Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 1 uku. 6-12
  • “Muende, na Mufanye Wanafunzi”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Muende, na Mufanye Wanafunzi”
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kazi ya Maana Sana
  • Habari Fulani Kuhusu Kitabu ya Matendo
  • Hii Kitabu Itatusaidia Kujifunza Biblia
  • “Mupaka Kwenye Sehemu ya Mbali Zaidi ya Dunia”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • “Kutoa Ushahidi Kamili”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • “Mapenzi ya Yehova yatendeke”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
Ona Habari Zaidi
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 1 uku. 6-12

SURA YA 1

“Muende na Mufanye Wanafunzi”

Mawazo makubwa ya kitabu ya Matendo ya Mitume na namna tunaweza kufaidika nayo leo

1-6. Ni mifano gani inaonyesha kama Mashahidi wa Yehova wanahubiri mu hali mbalimbali?

REBECCA, kijana mwanamuke Shahidi wa Yehova mu inchi ya Ghana, aliona masomo yao kuwa eneo yake ya mahubiri. Hakukuwa nakosa vitabu na magazeti wakati alikuwa naenda ku masomo. Wakati wa mapumuziko alikuwa natafuta nafasi za kutolea wanafunzi wenzake ushahidi. Alianza kujifunza Biblia na wanafunzi wengi.

2 Mu kisiwa ya Madagaska yenye kuwa mashariki mwa Afrika, mapainia wawili walizoea kutembea karibu kilometre 25 mu kifukutu sana juu ya kufika mu kijiji moya ya mbali. Kule walikuwa najifunza Biblia na watu wengi wenye kupendezwa.

3 Juu ya kuhubiria watu wenye kuishi pembeni-pembeni ya muto Paraguay na Paraná, Mashahidi wa Yehova wa Paraguay pamoya na Mashahidi wengine kutoka inchi 15 walitengeneza mashua (bateau). Ile mashua ni ya kilo 45 000 na watu 12 wanaweza kuishi ndani. Wahubiri wa Ufalme wenye bidii wanatumia ile mashua juu ya kutangaza habari njema mu maeneo yenye wahubiri hawawezi kufika kwa vyepesi.

4 Mu sehemu ya kaskazini ya Alaska Mashahidi wa Yehova wa mu ile eneo walipata nafasi ya pekee ya kuhubiria wageni wenye walitembelea ile eneo mu kipindi ya kifukutu. Wakati mashua zenye kubeba wale watu kutoka inchi mbalimbali zilikuwa nafika, Mashahidi walikuwa pale na vichapo vyenye kutegemea Biblia vya mu luga mbalimbali. Mu ileile eneo, ndugu walitumia ndege (avion) ili kusafiri mu vijiji vya mbali. Ile ilisaidia kutangazia habari njema watu wa Aleut, Athabascan, Tsimshian, na Tlingit.

5 Larry aliishi mu nyumba ya kutunzia watu wenye kuzeeka katika Texas mu Amerika. Ile nyumba njo ilikuwa eneo yake ya mahubiri. Hata kama alilazimika kutumia kinga ya vilema kwa sababu ya aksida yenye alifanyaka, aliendelea kuwa na bidii mu kazi ya kuhubiri. Alikuwa naambia wengine kuhusu ujumbe wa Ufalme, na kama iko na tumaini ya kutembea tena wakati Ufalme wa Mungu utatawala dunia.​—Isa. 35:5, 6.

6 Kikundi ya ndugu na dada wa Mandalay katika inchi ya Myanmar walifanya safari ya siku tatu kwa mashua ili kuenda kuhuzuria mukusanyiko kaskazini mwa Myanmar. Juu walipenda sana kuhubiri habari njema, walibeba vichapo na walivitolea watu wenye walisafiri pamoya nao. Wakati mashua ilisimama mu muji fulani ao mu kijiji fulani, wale wahubiri wenye bidii walishuka na kuenda haraka kutolea watu wa pale vichapo. Wakati walirudia, walikuta watu wengine wameingia mu mashua. Kwa hiyo, walikuwa na watu wengine wapya wa kuhubiria.

7. Ni njia gani mbalimbali zenye waabudu wa Yehova wanatumia ili kutoa ushahidi juu ya Ufalme wa Mungu, na wako na kusudi gani?

7 Vile ile mifano inaonyesha, waabudu wa Yehova wenye bidii ‘wanatoa ushahidi kamili juu ya Ufalme wa Mungu’ mu dunia yote. (Mdo. 28:23) Wanahubiri nyumba kwa nyumba, mu barabara, kupitia barua, na hata kupitia telefone. Ikuwe wako mu bisi, wakati wanatembea mu bustani, ao wako napumuzika ku kazi, wanatumiaka kila nafasi yenye wanapata ili kutoa ushahidi juu ya Ufalme wa Mungu. Wanatumia njia mbalimbali, lakini wako na kusudi moya tu, ni kusema, kuhubiri habari njema fasi yote kwenye watu wanaweza kupatikana.​—Mt. 10:11.

8, 9. (a) Juu ya nini tunaweza kusema kama ongezeko mu kazi ya kuhubiri Ufalme ni muujiza? (b) Ni ulizo gani yenye tunaweza kujiuliza, na tunaweza kufanya nini ili kupata jibu?

8 Musomaji mupendwa, uko kati ya wahubiri wenye wanatangaza Ufalme mu inchi zaidi ya 235? Kama ni vile, uko nasaidia ili habari njema ifikie watu wengi zaidi mu maeneo mbalimbali! Jambo yenye ile kazi iko natimiza mu dunia yote ni muujiza. Mashahidi wa Yehova wanapataka magumu mbalimbali. Kwa mufano, serikali fulani zinakataza kazi yao na kuwatesa. Lakini wanaendelea kutolea watu wa mataifa yote ushahidi kamili juu ya Ufalme wa Mungu.

9 Pengine mutu anaweza kujiuliza hivi: Juu ya nini hakuna kizuizi yoyote wala upinzani wowote wenye kuchochewa na Shetani wenye umeweza kusimamisha kazi ya kuhubiri Ufalme? Ili kupata jibu, tukumbuke mambo yenye ilitokea wakati wa mitume, juu siye Mashahidi wa Yehova leo tuko naendelesha kazi yenye ilianza ile wakati.

Kazi ya Maana Sana

10. Kazi kubwa mu maisha ya Yesu ilikuwa nini, na alijua nini?

10 Yesu Kristo, Mwenye alianzisha kutaniko ya Kikristo, alihubiri kwa bidii habari njema ya Ufalme wa Mungu. Ile njo ilikuwa kazi kubwa mu maisha yake hapa ku dunia. Wakati fulani alisema: “Ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika miji ingine, kwa sababu nilitumwa ili kufanya vile.” (Lu. 4:43) Yesu alijua kama hangeweza kumaliza yeye peke ile kazi yenye alianzisha. Muda mufupi mbele akufe, alitabiri kama ujumbe wa Ufalme utahubiriwa “katika mataifa yote.” (Mk. 13:10) Ile kazi ingefanywa namna gani, na nani njo wangeifanya?

Ku mulima wa Galilaya, Yesu anapatia mitume na wanafunzi wake kazi ya kufanya

“Muende, na mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.”​—Matayo 28:19

11. Yesu alipatia wanafunzi wake kazi gani ya maana, na wangetegemezwa namna gani?

11 Kisha kufufuliwa, Yesu alitokea wanafunzi wake na kuwapatia hii kazi ya maana sana: “Kwa hiyo, muende, na mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na muwabatize katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na muwafundishe kushika mambo yote yenye nimewaamuru ninyi. Na muangalie! niko pamoja na ninyi sikuzote mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.” (Mt. 28:19, 20) Maneno “niko pamoja na ninyi,” inaonyesha kama Yesu angetegemeza wanafunzi wake mu kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Walikuwa na lazima ya kutegemezwa juu, sawa vile Yesu alitabiri, ‘wangechukiwa na mataifa yote.’ (Mt. 24:9) Tena, kuko jambo ingine yenye ingetegemeza wale wanafunzi. Mbele tu ya kurudia mbinguni, Yesu aliwaambia kama roho takatifu ingewapatia nguvu, na wangekuwa mashahidi wake “mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”​—Mdo. 1:8.

12. Ni maulizo gani inatokea, na juu ya nini majibu ya ile maulizo ni ya maana sana?

12 Sasa, kunatokea maulizo ya maana sana: Mitume wa Yesu na wanafunzi wengine wa karne ya kwanza walikamata ile kazi kwa uzito? Hata kama hawakukuwa wengi, walitoa ushahidi kamili juu ya Ufalme wa Mungu hata wakati walipata mateso makali? Yehova aliwasaidia na kuwategemeza kupitia roho yake takatifu mu kazi yao ya kufanya wanafunzi? Ile maulizo na ingine ya mingi inajibiwa mu kitabu ya Matendo ya Mitume. Ni jambo ya maana sana tupate majibu ya ile maulizo. Juu ya nini? Yesu alisema kama kazi yenye alipatia wanafunzi wake ingeendelea “mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.” Kwa hiyo, ile kazi ingefanywa na Wakristo wote wa kweli, kutia ndani siye wenye kuishi mu siku hizi za mwisho. Njo maana tunapendezwa sana na kitabu ya Matendo.

