MAMBO YA KUFANYA WAKATI BITU BINAPANDA BEI
Uitike Hali Vile Iko
Hatuhangaikake sana kama bei ya bitu iko napanda polepole na mishahara nayo iko inaongezeka. Lakini kama bei ya bitu inapanda haraka sana na mishahara inabakia vilevile, ile inaletaka mahangaiko mingi, zaidi sana kama tuko na familia yenye tunapaswa kuhangaikia.
Ujue kama upende usipopenda, bitu binaweza kupanda bei. Njo maana kuitika ile hali vile iko itatuletea faida.
JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA KUITIKA HALI VILE IKO?
Ni juu kama mutu anaitika kama hawezi kuzuia bitu kupanda bei, inakuwaka mwepesi kwake . . .
- kubakia mwenye kutulia. Wakati mutu anatulia, anawaza muzuri na anakamata maamuzi ya muzuri. 
- kuepuka tabia zenye haziko za muzuri. Kwa mufano, hauze bitu byenye hana nabyo lazima na analipa ma faktire pa wakati. 
- kuepuka kukosana na batu ya familia yake juu tu ya makuta. 
- kufikiria mambo yenye anaweza kufanya kama bitu binapanda bei, kwa mufano kuuza tu bitu byenye iko nabyo lazima na kupunguza bitu byenye ananunuaka. 
MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA
Ujipatanishe na hali. Wakati bitu binapanda bei sana, ni muzuri kununua tu bitu kidogo kama inawezekana. Lakini, batu bamoya banapendaka kuendelea kuishi tu vile balikuwaka naishi mbele bitu bipande bei. Ile iko sawa vile mutu mwenye iko naogelea mu mutoni yenye mayi iko nashuka nguvu sana lakini yeye iko napanda kule kwenye mayi iko natokea! Kama anafanya vile, ku mwisho atafikia tu kuchoka! Ni kweli kama ni kawaida kuhangaikia batu ya familia yako na kubapatia mambo yenye biko nayo lazima! Lakini ukumbuke kama, mambo yenye batu ya familia yako biko nayo lazima kuliko kitu ingine yoyote, ni kubaonyesha kama unabapenda, unabahangaikia na unapitisha wakati pamoya nabo.
Kuendelea kuishi tu vile tulikuwaka naishi mbele bitu bipande bei iko sawa vile kuogelea mu mutoni yenye mayi iko nashuka nguvu sana lakini siye tuko napanda tu kule kwenye mayi iko natokea