Ninaona Namna Gani Sehemu za Damu na Namna Mbalimbali za Matunzo Zinazoomba Kutumia Damu Yangu Mwenyewe?
Biblia inaamuru Wakristo “wajiepushe . . . na damu.” (Mdo. 15:20) Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova wanakataa kutiwa damu mishipani, iwe damu yenyewe au sehemu kuu zayo ine zifuatazo: chembe nyekundu (globules rouges), chembe nyeupe (globules blancs), vigandisha damu (plaquettes) na plazima (plasma). Hawakubali pia kuwapatia wagonjwa wengine damu au kuchunga damu yao katika chombo fulani kwa muda ili kuirudisha tena ndani ya mwili.—Law. 17:13, 14; Mdo. 15:28, 29.
Sehemu za damu ni nini, na kwa nini kila Mkristo anapaswa kuamua ikiwa atazikubali au kuzikataa?
Sehemu za damu ni visehemu vilivyo katika damu ambavyo vinatenganishwa kupitia ufundi wa kugawanya damu. Kwa mfano, plazima ambayo ni moja kati ya zile sehemu kuu ine za damu, inaweza kugawanywa tena katika visehemu vidogovidogo zaidi kama ifuatavyo: maji, karibu 91%, proteini, karibu 7%, kama vile albumini, globulini, fibrinojeni, na vitu vingine kama vile virutubishi (nutriments), hormoni, gesi (gaz respiratoires), vitamini, takataka za nitrojeni (déchets azotés) na elektroliti (électrolytes) vinafanyiza karibu 1,5%.
Je, amri ya kujiepusha na damu inahusu pia visehemu hivyo vya damu? Hakuna jibu lililo wazi kwa ulizo hilo. Biblia haitoi mwongozo ulio wazi kuhusu habari ya visehemu vya damu.a Kwa kweli sehemu nyingi zinatokana na damu ambayo watu wengine wametoa kwa ajili ya matunzo. Kila Mkristo anapaswa kuamua kulingana na zamiri yake ikiwa atakubali au kukataa matunzo ya kiganga yanayoomba kutumia visehemu hivyo vya damu.
Unapoamua kuhusu mambo hayo, fikiria maulizo yafuatayo: Je, ninajua kwamba kukataa sehemu kuu zote za damu kunamaanisha kwamba nitakataa dawa fulani, kama vile dawa zenye kugombanisha virusi (virus) na magonjwa au zile zinazosaidia kugandisha damu ili isivuje? Je, ninaweza kufasiria mganga kwa nini ninakubali au kukataa matumizi ya sehemu fulani za damu?
Kwa nini mimi peke ndiye nitaamua ikiwa nitakataa au kukubali matunzo fulani ya kiganga yanayoomba kutumia damu yangu mwenyewe?
Ijapokuwa Wakristo hawakubali kupatia watu damu yao au kuchunga damu yao katika chombo fulani kwa muda ili kuirudisha tena ndani ya miili yao wenyewe, kanuni za Biblia hazikataze waziwazi matumizi fulani yanayoomba kutumia damu ya mtu mwenyewe au kuichukua ili kupima kuwapo kwa jambo fulani katika mwili. Kwa hiyo, kila mtu anapaswa kuamua kulingana na zamiri yake ikiwa atakubali au kukataa aina mbalimbali za matunzo zinazoomba kutumia damu yake mwenyewe.
Unapofanya maamuzi hayo, ujiulize maulizo yafuatayo: Ikiwa kiasi fulani cha damu kitaongozwa inje ya mwili wangu kwa kusafirishwa katika vyombo vya kiganga na huenda mtiririko ukasimamishwa kwa muda, je, zamiri yangu itaniruhusu kuona damu hiyo kuwa ingali bado sehemu ya mwili wangu, na hivyo isihitajiwe ‘kumwagwa kwenye udongo’? (Kum. 12:23, 24) Je, zamiri yangu iliyofundishwa na Biblia haitavurugwa ikiwa, wakati wa matunzo fulani ya kiganga, kiasi fulani cha damu yangu kinachukuliwa, kinabadilishwa na kurudishwa tena mwilini mwangu? Je, ninajua kwamba kukataa aina zote za matunzo zinazoomba kutumia damu yangu mwenyewe kunamaanisha kwamba ninakataa aina ya matunzo kama vile kuondoa uchafu katika damu (dialyse) au kutumia moyo au mapafu iliyotengenezwa na watu (cœur-poumon artificiel)? Je, nimefikiria sana jambo hilo katika sala mbele ya kuamua?b
Mimi mwenyewe nitaamua namna gani?
Chunguza karatasi mbili za maulizo na majibu kwenye kurasa zinazofuata. Karatasi 1 inaonyesha sehemu fulani za damu na jinsi zinavyotumiwa mara nyingi katika matunzo ya kiganga. Chagua wewe mwenyewe ikiwa utakubali au kukataa matumizi ya sehemu hizo za damu. Karatasi 2 inaonyesha aina za matunzo ya kiganga zenye kujulikana zinazoomba kutumia damu yako mwenyewe. Chagua wewe mwenyewe ikiwa utakubali au kukataa aina hizo za matunzo. Karatasi hizo si hati za kisheria (documents légals), lakini unaweza kutumia majibu yako yaliyo kwenye karatasi hizo ili kukusaidia kujaza kadi yako ya kiganga DPA (Instructions médicales/Désignation d’une personne de confiance).
Unapaswa kuamua wewe mwenyewe na usitegemee zamiri ya mtu mwingine. Vivyo hivyo mtu hapaswi kusema vibaya kuhusu maamuzi ya Mkristo mwingine. Kuhusu mambo hayo, “kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe.”—Gal. 6:4, 5.
[Vielezi-chini]
a Habari za kusaidia kuhusu jambo hilo zinapatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 2004 (15/6/2004), ukurasa wa 29-31.
b Habari zenye kusaidia kuhusu jambo hilo zinapatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15, 2000, (15/10/2000), ukurasa 30-31, na DVD yenye kichwa Des alternatives à la transfusion — Documentaires.
[Kisanduku kwenye ukurasa wa 5]
Karatasi ya Maulizo na Majibu 1
MAMBO YASIYOKUBALIWA UAMUZI WAKO MWENYEWE
NA WAKRISTO
DAMU Maamuzi Ambayo
YOTE SEHEMU ZA DAMU Unaombwa Kufanya
PLAZIMA ALBUMINI—INAFANYIZA
KARIBU 4% YA PLAZIMA
Albumini ni proteini inayochu-
kuliwa katika plazima. Aina
nyingine za albumini zinapati-
kana katika mimea, chakula
kama vile maziwa na mayayi na
katika maziwa ya mama anayenyo-
nyesha. Wakati mwingine, albumini
inayochukuliwa katika damu ․․ Ninakubali
inatumiwa pamoja na vitu vina- albumini
vyoongeza kiasi cha damu ili au
kutunza mtu anayepoteza damu ․․ Ninakataa
nyingi au aliye na vidonda albumini
vikali vya moto. Mchanganyiko
huo (maana yake vitu vinayoo-
ngeza kiasi cha damu na albumini)
unaweza kuwa karibu 25% ya
albumini. Kiasi kidogo sana
cha mchanganyiko huo kinatumiwa
kufanya dawa nyingine nyingi,
kama vile dawa inayoitwa
érythropoïétine (EPO).
PROTEINI ZA KINGA—(IMMUNOGLOBULINES)
ZINAFANYIZA KARIBU 3% YA PLAZIMA
Ni sehemu za proteini zinazoweza
kutumiwa katika dawa fulani
zinazogombanisha virusi (virus) ․․ Ninakubali
na magonjwa kama vile dondakoo proteini
(diphtérie), pepo punda (tétanos), za kinga
uvimbe wa maini (hépatite) au
na wazimu wa imbwa (rage). ․․ Ninakataa
Zinaweza pia kutumiwa ili proteini
kujikinga na hali fulani zina- za kinga
zoweza kuharibu mimba na kutunza sumu ya nyoka au ya buibui.