Habari Fulani Kuhusu Kitabu ya Matendo

13, 14. (a) Nani njo aliandika kitabu ya Matendo, na alipata namna gani habari zenye aliandika? (b) Kitabu ya Matendo inazungumuzia nini?

13 Nani njo aliandika kitabu ya Matendo? Ile kitabu haiseme, lakini mistari kidogo ya kwanza inaonyesha wazi kama muandikaji wa ile kitabu njo aliandika Injili ya Luka. (Lu. 1:1-4; Mdo. 1:1, 2) Kwa hiyo, tangu zamani watu wengi wameamini kama kitabu ya Matendo iliandikwa na Luka, “munganga mupendwa” mwenye alikuwa pia mwanahistoria muangalifu. (Kol. 4:14) Ile kitabu inazungumuzia mambo yenye ilitokea mu kipindi ya miaka 28 hivi, tangu Yesu arudie mbinguni mu mwaka wa 33 mupaka kufungwa kwa mutume Paulo kule Roma mu mwaka wa 61 hivi K.K.Y. Luka anazungumuzia matukio ya mingi ya mu kitabu ya Matendo mu njia yenye kuonyesha kama pengine alikuwa pale, juu anatumia maneno yenye inamutia ndani ya ile matukio. (Mdo. 16:8-10; 20:5; 27:1) Juu Luka alikuwa anapenda kutafuta habari kwa uangalifu, pengine alipata habari moja kwa moja kutoka kwa Paulo, Barnaba, Filipo, na wengine wenye wanatajwa mu habari yake.

14 Ni mambo gani yenye inazungumuziwa mu kitabu ya Matendo? Mu Injili yenye aliandika mbele ya pale, Luka aliandika kuhusu mambo yenye Yesu alisema na kufanya. Lakini, mu kitabu ya Matendo, Luka anaandika kuhusu mambo yenye wanafunzi wa Yesu walisema na kufanya. Kwa hiyo, kitabu ya Matendo inazungumuzia watu wenye walitimiza kazi kubwa, hata kama wengi wao walionwa kuwa watu “wenye hawana elimu na watu wa kawaida.” (Mdo. 4:13) Kwa kifupi, ile kitabu inazungumuzia namna kutaniko ya Kikristo ilianza na namna iliendelea kukomala. Inaeleza njia zenye Wakristo wa wakati wa mitume walitumia ili kuhubiri, na muelekeo wenye walikuwa nao. (Mdo. 4:31; 5:42) Tena, inaonyesha namna roho takatifu ilisaidia wale Wakristo waeneze habari njema. (Mdo. 8:29, 39, 40; 13:1-3; 16:6; 18:24, 25) Kitabu ya Matendo inakazia tungo kubwa ya Biblia, ni kusema, kutakaswa kwa jina ya Mungu kupitia Ufalme wake chini ya utawala wa Kristo. Ile kitabu inaonyesha pia namna habari njema juu ya Ufalme ilihubiriwa hata kama kulikuwa upinzani mukali.​—Mdo. 8:12; 19:8; 28:30, 31.

15. Tutapata faida gani kwa kuchunguza kitabu ya Matendo?

15 Habari zenye kuwa mu kitabu ya Matendo ni zenye kuchochea na zinatia imani nguvu! Kufikiri sana juu ya bidii na uhodari wenye wanafunzi wa Kristo walionyesha mu karne ya kwanza, kutatugusa moyo sana. Kutafanya tuige imani yao juu tukuwe tayari kutimiza kazi yenye tulipewa ya ‘kuenda na kufanya wanafunzi.’ Hii kitabu itakusaidia ujifunze kwa uangalifu kitabu ya Matendo.

Hii Kitabu Itatusaidia Kujifunza Biblia

16. Hii kitabu iko na kusudi gani?

16 Kusudi ya hii kitabu ni nini kabisa? Kusudi ya hii kitabu ni (1) kutusadikisha kama Yehova anatumia roho yake takatifu juu ya kutegemeza kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi, (2) kutuchochea tufuate mufano wa wanafunzi wa Kristo wa karne ya kwanza kwa kuwa na bidii katika kazi yetu ya kuhubiri, na (3) kusamini hata zaidi tengenezo ya Yehova na wale wenye wanaongoza makutaniko na kusimamia kazi ya kuhubiri.

17, 18. Eleza vile hii kitabu imepangwa, na namna itatusaidia mu funzo yetu ya kipekee.

17 Hii kitabu imepangwa namna gani? Utaona kama imegawanywa mu sehemu munane zenye zinazungumuzia sehemu mbalimbali za kitabu ya Matendo. Sura zenye kufuata hazizungumuzie kitabu ya Matendo mustari kwa mustari, lakini zinazungumuzia mambo mbalimbali yenye habari zenye kuwa mu Matendo zinaweza kutufundisha na zinatusaidia kuona namna ya kutumia ile mambo mu maisha yetu. Ku mwanzo wa kila sura kuko maelezo ya mufupi yenye kuonyesha mambo yenye kuzungumuziwa mu ile sura na mistari ya kitabu ya Matendo yenye kuhusika.

18 Hii kitabu iko na mambo ingine yenye inaweza kufanya funzo yetu ya kipekee ikuwe muzuri sana. Muko picha za muzuri zenye kuonyesha mambo yenye kuchochea sana yenye kuwa mu kitabu ya Matendo. Zile picha zitakusaidia uwazie mu akili zile habari za Biblia. Sura mingi ziko na visanduku vyenye kuwa na habari za zaidi. Visanduku fulani vinazungumuzia watu mbalimbali wenye kutajwa mu Biblia wenye tunaweza kuiga imani yao. Visanduku vingine viko na habari za zaidi kuhusu maeneo, matukio, desturi, ao watu wengine wenye kutajwa mu kitabu ya Matendo. Ku sehemu za pembeni kuko fasi kwenye unaweza kuandika mambo ya maana wakati uko unajifunza hii kitabu.

Ndugu iko anapatia ndugu na dada eneo ya kuhubiri

Hubiri eneo yako mu njia yenye kuonyesha kama unatambua kuwa mwisho uko karibu sana

19. Tukuwe najiuliza maulizo gani juu ya kujichunguza?

19 Hii kitabu inaweza kukusaidia ujichunguze. Hata kama ulishakuwa muhubiri wa Ufalme kwa muda gani, ni muzuri mara kwa mara kutua na kuchunguza kwa uangalifu mambo yenye uko unatia pa nafasi ya kwanza mu maisha yako na namna unaona utumishi wa Kikristo. (2 Ko. 13:5) Ujiulize: ‘Namna yangu ya kuhubiri inaonyesha kama ninatambua kuwa mwisho uko karibu? (1 Ko. 7:29-31) Niko nahubiri habari njema kwa usadikisho na kwa bidii? (1 Te. 1:5, 6) Niko nafanya yote yenye ninaweza juu ya kuhubiri na kufanya wanafunzi?’​—Kol. 3:23.

20, 21. Juu ya nini kazi yetu ni ya haraka sana, na tunapaswa kuazimia kufanya nini?

20 Sikuzote, tusisahau kama tulipewa kazi ya maana sana, kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Muda wa kufanya ile kazi unaendelea kupunguka. Mwisho wa huu ulimwengu unakaribia sana. Maisha ya watu wengi iko mu hatari. Hatujue kungali watu ngapi wenye kuwa na muelekeo wenye kufaa, wenye watakubali ujumbe wetu. (Mdo. 13:48) Tuko na daraka ya kusaidia wale watu mbele mwisho ufike.​—1 Ti. 4:16.

21 Tuige basi bidii ya wahubiri wa Ufalme wa wakati wa mitume. Kuchunguza hii kitabu kukuchochee ukuwe na uhodari na bidii zaidi mu kazi ya kuhubiri. Uazimie basi kuendelea “kutoa ushahidi kamili juu ya Ufalme wa Mungu.”​—Mdo. 28:23.

TAREHE ZA MAANA ZENYE KUHUSU KUENEA KWA UKRISTO MU KARNE YA KWANZA

  1. Mwaka wa 33

    Yesu anafufuliwa

    Yesu anapatia wafuasi wake kazi ya kufanya wanafunzi

    Wanafunzi wanapokea roho takatifu siku ya Pentekoste

    Kutaniko ya Kikristo inaanzishwa

  2. Mwaka wa 33-34 hivi

    Stefano anauawa

    Towashi Mwetiopia anabatizwa

  3. Mwaka wa 34 hivi

    Sauli wa Tarso anakuwa mufuasi wa Kristo

  4. Mwaka wa 34-36 hivi

    Sauli anahubiri Damasko

  5. Mwaka wa 36 hivi

    Paulo anatembelea Yerusalemu kwa mara ya kwanza akiwa mufuasi wa Kristo

    Paulo anamutembelea Petro katika Yerusalemu (Gal. 1:18)

  6. Mwaka wa 36

    Kornelio anakuwa mufuasi wa Kristo

    Watu wa kwanza wa mataifa wanakuwa Wakristo

  7. Mwaka wa 41 hivi

    Injili ya Matayo inaandikwa

    Paulo anaona “mbingu ya tatu” mu maono (2 Ko. 12:2)

  8. Mwaka wa 44 hivi

    Agabo anatabiri kuhusu njaa

    Yakobo (mwana wa Zebedayo) anauawa

    Petro anafungwa na anafunguliwa kwa muujiza

  9. Mwaka wa 44

    Herode Agripa wa Kwanza anakufa

  10. Mwaka wa 46 hivi

    Njaa yenye ilitabiriwa inatokea

    Paulo anapeleka makuta na michango ingine Yerusalemu

  11. Mwaka wa 47-48 hivi

    Safari ya kwanza ya umisionere ya Paulo

  12. Mwaka wa 49 hivi

    Tatizo ya kutahiriwa inatokea Antiokia

    Mukutano unafanywa Yerusalemu

    Paulo anamurekebisha Petro (Gal. 2:11-14)

  13. Mwaka wa 49-52 hivi

    Safari ya pili ya umisionere ya Paulo

    Barnaba na Marko wanahubiri Kipro

  14. Mwaka wa 49-50 hivi

    Klaudio anawafukuza Wayahudi Roma

  15. Mwaka wa 50 hivi

    Luka anajiunga na Paulo kule Troa

    Paulo anamuona mwanaume Mumakedonia mu maono

    Paulo anaenda Filipi

    Kutaniko ya Filipi inaanzishwa

    Kutaniko ya Tesalonike inaanzishwa

    Paulo anaenda Atene

  16. Mwaka wa 50-52 hivi

    Paulo anaenda Korinto

    1 Watesalonike inaandikwa

    Wagalatia inaandikwa

  17. Mwaka wa 51 hivi

    2 Watesalonike inaandikwa

  18. Mwaka wa 52-56 hivi

    Safari ya tatu ya umisionere ya Paulo

  19. Mwaka wa 52-55 hivi

    Paulo anaenda Efeso

  20. Mwaka wa 55 hivi

    1 Wakorinto inaandikwa

    Tito anatumwa Korinto

    2 Wakorinto inaandikwa

  21. Mwaka wa 56 hivi

    Waroma inaandikwa

    Paulo anamufufua Eutiko kule Troa

    Paulo na Luka wanakaa kwa Filipo kule Kaisaria

    Paulo anakamatwa kule Yerusalemu

  22. Mwaka wa 56-58 hivi

    Paulo anatiwa mu kifungo kule Kaisaria

    Injili ya Luka inaandikwa

  23. Mwaka wa 58 hivi

    Festo anakuwa gavana kisha Feliksi

  24. Mwaka wa 58

    Herode Agripa wa Pili anamusikiliza Paulo

  25. Mwaka wa 59-61 hivi

    Paulo anafungwa Roma kwa mara ya kwanza

  26. Mwaka wa 60-61 hivi

    Wakolosai inaandikwa

    Waefeso inaandikwa

    Filemoni inaandikwa

    Wafilipi inaandikwa

  27. Mwaka wa 60-65 hivi

    Injili ya Marko inaandikwa

  28. Mwaka wa 61 hivi

    Matendo ya Mitume inaandikwa

    Waebrania inaandikwa

  29. Mwaka wa 61-64 hivi

    1 Timoteo inaandikwa

    Tito anabakia Krete (Tit. 1:5)

    Tito inaandikwa

  30. Mbele ya mwaka wa 62

    Yakobo inaandikwa

  31. Mwaka wa 62-64 hivi

    1 Petro inaandikwa

  32. Mwaka wa 64 hivi

    2 Petro inaandikwa

  33. Mwaka wa 65 hivi

    Paulo anafungwa Roma kwa mara ya pili

    2 Timoteo inaandikwa

    Tito anaenda Dalmatia (2 Ti. 4:10)

    Paulo anauawa

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine