WIMBO 17
“Ninataka”
Maandishi
1. Yesu Kristo alikuya
Kwa sababu ya upendo.
Alisaidia watu wengine
Kwa maneno na matendo.
Aliponyesha wagonjwa,
viziwi, vipofu pia.
Na kwa watu wa hali ya chini
Alisema: “Ninataka.”
2. Tujikaze kumuiga
Kwa kuwapenda wengine.
Tuwahubirie na tusikose
Kuwaonyesha huruma.
Tuwasaidie ndugu
Kwa maneno na matendo.
Kwa mujane na pia yatima,
Tutasema: “Ninataka.”
(Ona pia Yoh. 18:37; Efe. 3:19; Flp. 2:7.)