SURA YA 7
Mungu Anauona Uzima Kuwa Kitu cha Bei: Halafu Wewe?
“Kwako wewe iko chemchemi ya uzima.”—ZABURI 36:9.
1, 2. Mungu ametupatia zawadi gani ya bei sana, na sababu gani zawadi hiyo ni ya lazima sana?
BABA yetu wa mbinguni ametupatia zawadi ya bei sana: ametupatia uzima na pia ametuumba na akili ili tuweze kuiga sifa zake. (Mwanzo 1:27) Kwa hiyo, tuna uwezo wa kufikiri namna kanuni za Biblia zinavyotufaidi. Tukizitumia, tunaweza kukomaa kiroho na kuwa watu wanaomupenda Yehova na wanaotumia “nguvu zao za ufahamu [ambazo] zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.”—Waebrania 5:14.
2 Leo ni jambo la lazima sana kujua kanuni za Biblia, kwa sababu dunia imekuwa na mambo mengi na haiwezekane kuwa na sheria inayosemea kila hali tunayoweza kukutana nayo katika maisha. Kwa mufano, matunzo ya kiganga, zaidi sana matunzo na ufundi unaoomba kutumia damu. Ikiwa tunaelewa vizuri kanuni za Biblia juu ya jambo hilo, tunaweza kumutii Yehova na kuchukua maamuzi ya hekima yasiyosumbua zamiri yetu, na jambo hilo litatusaidia tubaki katika upendo wa Mungu. (Methali 2:6-11) Acha tuzungumuzie kanuni fulani.
UZIMA NA DAMU NI VITU VITAKATIFU
3, 4. Ni wakati gani kwa mara ya kwanza, Yehova alionyesha kama damu ni kitu kitakatifu, na ni kanuni gani zinazoonyesha jambo hilo?
3 Muda mufupi tu kisha Kaini kumuua Abeli, Yehova alionyesha kwa mara ya kwanza kama uzima na damu vinatembea pamoja. Mungu alimuambia Kaini: “Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika udongo.” (Mwanzo 4:10) Machoni pa Yehova, damu ya Abeli ilimaanisha uzima wake ambao Kaini alikatiza kwa kumushambulia. Kwa hiyo, tunaweza kusema damu ya Abeli ilikuwa inamulilia Mungu ili ailipishie kisasi.—Waebrania 12:24.
4 Kisha Garika ya siku za Noa, Mungu aliwaruhusu wanadamu wakule nyama, lakini aliwakataza kula damu. Aliwaambia: ‘Isipokuwa tu nyama pamoja na nafsi yake—damu yake—musikule. Na, tena, damu ya nafsi zenu nitaitaka.’ (Mwanzo 9:4, 5) Amri hiyo ni kwa ajili ya wazao wote wa Noa mupaka leo. Inarudilia yale Mungu alitaka kumuambia Kaini, ni kusema, unaposema damu, unamaanisha uzima wa kila kiumbe. Tena, amri hiyo inaonyesha kama uzima umetoka kwa Yehova; basi, wanadamu wote wasioheshimu uzima na damu watatoa hesabu kwake.—Zaburi 36:9.
5, 6. Sheria ya Musa ilionyesha namna gani kama damu ni kitu kitakatifu na chenye bei sana? (Soma pia kisanduku “Kuheshimu Uzima wa Wanyama.”)
5 Sheria ambayo Mungu alimupatia Musa ilionyesha pia mambo hayo mawili. Andiko la Mambo ya Walawi 17:10, 11 linasema: ‘Na mutu yeyote atakayekula namna yoyote ya damu, nitauweka uso wangu zidi ya nafsi hiyo inayokula damu, nami hakika nitamukatilia mbali kutoka katikati ya watu wake. Kwa maana nafsi ya mwili iko katika damu, nami mwenyewe nimeiweka juu ya mazabahu ili ninyi mufanye upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu, kwa sababu damu ndio hufanya upatanisho kupitia nafsi iliyo ndani yake.’a—Soma kisanduku “Damu Ina Nguvu ya Kufanya Upatanisho,.”
6 Sheria ya Mungu ilionyesha wazi kama ikiwa damu ya munyama aliyechinjwa haikutumiwa kwenye mazabahu, ilipaswa kumwangwa chini kwenye udongo. Hivyo, kwa njia ya mufano, uzima ulirudishwa kwa Mupaji wa uzima. (Kumbukumbu la Torati 12:16; Ezekieli 18:4) Hilo halimaanishe kama Mungu aliomba Waisraeli wajaribu kuondoa kila alama ya damu katika nyama. Lakini, ikiwa tu munyama angechinjwa vizuri, na damu yake kumwangwa, Muisraeli angeweza kula nyama hiyo kwa zamiri safi, kwa sababu angekuwa amemuonyesha Mupaji wa uzima heshima anayostahili.
7. Daudi alifanya nini ili kuonyesha kwamba aliheshimu damu kwa sababu ni kitu kitakatifu?
7 Daudi, aliyekuwa “mutu anayekubalika kwa moyo wa [Mungu],” alielewa sheria inayotegemea kanuni hiyo ya Mungu. (Matendo 13:22) Siku moja alisikia kiu sana, wanaume wake watatu walifanya nguvu, wakaingia katika kambi ya maadui, wakachota maji katika tangi, na wakamuletea. Daudi alifanya nini? Aliuliza hivi: “Je, ninywe damu ya watu wanaoenda kwa kuhatarisha nafsi zao?” Daudi aliona kama akikunywa maji hayo itakuwa kama amekunywa damu ao uzima wa wanaume hao. Kwa hiyo, hata ikiwa alikuwa na kiu, ‘aliyamwanga mbele za Yehova.’—2 Samweli 23:15-17.
8, 9. Je, mawazo ya Mungu juu ya uzima na damu yalibadilika wakati kutaniko la Kikristo lilianza? Fasiria.
8 Miaka 2400 hivi kisha Noa kupewa amri juu ya damu, na karibu miaka 1500 kisha Mungu kufanya Agano la Sheria na Waisraeli, Yehova aliongoza baraza linaloongoza la kutaniko la Kikristo la kwanza kuandika hivi: ‘Roho takatifu na sisi wenyewe tumependelea tusiwaongezee ninyi muzigo zaidi, ila mambo haya ya lazima: kuendelea kujiepusha na vitu vilivyotolewa zabihu kwa sanamu na damu na vitu vilivyonyongwa, na uasherati.’—Matendo 15:28, 29.
9 Ni wazi kama ndugu wa baraza hilo walitambua kama damu ni kitu kitakatifu na kuitumia isivyofaa ni vibaya sana, ni kama vile kuabudu sanamu ao kufanya uasherati. Leo, Wakristo wa kweli wanaona mambo hivyohivyo. Tena, kwa sababu wao wanaheshimu kanuni za Biblia, wanaweza kumupendeza Yehova wakati wanachukua maamuzi juu ya matumizi ya damu.
MATUMIZI YA DAMU KAMA DAWA
Namna gani ninaweza kuelezea munganga uamuzi wangu juu ya matumizi ya visehemu vya damu?
10, 11. (a) Mashahidi wa Yehova wanaona namna gani kutiwa damu katika mwili ao kutiwa zile sehemu ine kubwa-kubwa za damu? (b) Wakristo wanaweza kuwa na mawazo tofauti kuhusu ufundi gani wa matumizi ya damu?
10 Mashahidi wa Yehova wanatambua kama ‘kujiepusha na damu’ kunamaanisha kuwa damu haipaswe kutiwa katika mwili; wanaepuka kupana damu yao ili itiwe katika mwili wa mutu mwengine, ao kuchunga damu yao pembeni ili kuirudisha tena katika mwili wao. Tena, kwa sababu wanaheshimu sheria ya Mungu, hawakubali sehemu ine kubwa-kubwa za damu: chembe nyekundu (globules rouges), chembe nyeupe (globules blancs), vigandisha-damu (plaquettes), na plazima (plasma).
11 Leo, kupitia ufundi fulani, mara nyingi sehemu hizo kubwa-kubwa zinaweza kugawanywa katika sehemu ndogo-ndogo na kutumiwa katika njia mbalimbali. Je, Mukristo anapaswa kuona sehemu hizo kuwa “damu”? Kila Mukristo atajiamulia mwenyewe. Atajiamulia pia kuhusu ufundi unaoitwa hémodialyse: damu inafyonzwa na kupitishwa kaika mashini iliyo kama figo ili kuisafisha na kumurudishia tena mugonjwa damu hiyo yake. Ufundi mwengine unaitwa récuperation du sang épanché: damu inayovuja wakati wa upasuaji inachukuliwa, inasafishwa, na kisha inarudishwa tena katika mwili. Mukristo anaweza kukubali ufundi huo ikiwa tu damu yake haikuchungwa kwanza mahali fulani ili wamutie damu hiyo tena.—Soma Nyongeza “Visehemu Vidogo-vidogo vya Damu na Ufundi wa Waganga.”
12. Namna gani tunapaswa kuona na kushugulikia mambo yanayotegemea zamiri ya kila mutu?
12 Je, ni kusema Yehova hahangaikie jambo hilo la uamuzi wa pekee ambao Mukristo anapaswa kuchukua? Jibu ni hapana. Yehova anahangaikia sana mawazo yetu na sababu zinazotuchochea kufanya jambo fulani. (Methali 17:3; 21:2; 24:12) Kwa hiyo, Mukristo anapaswa kwanza kusali na kutafuta maelezo zaidi juu ya dawa fulani ao ufundi fulani wa kutunza, na anapaswa kusikiliza zamiri yake iliyofundishwa na Biblia. (Waroma 14:2, 22, 23) Juu ya jambo hilo, hakuna Mukristo anayepaswa kukuambia ufanye hivi ao vile kulingana na zamiri yake, wala wewe pia haupaswe kuuliza wengine ulizo kama vile, “Ingelikuwa wewe ungelifanya nini?” Katika mambo haya, kila Mukristo anapaswa “kuubeba muzigo wake mwenyewe.”b—Wagalatia 6:5; Waroma 14:12; soma kisanduku “Je, Ninaiona Damu Kuwa Kitu Kitakatifu?”
SHERIA ZA YEHOVA ZINAONYESHA UPENDO WAKE
13. Sheria na kanuni za Yehova zinaonyesha nini juu yake? Toa mufano.
13 Sheria na kanuni za Biblia zinaonyesha kama Yehova ni Mupaji wa sheria mwenye hekima na Baba mwenye upendo anayehangaikia sana watoto wake. (Zaburi 19:7-11) Hata kama amri ya ‘kujiepusha na damu’ haikutolewa kwa sababu ya matunzo, inatuchunga tusipatwe na matatizo yanayotokana na kutiwa damu. (Matendo 15:20) Kwa kweli, siku hizi waganga wengi wanaona upasuaji bila kutumia damu kuwa ‘njia nzuri zaidi’ ya kutunza. Wakristo wa kweli wanaona mawazo hayo mapya ya waganga kuwa ushuhuda unaoonyesha waziwazi hekima ya Yehova isiyo na kipimo na upendo wake.—Isaya 55:9; Yohana 14:21, 23.
14, 15. (a) Namna gani Mungu alionyesha kama anawapenda watu wake? (b) Namna gani unaweza kutumia kanuni ambazo sheria hizo zinategemea?
14 Sheria nyingi ambazo Mungu aliwapatia Waisraeli zinaonyesha kama Mungu anapenda watu wake wawe salama. Kwa mufano, Mungu alisema kama paa ao dari za nyumba za Waisraeli zilipaswa kuwa na ukuta wa kukinga ili mutu asianguke kutoka huko; kwa sababu Waisraeli walikuwa wakifanyia mambo mengi kwenye paa ao dari ya nyumba. (Kumbukumbu la Torati 22:8; 1 Samweli 9:25, 26; Nehemia 8:16; Matendo 10:9) Tena Mungu alitoa sheria kama ngombe-dume ambao ni hatari wachungwe vizuri. (Kutoka 21:28, 29) Ikiwa mutu angepuuza maagizo hayo angeonyesha kabisa kama haheshimu uzima wa wengine na angeweza kuwa na deni la damu.
15 Sheria hizo zinategemea kanuni fulani. Namna gani unaweza kutumia kanuni hizo? Unaweza kufikiria hali ya motokari yako ao pikipiki yako, namna yako ya kutembeza, wanyama unaofuga, nyumba yako, mahali pako pa kazi, na namna yako ya kujifurahisha? Katika inchi fulani, aksida zinaua vijana wengi, kwa sababu mara nyingi wao wenyewe wanajihatarisha. Lakini, vijana wanaotaka kubaki katika upendo wa Mungu wanaona uzima kuwa kitu cha bei sana na wanaepuka michezo inayoweza kuhatarisha maisha yao hata ikiwa michezo hiyo inawafanya watu wapate raha fulani. Wao si kama vijana wapumbavu wanaofikiri kwamba kwa sababu mutu ni kijana, basi, hawezi kupatwa na shida yoyote ao kuumia. Lakini, wanafurahia ujana wao na wanajiepusha na misiba.—Mhubiri 11:9, 10.
16. Ni kanuni gani ya Biblia inayokataza kutosha mimba? (Soma pia maelezo yaliyo chini.)
16 Hata uzima wa mutoto ambaye hajazaliwa ni wenye bei machoni pa Mungu. Zamani katika Israeli, ikiwa mutu fulani angemuumiza mwanamuke mwenye mimba, na mwanamuke huyo anakufa ao mutoto wake, Mungu aliona mutu yule kuwa muuaji, na alipaswa kulipa “nafsi kwa nafsi.”c (Kutoka 21:22, 23) Leo, wanawake wengi sana wanatosha mimba kimakusudi ili kuepuka kazi ya kulea mutoto ao kuepuka kuwa na mutoto mwengine. Wengi kati ya wanawake hao wanafanya hivyo kisha kuishi maisha machafu ao kwa sababu wanataka waendelee na maisha hayo. Wakati Yehova anaona mambo hayo anachukizwa sana.
17. Namna gani unaweza kumufariji mwanamuke aliyewahi kutosha mimba mbele ya kujifunza sheria za Mungu?
17 Basi, tunawaza nini juu ya mwanamuke ambaye alitosha mimba mbele ya kujifunza kweli ya Biblia? Je, inamaanisha kama Yehova hawezi kumuhurumia? Sivyo hata kidogo! Kwa kweli, mutu anayetubu kabisa anaweza kutumainia musamaha wa Yehova unaotegemea damu ya Yesu iliyomwangwa kwa ajili yetu. (Zaburi 103:8-14; Waefeso 1:7) Kristo yeye mwenyewe alisema hivi: ‘Nimekuja kuwaita, si watu waadilifu [ao wenye haki], bali watenda-zambi watubu.’—Luka 5:32.
EPUKA CHUKI!
18. Kulingana na Biblia, ni nini inayowafanya watu wamwange damu sana?
18 Yehova haseme tu kwamba tuepuke kuwafanyia wengine mambo mabaya, lakini anataka tuondoe kabisa katika mioyo yetu sababu inayowafanya watu wamwange damu sana, ni kusema, chuki. Mutume Yohana aliandika hivi: ‘Kila mutu anayemuchukia ndugu yake ni muuaji.’ (1 Yohana 3:15) Mutu anayechukia ndugu yake hakose tu kumupenda ndugu yake, lakini anamutakia pia kifo. Uadui huo unaweza kuonekana kwa kumusingizia kwa chuki ao kumushitaki kwa uongo; tabia mbaya kama hiyo itamufanya mutu astahili hukumu ya Yehova. (Mambo ya Walawi 19:16; Kumbukumbu la Torati 19:18-21; Mathayo 5:22) Basi, ni jambo la lazima tuondoe kabisa chuki yote inayoweza kuwa katika mioyo yetu!—Yakobo 1:14, 15; 4:1-3.
19. Namna gani mutu anayeongozwa na kanuni za Biblia atafikiria maandiko kama vile Zaburi 11:5 na Wafilipi 4:8, 9?
19 Watu wote wanaoona uzima kama Yehova anavyouona na wanaotaka pia kubaki katika upendo wake wanaepuka namna yote ya jeuri (ao mambo ya kuuana). Andiko la Zaburi 11:5, linasema hivi: ‘Na mutu yeyote anayependa jeuri, nafsi yake [Yehova] hakika inamuchukia.’ Andiko hilo linaonyesha sifa za Mungu, lakini pia ni kanuni inayoweza kuongoza maisha yetu. Linasukuma wale wanaomupenda Mungu kuepuka namna yote ya kujifurahisha inayochochea jeuri. Tena, Biblia inaposema kama Yehova ni “Mungu wa amani,” inawachochea watumishi wake kujaza katika akili na mioyo yao mambo ya kupendeka, yaliyo mema, yanayostahili kusifiwa, na mambo yanayofanya kuwe na amani.—Wafilipi 4:8, 9.
ACHANA NA TENGENEZO LOLOTE LILILO NA DENI LA DAMU
20-22. Kuhusu ulimwengu, Wakristo wana musimamo gani na sababu gani?
20 Kulingana na mawazo ya Yehova, ulimwengu wote wa Shetani una deni la damu. Biblia inafananisha serikali zote za politike za ulimwengu na wanyama-mwitu wakali. Kama munyama mukali asiye na huruma, politike imefanya watu wengi sana wauawe, na pia watumishi wa Yehova wengi. (Danieli 8:3, 4, 20-22; Ufunuo 13:1, 2, 7, 8) Tengenezo la kibiashara na la kisayansi yameshirikiana na serikali za politike, ni kusema, na wanyama-mwitu wenye mamlaka, ili kutengeneza silaha zenye kuogopesha sana; na kwa kufanya hivyo, matengenezo hayo yamejipatia feza nyingi sana. Biblia inaposema kama ‘ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za yule muovu,’ ni kweli kabisa!—1 Yohana 5:19.
21 Kwa sababu wafuasi wa Yesu wao “si sehemu ya ulimwengu” huo wa Shetani, wanajitenga kabisa-kabisa na mambo ya politike na pia mambo ya vita. Kwa hiyo, hawana deni la damu; iwe mutu mumoja-mumoja ao wote kwa ujumla.d (Yohana 15:19; 17:16) Na kwa sababu wanamuiga Kristo, wao hawalipishe kisasi wakati watu wengine wanawatesa. Wanaonyesha maadui zao upendo na kuwaombea.—Mathayo 5:44; Waroma 12:17-21.
22 Zaidi ya yote, Wakristo wa kweli wanaepuka kujiunga na “Babiloni Mukubwa, ni kusema, tengenezo la duniani pote la dini zote za uongo. Tengenezo hilo la kidini limemwanga damu sana kupita tengenzo la kibiashara na la politike. Neno la Mungu linasema kama ‘ndani yake [Babiloni Mukubwa],’ “ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu na ya wale wote ambao wameuawa juu ya dunia.” Kwa hiyo, Biblia inatuonya hivi: “Tokeni kwake, watu wangu.”—Ufunuo 17:6; 18:2, 4, 24.
23. Inamaanisha nini kutoka katika Babiloni Mukubwa?
23 Kutoka katika Babiloni Mukubwa kunamaanisha kuomba waondoe jina lako kati ya majina ya waamini wa dini ya uongo. Inamaanisha pia kuchukia matendo yote mabaya ambayo dini hiyo inaachilia ao inachochea waziwazi, kama vile mambo ya uasherati, kujiingiza katika mambo ya politike, na kufuatia mali kwa pupa. (Zaburi 97:10; Ufunuo 18:7, 9, 11-17) Mara nyingi mambo hayo yanaongoza kabisa kwenye umwangaji wa damu!
24, 25. Ni kwa musingi gani Mungu atamuhurumia mutu aliye na deni la damu na ambaye anatubu, na mupango huo ulilinganishwa na nini wakati wa zamani?
24 Mbele ya kujua dini ya kweli, kila mumoja wetu aliunga mukono ulimwengu wa Shetani, katika njia fulani, na kwa hiyo, tulikuwa na deni la damu kwa kiasi fulani. Lakini, kwa sababu tulibadilisha mwenendo wetu, tuliamini zabihu ya ukombozi ambayo Kristo alitoa, tukajitoa kwa Mungu katika sala, basi, Yehova ametukubali ao kutusamehe na anatupatia ulinzi ili urafiki wetu pamoja naye usiharibike. (Matendo 3:19) Katika Biblia ulinzi huo ulifananishwa na miji ya makimbilio.—Hesabu 35:11-15; Kumbukumbu la Torati 21:1-9.
25 Miji hiyo ilitumiwa namna gani? Ikiwa Muisraeli angemuua mwenzake bila kukusudia, ilimuomba akimbilie katika moja ya miji hiyo. Waamuzi waliostahili walichunguza jambo hilo; ikiwa mutu hakutenda kimakusudi, basi aliruhusiwa kubaki katika muji wa makimbilio mupaka kifo cha kuhani mukubwa. Kisha angeweza kuwa huru kuishi mahali popote alipopenda. Mupango huo muzuri sana ulionyesha rehema ya Yehova na ulionyesha kwamba anaona uzima kuwa kitu cha bei sana! Leo, miji hiyo inalinganishwa na mipango iliyochukuliwa na Mungu, inayotegemea zabihu ya ukombozi ambayo Kristo alitoa, ili kutulinda tusife kwa sababu tulivunja bila kukusudia sheria ya Mungu inayohusu utakatifu wa uzima na damu. Je, unaheshimu mupango huo? Namna gani unaweza kuonyesha kama unauheshimu kabisa? Njia moja ni kwa kuwaalika wengine ili wao pia waje kuingia katika muji wa makimbilio wa mufano, kwa sababu ‘ziki kubwa’ inakaribia sana.—Mathayo 24:21; 2 Wakorintho 6:1, 2.
HUBIRI UJUMBE WA UFALME ILI KUONYESHA KWAMBA UNAHESHIMU UZIMA
26-28. Ni katika njia gani hali yetu inafanana na ile ya nabii Ezekieli, na tunaweza kufanya nini ili tubaki katika upendo wa Mungu?
26 Hali ya watumishi wa Mungu leo inatukumbusha hali ya nabii Ezekieli, ambaye Yehova alituma ili awe kama mulinzi wa nyumba ya Israeli. Mungu alimuambia hivi: “Lazima usikie neno [langu] na kuwapa onyo kutoka kwangu.” Ikiwa Ezekieli angepuuza daraka lake, angekuwa na deni la damu ya watu walioangamizwa wakati muji wa Yerusalemu ulitoa hesabu. (Ezekieli 33:7-9) Lakini, nabii huyo alitii, na kwa hiyo, hakuwa na deni la damu.
27 Leo, tunakaribia mwisho wa ulimwengu muzima wa Shetani. Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova wanaona kwamba wana daraka na pendeleo la kutangaza “siku ya kisasi” ya Mungu, wakati wanatangaza habari njema ya Ufalme. (Isaya 61:2; Mathayo 24:14) Wewe pia unafanya hivyo? Mutume Paulo alichukua kwa uzito daraka lake. Ndio sababu aliweza kusema: “Mimi ni safi kutokana na damu ya watu wote, kwa maana sikuepuka kuwaambia ninyi mashauri yote ya Mungu.” (Matendo 20:26, 27) Ni mufano muzuri kabisa wa kuiga, sivyo?
28 Kwa kweli, ili tubaki katika upendo wa Baba yetu Yehova, haitoshe tu kuwa na mawazo ya Yehova juu ya uzima na damu. Tunapaswa pia kubaki safi, ao watakatifu, machoni pa Yehova kama tutakavyoona katika sura inayofuata.
a Juu ya maneno “nafsi ya mwili iko katika damu,” gazeti moja linasema hivi: “Hata bila kutumiwa kwa njia ya mufano, maneno haya ni ya kweli tu kwa sababu kila chembe ya damu ni ya lazima ili kuishi.”—Scientific American
b Soma Amkeni! ya Mwezi 8, 2006, ukurasa wa 3-12, iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
c Watu wanaofasiria maneno ya Biblia wanasema kama maneno yaliyotumiwa katika Kiebrania yanaonyesha kama “aksida hiyo ni ya wote wawili, mama na mutoto.” Tena, unaposoma andiko hilo utaona kama Biblia haiseme kama hukumu ya Yehova ilitegemea muda ambao kitoto kilifanya katika tumbo la mama yake.
d Soma Sura ya 5, “Namna ya Kuendelea Kujitenga na Ulimwengu.”
e Ili kupata maelezo mengine, soma Nyongeza “Visehemu Vidogo-vidogo vya Damu na Ufundi wa Waganga”.