Musamaha
Yehova anakuwaka natusamehe kwa kiasi gani?
Ona pia 2Pe 3:9
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Zb 78:40, 41; 106:36-46—Yehova anasamehe mara kwa mara watu wake wenye kupotoka, hata kama zambi yao inamuhuzunisha sana
Lu 15:11-32—Yesu anaonyesha namna Yehova anakuwaka nasamehe, kwa kuzungumuzia mufano wa baba mwenye rehema mwenye anatendea muzuri mutoto wake mwenye alikuwa amepotoka lakini akatubu
Yehova alifanyaka nini juu tuweze kupata musamaha wa zambi zetu?
Yoh 1:29; Efe 1:7; 1Yo 2:1, 2
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Ebr 9:22-28—Mutume Paulo anafasiria namna kupitia damu ya Yesu tu njo tunaweza kusamehewa zambi
Ufu 7:9, 10, 14, 15—Mu maono, mutume Yohana anaona “kundi kubwa la watu” wenye wako safi mbele ya Mungu kwa sababu ya damu ya Kristo yenye ilimwangwa
Kama tunapenda Yehova atusamehe, tunapaswa kufanya nini wakati wengine wanatukosea?
Mt 6:14, 15; Mk 11:25; Lu 17:3, 4; Yak 2:13
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Yob 42:7-10—Mbele amalize magumu ya Yobu na kumurudishia afya ya muzuri na utajiri, Yehova anamuomba asali kwanza kwa ajili ya wale marafiki wake tatu wa uongo
Mt 18:21-35—Yesu anakazia kabisa juu ya nini ni lazima tusamehe wengine kama tunapenda kusamehewa
Juu ya nini ni jambo ya maana kuungama na kutubu kikweli?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Zb 32:1-5; 51:1, 2, 16, 17—Juu alifanya zambi nzito, Mufalme Daudi anahuzunika na kuvunjika moyo, kisha anatubu kikweli
Yak 5:14-16—Yakobo anaonyesha kama ikiwa tunafanya zambi nzito tunapaswa kuenda kuona wazee
Tunapaswa kufanya mabadiliko gani kama tunapenda Yehova atusamehe?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
1Fa 21:27-29; 2Ny 18:18-22, 33, 34; 19:1, 2—Wakati Mufalme Ahabu anahukumiwa, anajinyenyekeza na Yehova anamuongezea kiasi fulani ya rehema, lakini hafanye jambo yenye kuonyesha kama ametubu kikweli; kwa hiyo Yehova anaendelea kumuona kuwa muovu na anamuua
2Ny 33:1-16—Mufalme Manase ni muovu sana; lakini Yehova anamusamehe wakati anatubu. Manase anaonyesha kama amebadilika kwa kupiganisha ibada ya uongo na kuunga mukono ibada safi
Ni kwa kiasi gani Yehova anakuwaka nasamehe kama tunatubu kikweli?
Zb 103:10-14; Isa 1:18; 38:17; Yer 31:34; Mik 7:19
Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:
2Sa 12:13; 24:1; 1Fa 9:4, 5—Hata kama Daudi alifanya zambi nzito, Yehova anamusamehe juu alitubu, na kisha anamutaya kuwa mwanaume muaminifu-mushikamanifu
Namna gani Yesu alifuata mufano wa Yehova wa kuwa tayari kusamehe?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mt 26:36, 40, 41—Wafuasi wa karibu sana wa Yesu wanalala usingizi wakati iko na lazima yao kabisa; hata vile Yesu anaelewa kama wako na mipaka
Mt 26:69-75; Lu 24:33, 34; Mdo 2:37-41—Petro anamukana Yesu mara tatu, lakini Yesu anamusamehe juu alitubu; kisha Yesu kufufuliwa, anamutokea na kisha anamupatia madaraka ya pekee mu kutaniko
Tunajua namna gani kama musamaha wa Yehova uko na mipaka?
Mt 12:31; Ebr 10:26, 27; 1Yo 5:16, 17
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mt 23:29-33—Yesu anaonya waandishi na Mafarisayo kama watapata hukumu ya Gehena, ao uharibifu wa milele
Yoh 17:12; Mk 14:21—Yesu anamuita Yuda Iskariote “mwana wa uharibifu” na anasema kama ingekuwa muzuri kama hangezaliwaka