VIGANDISHA DAMU—HAVIFIKIE
1% YA PLAZIMA
Kuna proteini nyingi zinazosaidia ․․ Ninakubali
kugandisha damu ili isiendelee vigandisha
kuvuja. Proteini fulani zinapewa damu
wagonjwa wenye kuvuja damu kwa vinavyo-
vyepesi.Zinatumiwa pia pamoja tokana na
na dawa za gundi (colle) ili damu
kugandisha vidonda na kuzuia au
damu isivuje sana kisha upasuaji. ․․ Ninakataa
Mchanganyiko mmoja wa vigandisha vigandisha
damu hivyo unapatikana kwa kuga- damu
ndisha na kisha kuyeyusha plazima vinavyo-
(cryoprécipité). Tangazo: Vigandisha tokana na
damu fulani vinatengenezwa kutokana damu
na dawa zisizofanyizwa na damu.
CHEMBE NYEKUNDU HEMOGLOBINI—INA 33% YA CHEMBE NYEKUNDU
Hemoglobini ni proteini inayosa-
firisha hewa safi (oxygène) katika
mwili wote na kubeba hewa chafu ․․ Ninakubali
(gaz carbonique) kwenye mapafu. hemoglobini
Dawa zinazofanywa kutokana na au
hemoglobini za mtu au za mnyama ․․ Ninakataa
zinaweza kutumiwa ili kutunza hemoglobini
wagonjwa wanaopungukiwa sana na damu.
HEMU (HÈME)—HAIFIKIE 2% YA CHEMBE NYEKUNDU
Hemu ni proteini inayochukuliwa
katika hemoglobini na inatumiwa
ili kutunza magonjwa ya watu wanao-
zaliwa na matatizo mbalimbali ya ․․ Ninakubali
damu na ambayo watu hawagonjwe hemu
zaidi (yanaitwa porphyries); au
magonjwa hayo yanashambulia mfumo ․․ Ninakataa
wa kusaga chakula (système digestif), hemu
wa neva (système nerveux) na mfumo
wa kuzungusha damu mwilini
(système circulatoire).
CHEMBE NYEUPE INTERFÉRONS—ZINAFANYIZA SEHEMU
NDOGO SANA ZA CHEMBE NYEUPE
Ni proteini zinazogombanisha ․․ Ninakubali
magonjwa yenye kutokana na vi- interférons
rusi na kansa (cancers). zinazotokana
Nyingi kati ya proteini hizo na damu
hazitokane na damu. Zingine au
zinafanyizwa na sehemu ․․ Ninakataa
za chembe nyeupe za damu ya mtu. interférons zinazotokana
na damu
VIGANDISHA DAMU Mpaka sasa hakuna sehemu za
vigandisha damu zinazotenga-
nishwa ili kutumiwa katika
matunzo ya kiganga.
[Kisanduku kwenye ukurasa wa 6]
KARATASI YA MAULIZO NA MAJIBU 2
UAMUZI WAKO MWENYEWE
AINA ZA MATUNZO ZINAZOOMBA KUTUMIA DAMU YAKO MWENYEWE
*Tangazo: Kila mganga ana namna yake mwenyewe ya kutumia matunzo hayo. Unapaswa kuomba mganga wako akufasirie vizuri ni mambo gani yanayoombwa katika kila aina ya matunzo anayokupendekeza, ili uhakikishe kwamba inapatana na kanuni za Biblia na maamuzi yako yanayoongozwa na zamiri yako.
JINA LA MATOKEO YA Maamuzi Ambayo
MATUNZO MATUNZO HAYO Unaombwa Kuchukua
(Labda utataka
kuongea na mganga
wako mbele ya
kukubali au kukataa
aina yoyote ya
matunzo hayo.)
KUOKOA CHEMBE Aina hiyo ya matunzo
ZA DAMU inapunguza kupotezwa kwa damu.
Wakati wa upasuaji, damu
yenye kuvuja kutoka kidonda
inachukuliwa na mfumo wa
kutembeza damu hiyo. ․․ Ninakubali
Damu inasafishwa au ku- ․․ Ninaweza
chujwa, na kisha inarudi- kukubali*
shwa tena katika mwili wa ․․ Ninakataa
mgonjwa labda kwa kutumia
vyombo vinavyoitembeza bila
kusimamishwa.
MCHANGANYIKO Aina hiyo ya matunzo
WA CHEMBE-DAMU inapunguza kupotezwa kwa damu.
Wakati wa upasuaji, damu
inaelekezwa katika vyombo
vya kiganga; umajimaji fulani
usio na damu unatiwa mwilini ․․ Ninakubali
mwa mgonjwa mahali pa ile damu. ․․ Ninaweza
Hivyo, damu inayobaki mwilini kukubali*
mwa mgonjwa wakati wa upasuaji ․․ Ninakataa
inachanganywa na ule umajimaji
na inakuwa na kiasi kidogo cha
chembe nyekundu. Wakati wa
upasuaji au mwishoni, ile damu
iliyoelekezwa katika vyombo
vya kiganga inarudishwa tena
katika mwili wa mgonjwa.
MOYO AU MAPAFU Inasaidia kuendelesha
ILIYOTE- usafirishaji wa damu.
NGENEZWA Damu inaelekezwa katika moyo ․․ Ninakubali
NA WATU au mapafu iliyotengenezwa na ․․ Ninaweza
watu, na humo inachukua hewa kukubali*
safi na kurudishwa tena katika ․․ Ninakataa
mwili wa mgonjwa.
KUONDOA UCHAFU Aina hiyo ya matunzo
KATIKA DAMU inatumika kama kiungo
cha mwili. Wakati wa matunzo ․․ Ninakubali
hayo, damu inasafirishwa ․․ Ninaweza
kupitia mashine inayoichuja kukubali*
na kuisafisha mbele ya kuiru- ․․ Ninakataa
disha katika mwili wa mgonjwa.
KUINGIZA KIASI Inasaidia kusimamisha kuvuja
FULANI CHA DAMU kwa umajimaji wa uti wa mgongo.
KWENYE UTI WA Kiasi kidogo cha damu ya ․․ Ninakubali
MGONGO KWA mgonjwa kinaingizwa ndani ․․ Ninaweza
KUTUMIA SHINDANO ya ngozi nyepesi inayofunika kukubali*
uti wa mgongo. Waganga ․․ Ninakataa
wanafanya hivyo ili kuziba
tundu linalofanya umajimaji
wa uti wa mgongo uvuje.
KUTENGANISHA Inatunza magonjwa.
PLAZIMA Wanaongoza damu inje ya
mwili na kuichuja ili
kuondoa plazima. Plazima
nyingine inatiwa mahali ․․ Ninakubali
pa ile inayoondolewa, ․․ Ninaweza
kisha damu inarudishwa kukubali*
ndani ya mwili wa mgonjwa. ․․ Ninakataa
Waganga fulani wanaweza
kutumia plazima ya mtu
mwingine ili kuitia mahali
pa ile ya mgonjwa. Ikiwa
mganga anataka kufanya hivyo,
Mkristo hatakubali jambo hilo.
KUCHANGA DAMU Inasaidia kutambua magonjwa
NA VITU VYENYE au kuyatunza. Kiasi fulani cha
KUNUNURISHA damu kinachukuliwa katika mwili
wa mgonjwa, kinachangwa na dawa ․․ Ninakubali
na kisha kinarudishwa katika ․․ Ninaweza
mwili wa mgonjwa. Muda ambao kukubali*
damu hiyo itafanya inje ya ․․ Ninakataa
mwili wa mgonjwa unaweza kuto-
fautiana kulingana na hali.
KUTUMIA DAMU Inagandisha vidonda, inazuia
YA MTU MWENYEWE damu isivuje. Kiasi fulani cha
ILI KUFANYA damu kinachukuliwa na kukolezwa
MCHANGANYIKO WA kupitia mchanganyiko wa viga- ․․ Ninakubali
KIASI CHA ndisha damu na chembe nyeupe za ․․ Ninaweza
VIGANDISHA DAMU damu. Mchanganyiko huo unatumiwa kukubali*
NA CHEMBE NYEUPE kwenye kidonda cha upasuaji au ․․ Ninakataa
vidonda vingine. Tangazo: Wakati
mwingine waganga wanatumia viga-
ndisha damu kutoka damu ya ngombe
ili kufanya mchanganyiko huo.