Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g25 na. 1 uku. 4-5
  • Uitike Hali Vile Iko

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uitike Hali Vile Iko
  • Amuka!—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA KUITIKA HALI VILE IKO?
  • MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA
  • Bei ya Vitu Imepanda mu Dunia Yote—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2025
  • Ukuwe na Tumaini
    Amuka!—2025
  • Utumikishe Makuta Yako Muzuri
    Amuka!—2025
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2025
g25 na. 1 uku. 4-5
Picha: 1. Mwanamuke moya anachagula tomate ku soko. 2. Anapana makuta kwa mwenye kuuzisha.

MAMBO YA KUFANYA WAKATI BITU BINAPANDA BEI

Uitike Hali Vile Iko

Hatuhangaikake sana kama bei ya bitu iko napanda polepole na mishahara nayo iko inaongezeka. Lakini kama bei ya bitu inapanda haraka sana na mishahara inabakia vilevile, ile inaletaka mahangaiko mingi, zaidi sana kama tuko na familia yenye tunapaswa kuhangaikia.

Ujue kama upende usipopenda, bitu binaweza kupanda bei. Njo maana kuitika ile hali vile iko itatuletea faida.

JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA KUITIKA HALI VILE IKO?

Ni juu kama mutu anaitika kama hawezi kuzuia bitu kupanda bei, inakuwaka mwepesi kwake . . .

  • kubakia mwenye kutulia. Wakati mutu anatulia, anawaza muzuri na anakamata maamuzi ya muzuri.

  • kuepuka tabia zenye haziko za muzuri. Kwa mufano, hauze bitu byenye hana nabyo lazima na analipa ma faktire pa wakati.

  • kuepuka kukosana na batu ya familia yake juu tu ya makuta.

  • kufikiria mambo yenye anaweza kufanya kama bitu binapanda bei, kwa mufano kuuza tu bitu byenye iko nabyo lazima na kupunguza bitu byenye ananunuaka.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Ujipatanishe na hali. Wakati bitu binapanda bei sana, ni muzuri kununua tu bitu kidogo kama inawezekana. Lakini, batu bamoya banapendaka kuendelea kuishi tu vile balikuwaka naishi mbele bitu bipande bei. Ile iko sawa vile mutu mwenye iko naogelea mu mutoni yenye mayi iko nashuka nguvu sana lakini yeye iko napanda kule kwenye mayi iko natokea! Kama anafanya vile, ku mwisho atafikia tu kuchoka! Ni kweli kama ni kawaida kuhangaikia batu ya familia yako na kubapatia mambo yenye biko nayo lazima! Lakini ukumbuke kama, mambo yenye batu ya familia yako biko nayo lazima kuliko kitu ingine yoyote, ni kubaonyesha kama unabapenda, unabahangaikia na unapitisha wakati pamoya nabo.

“Ni nani kati yenu mwenye kwa kuhangaika anaweza kuongeza kipimo cha mukono mumoja kwenye urefu wa uzima wake?”—Luka 12:25.

“Basi, musihangaike hata kidogo juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Kila siku iko na matatizo yake yenye yanaeneana na siku hiyo.”—Matayo 6:34.

Kuendelea kuishi tu vile tulikuwaka naishi mbele bitu bipande bei iko sawa vile kuogelea mu mutoni yenye mayi iko nashuka nguvu sana lakini siye tuko napanda tu kule kwenye mayi iko natokea

Phazilya.

“Vile tu Biblia ilisemaka mu 2 Timoteo 3:​1, tunaishi mu “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.” Njo maana, sishitukake wakati inakuwa nguvu kupata makuta wala wakati bitu binapanda bei. Kitu yenye najikazaka kufanya ni kufikiria namna ya kuepuka kupoteza makuta mu mambo yenye haiko ya lazima kabisa.”—Phazilya, Azerbaijan.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine