kupatana na habari mliyozungumzia.
7 Kwa kawaida Wabuddha huheshimu Biblia kuwa maandishi matakatifu. Hivyo, soma moja kwa moja katika Biblia. (Ebr. 4:12) Ikiwa mtu ni mwenye wasiwasi juu ya uvutano wa utamaduni wa Magharibi, mwambie kwamba waandikaji wote wa Biblia walikuwa watu wa Asia.
8 Ni vichapo gani vilivyo vyenye matokeo zaidi? Ikiwa yenye kutangazwa zaidi kwa ajili ya Wabuddha, trakti Will Suffering Ever End? imechapwa katika Kichina, Kijapani, Kisinhali, na Kithailand. Kwa kuongezea, wahubiri wengi wametumia kwa matokeo vichapo vifuatavyo: vitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia, Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, na Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi; broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” na Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?; na, ikiwa bado inapatikana, trakti Habari za Ufalme No 35, Je! Kuna Wakati Ambao Watu Wataweza Kupendana? Wabuddha wengi wanaojifunza kweli sasa hujifunza kwanza broshua Anataka na kisha kitabu Ujuzi.
9 Ingawa wamishonari Wabuddha wanasemwa kuwa walifika Athene karibu miaka 400 kabla ya Paulo kuhubiri huko, hakuna uhakika kwamba yeye alikutana wakati wowote na mtu aliyepatwa na uvutano wa wazo la Kibuddha. Hata hivyo, tunajua jinsi Paulo alivyojisikia kuhusu kutoa ushahidi kwa watu wa aina zote. Alijifanya mwenyewe “mtumwa kwa wote” ili ‘apate kwa vyovyote kuokoa wengine.’ (1 Kor. 9:19-23) Tunaweza kufanya vivyo hivyo kwa kuonyesha kupendezwa kwa binafsi na watu, na kwa kukazia tumaini tulilo nalo sote wakati tunapotoa ushahidi kwa kila mtu tunayekutana naye.