Utoaji Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
Weka
Jinsi ya Kutumia Nyongeza Hii
Hesabu kubwa ya utoaji mbalimbali wenye kufuata ilitokea katika matoleo yaliyopita ya Huduma Yetu ya Ufalme. Jaribu utoaji mwingi zaidi unavyotaka katika kazi yako ya kutoa ushahidi, na uone matokeo utakayopata. Weka akiba nyongeza hii, na uiendee unapojitayarisha kwa ajili ya huduma.
Unaweza kufanya mtu apendezwe na Neno la Mungu ikiwa unasema moja kwa moja lile unalotaka kusema. Tokeza ulizo fulani, kisha usome jibu fupi la Kimaandiko. Unaweza kujaribu mapendekezo haya:
“Unapofikiria wakati ujao, je, unajisikia mwenye tumaini au mwenye mashaka? [Acha mtu ajibu.] Biblia ilitabiri matukio yenye kutia wasiwasi tunayoona leo na matokeo yayo.”—2 Tim. 3:1, 2, 5; Mez. 2:21, 22.
“Kuna hangaiko kubwa leo kuhusu matunzo ya kiafya. Je, unajua kwamba Mungu anaahidi ya kuwa atamaliza matatizo yote ya kiafya kwa njia yenye kudumu?”—Isa. 33:24; Ufu. 21:3, 4.
“Je, unajua kwamba Biblia inatabiri kwamba kutakuwa mwishowe serikali moja tu itakayotawala ulimwengu wote?”—Dan. 2:44; Mt. 6:9, 10.
“Unafikiri hali zingekuwa namna gani ikiwa Yesu Kristo angetawala dunia?”—Zab. 72:7, 8.
“Watu wengi hupatwa na ubaguzi kwa sababu ya kuwa mume au mke, kwa sababu ya dini, au rangi ya ngozi. Unafikiri Mungu anawaza nini kuhusu ubaguzi kama huo?”—Mdo. 10:34, 35.
“Tunajua kwamba Yesu Kristo alifanya miujiza mingi katika siku yake. Ikiwa ungeweza kumwomba afanye muujiza mmoja wa zaidi, huo ungekuwa muujiza gani?”—Zab. 72:12-14, 16.
“Watu wengi wamechoka kusikia kuhusu matatizo. Wanataka kusikia kuhusu utatuzi. Lakini ni wapi tunapoweza kupata utatuzi wa kweli wa matatizo yetu?”—2 Tim. 3:16, 17.
“Je, unaweza kusema ule Ufalme unaoomba katika Sala ya Bwana (au, Baba Yetu) ni nini?”—Ufu. 11:15.
[Picture on page 3]
Maneno ya Kuanzisha Mazungumzo
Orodha ya maulizo iliyo hapa chini, iliyokusanywa kutokana na vichwa vya habari katika kitabu Kutoa Sababu, inaonyesha ukurasa katika kitabu hicho ambako kila jibu linapatikana:
Je, dini zote zinakubalika kwa Mungu? (67)
Mtu anawezaje kujua dini iliyo ya kweli? (73)
Kwa nini tunazeeka na kufa? (100)
Ni nini iliyo hali ya wafu? (101)
Sababu gani Mungu anaruhusu kuteseka? (132)
Je, watu wema wote wanaenda mbinguni? (189)
Je, ni lazima mtu aende mbinguni ili awe na wakati ujao wenye furaha kwelikweli? (190)
Je, kuna sababu zenye kufaa za kuamini kwamba kuna Mungu? (218)
Je, Mungu kweli anajali yale yanayotupata sisi wanadamu? (219)
Je, Mungu ni mtu halisi? (220)
Ni nini kinachoweza kusaidia kufanya ndoa iwe bora? (246)
Shetani ni mtu mwenye nguvu jinsi gani katika ulimwengu wa leo? (287)
Ufalme wa Mungu utatimiza nini? (327)
Ni nini lililo kusudi la uhai wa kibinadamu? (341)
Ni nani anayetawala ulimwengu huu—Mungu au Shetani? (359)
Kwa nini kuna uovu mwingi sana? (369)
Kwa nini ni jambo la maana kujua na kutumia jina la kibinafsi la Mungu? (422)
Je, Yesu Kristo ni Mungu hakika? (430)