Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 1-7/07
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAKOLOSAI 1-4
“Muvue Utu wa Zamani, na Muvae Utu Mupya”
Pokea Roho ya Mungu, Hapana Roho ya Ulimwengu
12Utu wangu unaonyesha roho gani? (Soma Wakolosai 3:8-10, 13.) Roho ya ulimwengu inaendeleza matendo ya mwili. (Gal. 5:19-21) Kwa kweli, tunaweza kujua roho yenye iko inatuongoza wakati kunatokea matatizo, kwa mufano wakati ndugu ao dada Mukristo anafanya sawa vile hatuone, anatukasirisha, ao hata anatukosea sana, hapana wakati hakuna matatizo. Zaidi ya ile, roho yenye iko inatuongoza inaweza kuonekana waziwazi wakati tuko siye peke. Ni muzuri tujichunguze kwa kujiuliza hii maulizo: ‘Mu miezi sita yenye imepita, je, tabia zangu zimekuwa sawa za Kristo ao nimerudilia tena tabia fulani za mubaya mu maneno ao mu matendo?’
13Roho ya Mungu inaweza kutusaidia ‘kuvua utu wa zamani pamoja na mazoea yake’ na kuvaa “utu mupya.” Ile itatusaidia kuwa wenye fazili na wenye upendo zaidi. Tutakuwa na muelekeo wa kusamehe wengine kwa moyo wote, hata kama tuko na sababu ya kulalamika. Kama mutu anatukosea hatutomboka kwa “uchungu wenye uovu, hasira, kasirani kali, kufoka, matukano.” Lakini, tutajikaza kuonyesha “huruma nyingi.”—Efe. 4:31, 32.
Je, Umebadilika?
18Ili Neno la Mungu litusaidie kubadilika, tunapaswa kufanya mengi zaidi ya kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida. Watu wengi wanasoma Biblia mara kwa mara na kwa hiyo wamejua mambo mengi ambayo inasema. Pengine umekwisha kukutana na watu kama hao katika mahubiri. Wengine wanaweza hata kurudilia yale ambayo mistari fulani ya Biblia inasema bila hata kuwa na Biblia mukononi. Hata hivyo, hilo haliwasaidie kabisa kubadili mawazo na namna yao ya kuishi. Sababu gani? Ili Neno la Mungu limuchochee mutu na kumusaidia kubadilika, anapaswa kuliruhusu likaziwe kabisa katika moyo wake. (Gal. 6:6) Kwa hiyo, tunahitaji kutumia wakati ili kufikiri sana kuhusu yale tunayojifunza. Ni jambo la maana tujiulize hivi: ‘Je, niko hakika kama hili si fundisho tu la dini? Je, niko hakika kwamba hii ndiyo kweli? Zaidi ya hayo, kuliko tu kufundisha wengine mambo ninayojifunza, namna gani mimi mwenyewe ninaweza kuyatumia katika maisha yangu? Je, niko hakika kwamba Yehova ndiye anayenifundisha mambo haya?’ Kufikiri na kutafakari juu ya maulizo hayo kunaweza kutusaidia tujisikie kuwa karibu na Yehova. Upendo wetu kwake utaongezeka. Mambo tunayojifunza yanapogusa moyo wetu, hilo litatuchochea kufanya mabadiliko.—Mez. 4:23; Lu. 6:45.
19Kusoma Neno la Mungu kwa ukawaida na kutafakari juu yake kutatuchochea tuendelee kufanya yale ambayo labda tumekwisha kufanya kwa kiasi fulani, ni kusema, ‘kuvua utu wa zamani pamoja na mazoea yake, na kujivika utu mupya ambao kupitia ujuzi sahihi unafanywa kuwa mupya.’ (Kol. 3:9, 10) Tutaendelea kuvaa utu mupya ikiwa tunaelewa vizuri yale tunayojifunza na namna tunavyoweza kuyatumia katika maisha yetu. Utu huo mupya utatusaidia tuepuke mitego ya Shetani.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 833 fu. 4-6
Ufalme wa Mungu
“Ufalme wa Mwana Wake Mupendwa.” Mu Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y., siku kumi kisha Yesu kupanda mbinguni, wanafunzi wake walijionea jambo la kuhakikisha kama Yesu ‘ameinuliwa kwenye mukono wa kuume wa Mungu’ wakati Yesu alimwanga roho takatifu juu yao. (Mdo 1:8, 9; 2:1-4, 29-33) “Agano jipya” lilianza kufanya kazi kwa faida yao na wakakuwa washiriki wa kwanza wa ‘taifa jipya takatifu,’ Israeli wa kiroho.—Ebr 12:22-24; 1Pe 2:9, 10; Gal 6:16.
Ile wakati, Kristo alikuwa amekaa ku mukono wa kuume wa Baba yake na alikuwa Kichwa cha kutaniko. (Efe 5:23; Ebr 1:3; Flp 2:9-11) Maandiko inaonyesha kama kuanzia Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y. ufalme wa kiroho wa Yesu ulianza kuongoza wanafunzi wake. Wakati aliandikia Wakristo wa Kolosai, mutume Paulo alisema kama tayari Yesu alikuwa na ufalme. Alisema: “[Mungu] alituokoa kutoka katika mamlaka ya giza na kutuingiza katika ufalme wa mwana wake mupendwa.”—Kol 1:13; ona pia Mdo 17:6, 7.
Ufalme wenye Kristo alikuwa anaongoza kuanzia Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y. ulikuwa ufalme wa kiroho na ulikuwa unatawala Israeli wa kiroho, ni kusema, Wakristo wenye walizaliwa kwa roho ya Mungu juu wakuwe wana wa kiroho wa Mungu. (Yoh 3:3, 5, 6) Wakati wale Wakristo wenye walizaliwa kwa roho watapokea zawadi yao, hawatakuwa tena raia wa dunia wa ufalme wa kiroho wa Kristo, lakini watakuwa wafalme na Yesu mbinguni.—Ufu. 5:9, 10.
w08 15/8 uku. 28 fu. 8
Mambo Makubwa Katika Barua kwa Wagalatia, Waefeso, Wafilipi, na Wakolosai
2:8—“Mambo ya musingi ya ulimwengu” yenye Paulo alionya Wakristo wasidanganywe nayo, njo mambo gani? Ni mambo ya ulimwengu wa Shetani, ni kusema, mambo ao kanuni za musingi zenye zinafanyiza, ao kuongoza ulimwengu wa Shetani. (1 Yoh. 2:16) Ile mambo ni filozofia, kupenda vitu vya kimwili, dini za uongo za ulimwengu, na mambo ingine.
Hotuba
w04 1/5 uku. 19-20 fu. 3-7
3Tufikirie mwaka wa 60 K.K.Y. Mutume Paulo iko mu gereza kule Roma, wamemushitaki kwa uongo kama iko anachochea uasi. (Matendo 24:5; 25:11, 12) Paulo anataja Wakristo tano wenye walimutegemeza: Tikiko, mujumbe wake kipekee wa wilaya ya Asia na ‘mutumwa mwenzake katika Bwana’; Onesimo, “ndugu muaminifu na mupendwa” wa Kolosai; Aristarko, Mumakedonia wa Tesalonike mwenye wakati fulani alikuwa “mateka” pamoja na Paulo; Marko, binamu ya Barnaba mwenye aliandamana na Paulo mu kazi ya umisionere na mwenye aliandika kitabu cha Injili chenye kinaitwa mu jina lake; na Yusto, mumoja wa wale wenye walifanya kazi na mutume Paulo “kwa ajili ya ufalme wa Mungu.” Paulo anasema hivi kuhusu wale Wakristo tano: “Wamekuwa musaada wenye kutia nguvu kwangu.”—Wakolosai 4:7-11, maelezo ya chini.
4Paulo alisifu sana musaada wenye wale marafiki wake waaminifu walimupatiaka. Alitumia neno ya Kigiriki (pa·re·go·riʹa) yenye inatafsiriwa kuwa “musaada wenye kutia nguvu.” Ni mu ile mustari tu njo ile neno inapatikana. Ile neno iko na maana mingi na inatumiwaka zaidi sana kuhusu dawa. Inaweza kutafsiriwa kuwa ‘kitulizo ao faraja.’ Paulo alihitaji kutiwa nguvu vile, na wale wanaume tano walifanya vile.
Juu ya Nini Paulo Alihitaji “Musaada Wenye Kutia Nguvu”?
5Paulo alikuwa mutume, lakini naye alihitaji kutiwa nguvu, hata kama wengine wanaweza kushangalia ile jambo. Ni kweli kwamba Paulo alikuwa na imani ya nguvu, alivumilia kuteswa sana kimwili, ‘kupigwa mara mingi sana,’ “kukaribia kufa mara nyingi,” na mambo ingine ya kuumiza. (2 Wakorinto 11:23-27) Lakini, alikuwa mwanadamu, na wakati fulani wanadamu wote wanahitaji wengine wawafariji na watie nguvu imani yao. Hata Yesu alikuwa na lazima ya faraja na musaada. Usiku wake wa mwisho malaika alimutokea kule Getsemane na “kumutia nguvu.”—Luka 22:43.
6Paulo pia alihitaji kutiwa nguvu. Wakati alifika Roma na iko mufungwa, Wayahudi wenzake hawakumukaribisha muzuri. Kwa ujumla, hawakufurahia ujumbe wa Ufalme. Kisha wakubwa wa Wayahudi kumutembelea Paulo mu gereza, kitabu cha Matendo kinasema: “Wamoja wakaanza kuamini mambo yenye alisema; wengine hawakuamini. Lakini kwa sababu hawakukubaliana kati yao, wakaanza kuondoka.” (Matendo 28:17, 24, 25) Bila shaka, Paulo aliumia sana kuona kwamba hawakusamini fazili zenye hazistahiliwe za Yehova! Alionyesha wazi namna alihuzunika sana kuhusu ile jambo mu barua yenye alikuwa ameandikia kutaniko la Roma miaka fulani mbele: “Niko na huzuni kubwa na maumivu yenye hayaishe katika moyo wangu. Kwa maana ningependa mimi mwenyewe nitenganishwe na Kristo kama mwenye kulaaniwa kwa ajili ya ndugu zangu [Wayahudi], watu wa jamaa yangu kulingana na mwili.” (Waroma 9:2, 3) Lakini, kule Roma alipata waandamani wa kweli na washikamanifu wenye walimutuliza kupitia ujasiri na upendo wao. Walikuwa ndugu zake wa kweli wa kiroho.
7Wale ndugu tano walikuwa je musaada wenye kutia nguvu? Hawakusikia haya kutembelea Paulo hata kama alikuwa mu gereza. Lakini, walimusaidia kwa kupenda, walimufanyia mambo yenye hangeweza kufanya juu alikuwa mufungwa. Kwa mufano, Paulo aliwatuma wapelekee makutaniko mbalimbali barua na maagizo ya mudomo, na walimuletea habari za kumutia moyo kuhusu hali ya ndugu kule Roma na fasi ingine. Inaonekana waliletea Paulo vitu vyenye alihitaji kama vile nguo za kuvaa wakati wa baridi, vitabu vya kukunjwa, na vifaa vya kuandikia. (Waefeso 6:21, 22; 2 Timoteo 4:11-13) Ule musaada wote wenye walimutolea ulitia nguvu na kutia moyo mutume Paulo mwenye alikuwa mufungwa. Ulimusaidia naye aweze kuwa “musaada wenye kutia nguvu” kwa wengine, na hata kwa makutaniko.—Waroma 1:11, 12.
TAREHE 8-14/07
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | 1 WATESALONIKE 1-5
“Muendelee Kutiana Moyo na Kujengana”
“Muwaheshimie Wale Wenye Wanafanya Kazi kwa Bidii Kati Yenu”
12“Kusimamia” kutaniko haiko kufundisha tu, lakini kunatia ndani mambo mingi. Maneno ya Paulo mu 1 Timoteo 3:4 inaonyesha vile. Paulo alisema kama mwangalizi anapaswa kuwa “mwanamume mwenye kusimamia muzuri nyumba yake mwenyewe, mwenye watoto watiifu na wenye kuchukua mambo kwa uzito.” Mu hii andiko, “kusimamia” maana yake kufundisha watoto, kuongoza familia, na kusaidia ‘watoto wakuwe watiifu.’ Wazee wanasimamia kutaniko wakati wanasaidia washiriki wa kutaniko wamutii Yehova.—1 Tim. 3:5.
“Muwaheshimie Wale Wenye Wanafanya Kazi kwa Bidii Kati Yenu”
19Kwa mufano wanakupatia zawadi yenye ilitayarishwa tu juu yako, utafanya nini? Utaitumikisha juu ya kuonyesha kama unaifurahia. Kupitia Yesu, Yehova amekupatia “zawadi katika wanadamu.” Namna gani unaweza kuonyesha kama unafurahia ile zawadi? Kwa kusikiliza kwa uangalifu hotuba zenye wazee wanatoa na kujikaza kutumikisha mashauri yenye wanatoa. Tena unaweza kuonyesha kama unafurahia ile zawadi kwa kutoa maelezo ya muzuri ku mikutano. Unga mukono kazi yenye wazee wanaongoza, sawa vile kazi ya kuhubiri. Kama muzee alikupatia mashauri fulani na ikakusaidia, juu ya nini usimuambie? Usikose pia kushukuru watu wa familia ya muzee, juu kama muzee iko anaweza kufanya mambo mingi mu kutaniko, ni juu watu wa familia yake wako wanaitika kupitisha wakati kidogo naye juu ahangaikie mambo ya kutaniko.
“Tupendane . . . kwa Tendo na Kweli”
13Utegemeze wale wenye kuwa zaifu. Amri hii ya Biblia inaweza kuonyesha ikiwa upendo wetu ni wa kweli: ‘Mutegemeze walio zaifu, mukuwe wenye ustahimilivu [uvumilivu] kuelekea wote.’ (1 Te. 5:14) Hata kama wengi wenye kuwa zaifu wanafikia kuwa na imani yenye nguvu, wengine wako na lazima tuwaonyeshe uvumilivu, na tuendelee kuwategemeza. Tunaweza kufanya hivyo kwa kuzungumuza nao juu ya mawazo ya Maandiko yenye kujenga, kuwaalika ili tuhubiri pamoja nao, ao kuchukua tu nafasi ya kuwasikiliza. Pia, kuliko tu kufikiri kuwa ndugu ao dada fulani iko “nguvu” kiroho ao “zaifu,” tunapaswa kukumbuka kuwa kila mumoja wetu iko na sifa za muzuri na uzaifu wake. Hata mutume Paulo alikubali kwamba alikuwa na uzaifu. (2 Ko. 12:9, 10) Kwa hiyo, sisi wote tuko na lazima ya kutegemezwa na Wakristo wenzetu.
Tufuate Mufano wa Yesu: Tukuwe Wanyenyekevu na Tutendee Wengine kwa Huruma
16Tutumie maneno ya huruma. Ikiwa tunasikilia wengine huruma, tutachochewa kutumia maneno yenye “kuzifariji nafsi zilizohuzunika.” (1 Te. 5:14) Tunaweza kusema nini ili kutia moyo wale wenye kuhuzunika? Tunaweza kuwatia moyo ikiwa tunawaonyesha kupitia maneno yetu kwamba tunawahangaikia kabisa. Tunaweza kuwapongeza kutoka moyoni ili kuwasaidia waone sifa zao nzuri na uwezo wao mbalimbali. Tunaweza kuwakumbusha kwamba, ikiwa Yehova aliwavuta kwa Mwana wake, ni kwa sababu Yehova anawaona kuwa watu wa maana sana. (Yoh. 6:44) Tunaweza kuwatia moyo kwa kuwaonyesha kwamba Yehova anawahangaikia sana watumishi wake “waliovunjika moyo” ao “waliopondwa roho.” (Zb. 34:18) Maneno yetu yenye huruma yanaweza kusaidia wale wenye kuwa na lazima ya kufarijiwa.—Mez. 16:24.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
it-1-F uku. 921 fu. 2
Uasherati
Uasherati ni kosa yenye inaweza kufanya mutu atengwe na kutaniko. (1Ko 5:9-13; Ebr 12:15, 16) Mutume Paulo alieleza kama Mukristo mwenye anafanya uasherati anatendea mwili wake zambi, juu anatumia viungo vyake vya uzazi mubaya. Anaharibisha sana hali yake ya kiroho, anachafua kutaniko la Mungu na anaweza kupata magonjwa yenye inaweza kumuua yenye inatokana na ngono. (1Ko 6:18, 19) Tena, anaumiza ndugu zake Wakristo (1Te 4:3-7) 1) kwa kuingiza uchafu, upumbavu wenye kuzaraulisha, na lawama mu kutaniko (Ebr 12:15, 16); 2) kwa kuchafua mwenendo wa ule mwenye anafanya naye uasherati na, kama hayafunga ndoa, kumufanya aingiake mu ndoa na haiko tena safi; 3) kwa kuchafua jina ya familia yake; na 4) kwa kukosea wazazi, bwana ao muchumba wa ule mwenye anafanya naye uasherati. Kwa mwisho, anakosea Mungu heshima, kwa sababu Mungu njo ataletaka hukumu juu ya ile zambi, hapana mwanadamu mwenye wakati fulani anaweza kukataza usherati na wakati ingine kuukubali.—1Te 4:8.
w15 15/7 uku. 13-14 fu. 14-15
“Ukombozi Wenu Unakaribia”!
14Ni nini itatokea wakati Gogu wa Magogu ataanza kushambulia watumishi wa Mungu? Biblia inasema kwamba Mwana wa binadamu ‘atawatuma malaika zake pamoja na muvumo mukubwa wa tarumbeta, nao watawakusanya pamoja watu wake waliochaguliwa kutoka kwenye zile pepo ine, kutoka mwisho mumoja wa mbingu mupaka mwisho wake mwingine.’ (Marko 13:27; Matayo 24:31) Kazi hiyo ya kukusanya haizungumuzie wakati Wakristo watiwa-mafuta wanachaguliwa kwa mara ya kwanza. Tena, haizungumuzie wakati Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali duniani watatiwa muhuri kwa mara ya mwisho. (Matayo 13:37, 38) Wakristo hao watatiwa muhuri kwa mara ya mwisho muda mufupi tu mbele ya ziki kubwa kuanza. (Ufunuo 7:1-4) Kwa hiyo, kazi hiyo ya kukusanya itafanywa wakati gani? Itafanywa wakati Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali hapa duniani watapata zawadi yao ya kuenda mbinguni. (1 Watesalonike 4:15-17; Ufunuo 14:1) Kazi hiyo ya kukusanya itafanywa wakati fulani kisha tu Gogu wa Magogu kuanza shambulizi lake. (Ezekieli 38:11) Kisha, kama vile Yesu alisema, ‘waadilifu wataangaa kwa uangavu kama jua katika Ufalme wa Baba yao.’—Matayo 13:43.
15Je, hilo linamaanisha kwamba Wakristo watiwa-mafuta “watanyakuliwa”? Watu wengi wenye kujiita kuwa Wakristo wanaamini kwamba Wakristo watachukuliwa kuenda mbinguni wakiwa na mwili wa wanadamu. Pia, wanafikiri kwamba wakati Yesu atarudia kutawala dunia, watamuona na macho ya kimwili. Lakini, Biblia inasema waziwazi kwamba wakati Yesu atarudia, watu hawatamuona na macho ya kimwili. Inasema hivi: ‘Ishara ya Mwana wa binadamu itaonekana mbinguni’ na, Yesu atakuja “juu ya mawingu ya mbinguni.” (Matayo 24:30) Biblia inasema pia kwamba ‘nyama na damu haviwezi kuuriti Ufalme wa Mungu.’ Kwa hiyo, wale wenye wataenda mbinguni watakuwa kwanza na lazima ya ‘kubadilishwa, kwa muda mufupi, kufumba na kufumbua jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho.’ (Ona maelezo ya chini.) (Soma 1 Wakorinto 15:50-53.) Hatutumie neno “kunyakuliwa” ili kuzungumuzia tukio hilo kwa sababu neno hilo linapatana na mafundisho ya uongo ya dini zenye kujiita kuwa za Kikristo. Lakini, Wakristo watiwa-mafuta waaminifu wenye wangali duniani watakusanywa pamoja mara moja.
TAREHE 15-21/07
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | 2 WATESALONIKE 1-3
“Ule Mwenye Kuvunja Sheria Anafunuliwa”
it-1-F uku. 221 fu. 5
Ushikamanifu kwa Mungu
Hapa kuko fumbo, yenye inapingana kabisa na “siri takatifu” ya Yehova. Ni “fumbo la huu uvunjaji wa sheria.” Ilikuwa fumbo kwa Wakristo wa kweli, juu wakati ya Paulo, “ule mwenye kuvunja sheria” hakukuwa anajulikana waziwazi kama kikundi. Hata wakati angeanza kufanya kazi akiwa kikundi, watu mingi hawangemutambua, juu angekuwa anaonyesha kwa inje kama iko na ushikamanifu kwa Mungu lakini na iko anafanya mambo ya mubaya. Kufanya vile ni kuasi, na haiko ushikamanifu wa kweli kwa Mungu. Paulo alisema kama “fumbo la huu uvunjaji wa sheria” lilikuwa tayari limetokea mu siku zake, juu uvunjaji sheria ulikuwa umeanza kuonekana mu kutaniko la Kikristo, na ungefikia kutokeza kikundi cha “ule mwenye kuvunja sheria.” Ku mwisho, ile kikundi ingeharibiwa wakati kuwapo kwa Yesu Kristo kungeonekana wazi. “Ule mwenye kuvunja sheria” alikuwa anaongozwa na Shetani, na angejiinua “juu ya kila mwenye kuitwa mungu ao kitu cha kuabudiwa.” (Kigiriki: sébasma.) Kwa hiyo, ule mupinzani mukubwa wa Mungu, mwenye kuongozwa na Shetani, angedanganya sana watu na kuleta uharibifu juu ya wale wenye wangefuata matendo yake. “Ule mwenye kuvunja sheria” angeweza kudanganya watu mingi juu angekuwa anaonyesha kwa inje kama iko na ushikamanifu kwa Mungu, lakini kumbe ni munafiki.—2Te 2:3-12; ona pia Mt 7:15, 21-23.
it-2-F uku. 255 fu. 7
Uongo
Yehova Mungu “anaacha” watu wenye wanapenda uongo “wapotoshwe ili wafikie kuamini uongo” kuliko kuamini habari njema juu ya Yesu Kristo. (2Te 2:9-12) Mambo yenye ilipataka mufalme Ahabu wa Israeli inaonyesha vile. Manabii waongo walimuhakikishia kama atashinda vita kule Ramoti-Guileadi, lakini Mikaya, nabii wa Yehova, alitabiri kama hatashinda. Kulingana na mambo yenye Mikaya aliona mu maono, Yehova aliruhusu kiumbe kimoja cha kiroho kikuwe “roho ya udanganyifu” mu kinywa cha manabii wa Ahabu. Ni kusema, kile kiumbe cha kiroho kiliwafanya wasiseme kweli, lakini waseme mambo yenye wanataka na yenye Ahabu alipenda kusikia. Hata kama walimuonya, Ahabu alipendelea kusikiliza uongo wa wale manabii na alifikia kupoteza maisha yake.—1Fa 22:1-38; 2Ny 18.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
it-1-F uku 890 fu. 6
Moto
Petro aliandika kama “mbingu zenye ziko sasa na dunia yenye iko sasa vimewekwa pembeni kwa ajili ya moto.” Kulingana na maandiko yenye inatangulia na yenye inafuata, na pia maandiko ingine, inaonekana kama ile moto haiko moto ya kwelikweli, lakini inafananisha uharibifu wa milele. Garika haikuharibu mbingu na dunia ya kwelikweli, lakini iliharibu waovu. Vilevile, wakati Yesu Kristo atakuja na malaika wake wenye nguvu katika moto wenye kuwaka ataleta uharibifu wa milele juu ya waovu na juu ya mupangilio mubaya wa mambo wenye wanapatikana ndani.—2Pe 3:5-7, 10-13; 2Te 1:6-10; ona pia Isa 66:15, 16, 22, 24.
it-1-F uku. 1188 fu. 1
Kuongozwa na Roho
“Maneno Yenye Kuongozwa na Roho”—ya Kweli na ya Uongo. Neno la Kigiriki pneuma (“roho”) liko na maana ya pekee mu maandishi fulani ya mitume. Kwa mufano, mu 2 Watesalonike 2:2, mutume Paulo alishauria ndugu zake wa muji wa Tesalonike wasiache akili yao ivurugwe na “neno lenye liliongozwa na roho [neno kwa neno: “roho”], ao na ujumbe wa maneno, ao na barua yenye inaonekana kama vile imetoka kwetu ya kwamba siku ya Yehova iko hapa.” Ni wazi kama hapa, Paulo anatumia neno pneuma (roho) mu maana ya njia ya kupashana habari, sawa vile “ujumbe wa maneno” ao “barua.” Njo maana maelezo fulani kuhusu Biblia (Theologisch-homiletisches Bibelwerk, Die beiden Briefe Pauli an die Thessalonicher, ya J. P. Lange, 1864, uku. 110) inasema hivi kuhusu lile andiko: “Wakati mutume Paulo anatumia lile neno, anamaanisha wazo la uongo lenye linatokana na roho, utabiri ao unabii wa uongo.” Kitabu Les deux épîtres de saint Paul aux Thessaloniciens, cha C. Masson, (Neuchâtel, 1957, uku. 93, 94), kinasema: “Inaonekana kama maneno na roho, inamaanisha neno lenye liliongozwa na roho, ufunuo [...], sawa vile maneno yenye manabii walikuwa wanasema mu makutaniko ya kwanza-kwanza.” Kwa hiyo, hata kama tafsiri fulani zinatafsiri tu pneuma kuwa “roho” mu ile andiko na mu maandiko ingine, tafsiri zingine zinatumia maneno sawa vile “maneno yenye inaonekana kuwa inafunuliwa na roho” (PV), “ufunuo wa kiunabii” (TOB), “wazo lenye kuongozwa na roho” (Od; Sg) ao “neno lenye liliongozwa na roho” (nwt).
TAREHE 22-28/07
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | 1 TIMOTEO 1-3
“Ndugu, Mujikaze Kufikia Kazi ya Muzuri”
Unaona Lazima ya Kufanya Maendeleo ya Kiroho?
3Soma 1 Timoteo 3:1. Mutume Paulo alipongeza ndugu wenye walikuwa ‘wanajitahidi [kujikaza] kufikia’ kuwa waangalizi. Ili mutu afikie kitu fulani chenye kuwa mbali, anapaswa kujikaza sana ao pengine kunyoosha mukono wake ili kukikamata. Sasa wazia ndugu mwenye anapenda kutimiza sifa zenye kuombwa ili akuwe mutumishi wa huduma. Anatambua kama anapaswa kujikaza sana ili akomalishe zaidi sifa za Kikristo. Kisha, wakati anakuwa mutumishi wa huduma, anaendelea kujikaza kutimiza sifa zenye kuombwa ili akuwe muzee.
km-F 12/78 uku. 4 fu. 7
Wale “Wenye Wanajipatia Wenyewe Sifa ya Muzuri”
7Ni mwepesi kuona juu ya nini Paulo alisema kama wale wanaume “wanajipatia wenyewe sifa ya muzuri.” Haiko kusema wanapandishwa cheo mu kutaniko, sawa vile wengine wanawaza. Lakini, ile maneno inahakikisha kama Yehova na Yesu watabariki watumishi wa huduma wenye “kutumika muzuri.” Tena, kutaniko litawaheshimia na kuwategemeza. Na wanajipatia “uhuru mwingi wa kusema katika imani yenye kuwa katika Kristo Yesu.” Wanatimiza muzuri kazi yao na wanaheshimiwa juu ya kazi yenye wanafanya; imani yao iko nguvu na wanaweza kufundisha mambo yenye wanaamini bila kuogopa lawama.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
it-1-F uku. 980 fu. 2
Vizazi
Kujifunza na kubishana juu ya mambo ya vizazi haikukuwa na maana, na haikukuwa na maana hata zaidi wakati Paulo aliandikia Timoteo. Haikukuwa lazima tena kuweka maandishi ya kuonyesha kizazi cha mutu juu mbele ya Mungu hakukuwa tena tofauti kati ya Muyahudi na Mutu wa Mataifa (Gal 3:28). Tena, maandishi ya vizazi ilikuwa tayari imeonyesha kama Yesu alitokea mu kizazi cha Daudi. Na tena, wakati fulani tu kisha Paulo kutoa ile shauri, Yerusalemu ingeharibiwa, na ile maandishi ya vizazi vya Wayahudi ingeharibiwa pia. Mungu hakuichungaka isiharibiwe. Njo maana Paulo alipenda Timoteo na makutaniko isiache kufanya mambo ya maana na kupoteza wakati mu kutafuta habari na kubishana juu ya vizazi vyao. Kufanya vile haingeongeza kitu ku imani yao. Habari za vizazi zenye ziko mu Biblia zinatosha ili kuonyesha kama Yesu njo Masiya, na ile njo jambo ya vizazi yenye ilikuwa ya maana sana kwa Wakristo. Habari zingine za vizazi zenye ziko mu Biblia zinaonyesha kama Biblia inasemaka kweli, na ile inaonyesha kama Biblia iko na historia ya kweli.
cl uku. 12 fu. 15
“Angalia! Huyu Ndiye Mungu Wetu”
15Jina ingine ya cheo yenye inatumiwa kuhusu Yehova peke yake ni “Mufalme wa umilele.” (1 Timoteo 1:17; Ufunuo 15:3) Inamaanisha nini? Akili yetu ya kidogo haiwezi kuelewa kabisa maana yake, lakini Yehova ni Mungu wa umilele juu hana mwanzo na mwisho. Zaburi 90:2 inasema: “Tangu milele mupaka milele, wewe ni Mungu.” Kwa hiyo, Yehova hayakuwaka na mwanzo; iko pale tangu milele. Njo maana anaitwa “Muzee wa Siku,” juu iko pale tangu milele mbele ya mutu yeyote na mbele ya kitu chochote kukuwa! (Danieli 7:9, 13, 22) Nani njo anaweza kupinga na kusema kama Yehova hana haki ya kuwa Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi?
TAREHE 29/07–4/08
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | 1 TIMOTEO 4-6
“Faida ya Ushikamanifu kwa Mungu na Matokeo ya Mubaya ya Kupenda Feza”
Kujifunza Siri ya Kutosheka
Paulo alikuwa na furaha juu alitosheka na hali yake. Lakini kutosheka maana yake nini? Kwa kifupi, kutosheka maana yake kufurahia vitu vya lazima vyenye mutu iko navyo. Njo maana Paulo aliambia hivi Timoteo, mwandamani wake mu kazi ya kuhubiri: “Hakika, kuko faida kubwa katika ushikamanifu kwa Mungu pamoja na kutosheka. Kwa maana hatukuleta kitu katika ulimwengu, na hatuwezi kutoka na kitu. Basi, kama tuko na chakula na nguo, tutatosheka na vitu hivyo.’—1 Timoteo 6:6-8.
Ona kwamba Paulo alionyesha kama kuko uhusiano kati ya kutosheka na ushikamanifu kwa Mungu. Alitambua kwamba furaha ya kweli inatokana na ushikamanifu kwa Mungu, ni kusema, kutia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza, hapana kufuatia mali ao utajiri. Alikuwa na lazima tu ya “chakula na nguo” juu aendelee kumutumikia Mungu kwa ushikamanifu. Kwa hiyo, Paulo alijua kwamba siri ya kutosheka ni kumutegemea Yehova mu hali zote.
g 6/07 uku. 6
Matokeo ya Kuazimia Kuwa Tajiri
Ni kweli kwamba watu mingi hawakufake juu ya kutafuta mali. Lakini, wanaweza kukosa furaha mu maisha. Pia, maisha yao inaweza kuharibika juu kazi ao matatizo ya pesa inaweza kuwafanya wakuwe na tatizo la kushituka-shituka, kukosa usingizi, kichwa kuuma, ao vidonda vya tumbo—hali zenye zinaweza kuacha mutu anakufa mbio. Tena, pengine mutu anaweza kuvumbula kama inaomba abadishe mawazo yake kuhusu mambo yenye anapaswa kutanguliza mu maisha, lakini pengine itakuwa kuchelewa. Pengine bibi ao bwana yake hamuaminie tena, pengine watoto wake hawamupendi tena, pengine afya yake ilishaharibika kabisa. Pengine mutu anaweza kurekebisha mambo fulani, lakini haiko mwepesi. Watu wenye wanaazimia kuwa matajiri ‘wanajitoboa wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.’—1 Timoteo 6:10.
g 11/08 uku. 6 fu. 4-6
Njia Sita za Kupata Mafanikio
Vile tuliona mu habari ya kwanza, watu wenye wanafuatilia sana utajiri juu wanawaza kama ile njo kufanikiwa, wako wanafuatilia upepo. Zaidi ya kukata tamaa, wanajiletea maumivu mengi. Kwa mufano, mara mingi wakati wako wanatafuta utajiri, wanafikiaka kusahau familia na marafiki. Wengine wanakosa usingizi, hapana tu juu ya kazi, lakini juu ya woga na wasiwasi. Muhubiri 5:12 inasema: “Usingizi wa mutumishi ni mutamu, ikuwe amekula mingi ao kidogo. lakini vitu vingi vyenye tajiri iko navyo havimuruhusu alale.”
Feza ni bwana mubaya, na pia mudanganyifu. Yesu Kristo alizungumuzia “nguvu za udanganyifu za utajiri.” (Marko 4:19) Ile inamaanisha kama utajiri unaahidi mutu kwamba utamupatia furaha, lakini haumupatie ile furaha. Kuliko kufanya vile umufanya mutu atamani utajiri zaidi. Muhubiri 5:10 inasema: “Mwenye anapenda feza hatashiba feza.”
Kwa kifupi, mutu mwenye anapenda feza iko anajiumiza tu. Ku mwisho, atavunjika moyo, atakatishwa tamaa, na hata atafanya mambo ya mubaya. (Mezali 28:20) Kuwa mukarimu, kuwa tayari kusamehe, kuwa na mwenendo muzuri, kupenda wengine, na kuwa na uhusiano muzuri na Mungu njo mambo yenye inaletaka furaha na mafanikio ya kweli.
Chimba Ili Kupata Mali ya Kiroho
Kuwa na Zamiri ya Muzuri Mbele ya Mungu
17Mutume Petro aliandika hivi: “Muendelee kuwa na zamiri ya muzuri.” (1 Petro 3:16) Jambo la kuhuzunisha ni kuwa, wakati watu wanaendelea kuzarau kanuni za Yehova, mwishowe zamiri yao haiwaonye tena ao kuwaonyesha hatari. Paulo alisema kama zamiri kama hiyo imekuwa kama “kovu lenye lilifanywa kwa chuma cha moto cha kutilia alama.” (1 Timoteo 4:2) Umekwisha kuunguzwa mubaya sana na moto? Wakati jambo hilo linatokea, ngozi yako inakuwa yenye kovu sana hivi kwamba hauwezi kusikia kitu chochote ku ile kovu. Ikiwa mutu anaendelea kufanya mambo ya mubaya, zamiri yake inaweza kuwa kama “kovu” na inaweza kufikia kuacha kutumika.
it-2-F uku. 122 fu. 1-2
Kusoma Mbele ya Watu
Mu Kutaniko la Kikristo. Mu karne ya kwanza, haiko kila mutu njo alikuwa na kopi za vitabu vya kukunjwa vya Biblia. Njo maana ilikuwa lazima mutu asomee wengine. Mutume Paulo aliagiza barua zake zisomewe mbele ya watu mu makutaniko ya Kikristo na kwamba wabadilishane barua zenye alitumia makutaniko ingine juu nazo zisomewe. (Kol 4:16 ; 1Te 5:27) Paulo alishauria mwangalizi kijana Timoteo afanye bidii katika “kusoma mbele ya watu, kutia moyo, na kufundisha.”—1Ti 4:13.
Wakati mutu iko anasoma mbele ya watu, anapaswa kusoma bila kukwama-kwama (Hab 2:2). Juu mu mambo yenye atasoma muko mafundisho, anapaswa kuelewa muzuri mambo yenye iko anasoma, kujua sababu gani ile habari iliandikwa na kuwa muangalifu juu asifikie kudanganya wasikilizaji wake. Kulingana na Ufunuo 1:3, wale wenye wanasoma kwa sauti unabii huu, na wale wenye wanasikia maneno na kuitumikisha, watakuwa na furaha.