Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/10 uku. 3
  • Sababu Gani Unapaswa Kupendezwa na Biblia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Unapaswa Kupendezwa na Biblia?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Ujifunze Biblia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Biblia Ni Kitabu Chenye Kinaweza Kueleweka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Yehova Mungu, Anazungumuza na Watu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Biblia Ni Neno ya Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/10 uku. 3
[Picha katika ukurasa wa 3]

KICHWA

Sababu Gani Unapaswa Kupendezwa na Biblia?

Biblia ni kitabu ambacho kinapendwa sana na watu wengi duniani. Sababu gani? Sababu moja ni kwamba Biblia inaeleweka kwa vyepesi. Ina habari za kweli juu ya watu ambao waliishi kwelikweli na juu ya uhusiano kati yao wenyewe na kati yao na Mungu. Habari hizo zinafundisha mambo mazuri kwa kutumia maneno mepesi na yaliyo wazi. Maneno hayo yanaweza kutafsiriwa katika luga nyingi na kueleweka kwa watu wa kila mahali na wa vizazi vyote. Na kanuni za Biblia ni zenye kufaa sikuzote.

Jambo la maana zaidi, Biblia inajieleza kuwa kitabu kinachozungumuza juu ya Mungu na pia kilichotoka kwa Mungu. Inaonyesha jina la Mungu, sifa zake, na kusudi lake lisilobadilika ambalo alikuwa nalo alipoumba dunia na wanadamu. Biblia inaeleza pia mapambano ya muda murefu kati ya wema na uovu: habari yenye kuvutia inayohusu ulimwengu wote ambayo mwisho wake utakuwa wenye kufurahisha. Tunaposoma Biblia tukiwa na mawazo mazuri, jambo hilo linatusaidia kuwa na imani na tumaini.

Katika Biblia, tunapata habari ambazo hatuwezi kupata mahali pengine. Kwa mufano, Biblia inatueleza ukweli juu ya habari kama hizi:

  • Uzima wetu ulianza namna gani na sababu gani tunateseka

  • Mipango ambayo Mungu alifanya ili kukomboa wanadamu

  • Mambo ambayo Yesu alifanya kwa ajili yetu

  • Wakati ujao wa dunia na wanadamu

Ni vizuri uchunguze habari zinazofuata na kuona Biblia inazungumuzia habari gani.

MAELEZO MAFUPI JUU YA BIBLIA

  • Kichwa kikuu: Namna Ufalme wa mbinguni wa Mungu utakavyorudisha haki na amani duniani

  • Vitabu vilivyo ndani: Ina vitabu 39 ambavyo viliandikwa katika luga ya Kiebrania (mistari michache iliandikwa katika luga ya Kiaramu) na pia vitabu 27 ambavyo viliandikwa katika luga ya Kigiriki

  • Iliandikwa: Na waandikaji karibu 40 katika kipindi cha miaka 1 600 hivi, kuanzia mwaka wa 1513 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu mupaka mwaka wa 98 kisha kuzaliwa kwa Yesu

  • Luga: Kwa sasa inatafsiriwa ikiwa nzima ao sehemu katika luga zaidi ya 2 500

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine