Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/10 uku. 4
  • Uzima Wetu Ulianza Namna Gani Duniani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uzima Wetu Ulianza Namna Gani Duniani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu Anapenda Wanadamu Wakuwe na Maisha ya Namna Gani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Juu ya Nini Kuko Mateso na Mambo Mingi ya Mubaya?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Mungu Ana Kusudi Gani juu ya Dunia?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Maisha Ilikuwa Namna Gani mu Paradiso?
    Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/10 uku. 4
[Picha katika ukurasa wa 4]

KICHWA | BIBLIA INAZUNGUMUZIA HABARI GANI?

Uzima Wetu Ulianza Namna Gani Duniani?

Kwa kifupi na katika maneno machache, kitabu cha kwanza cha Biblia kinachoitwa Mwanzo, kinaeleza namna ulimwengu ulivyoanza kwa kusema hivi: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” (Mwanzo 1:1) Kisha Mungu kuumba mimea na wanyama, aliumba wanadamu wa kwanza, Adamu na Eva. Walikuwa tofauti na wanyama kwa sababu wanadamu wana sifa za Mungu kwa kiasi fulani, kutia ndani uhuru wa kuchagua. Kwa hiyo, walipaswa kukubali matokeo ya matendo yao. Ikiwa wangetii maagizo ya Mungu, wangechangia katika utimizo wa kusudi la Mungu wakiwa wazazi wa kwanza wa familia ya ulimwenguni pote ya wanadamu ambayo ingefurahia amani na uzima mukamilifu milele duniani.

Lakini, malaika mumoja, ao kiumbe wa roho, alichukua nafasi hiyo ili kutumia wanadamu kwa faida yake mwenyewe. Kwa kufanya hivyo akakuwa Shetani, jina linalomaanisha “Mupinzani.” Akizungumuza kupitia nyoka, Shetani alimudanganya Eva, kwa kumuambia kwamba maisha yake yangekuwa mazuri zaidi bila kuongozwa na Mungu. Adamu na Eva walimufuata Shetani, na hivyo wakavunja uhusiano wao pamoja na Muumbaji wao. Kwa sababu ya uamuzi mubaya, wazazi wetu wa kwanza walipoteza pendeleo la kuishi milele na wakatuambukiza sisi wote zambi, hali ya kutokamilika, na kifo ambacho hatuwezi kuepuka.

Mara moja, Mungu alitangaza nia yake ya kurekebisha hali hiyo mbaya na kuwapa wazao wa Adamu njia ya kupata uzima wa milele. Mungu alitabiri kwamba “uzao,” ni kusema, mutu wa pekee ambaye mwishowe angemuharibu Shetani na kumaliza mateso yote ambayo Shetani, Adamu, na Eva walitokeza. (Mwanzo 3:15) Ni nani angekuwa “uzao” huo? Siku zingesema.

Wakati huohuo, Shetani angejaribu mara kwa mara kuzuia kusudi nzuri la Mungu. Zambi na uovu vilienea haraka sana. Mungu aliazimia kuharibu watu waovu kupitia garika. Alimuagiza Noa mwanaume mwenye haki ajenge safina, ni kusema, sanduku kubwa ambalo lingeelea ao kuenda huku na huku juu ya maji, ili kujiokoa mwenyewe na kuokoa familia yake, pamoja na wanyama ambao aliagizwa kuingiza ndani ya safina hiyo.

Mwaka mumoja kisha Garika, Noa na familia yake walitoka ndani ya safina na kuingia katika dunia iliyosafishwa. Lakini “uzao” ulikuwa bado kutokea.

​—Habari hii inategemea Mwanzo sura ya 1-11; Yuda 6, 14, 15; Ufunuo 12:9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine