Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/10 uku. 7
  • Habari Njema kwa Watu Wote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Habari Njema kwa Watu Wote
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Adresi Yetu ya Internete Inayokubaliwa Kisheria Inatufaidi Sisi na Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Kuhubiri habari njema ukiwa na usadikisho wenye nguvu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/10 uku. 7
[Picha katika ukurasa wa 7]

KICHWA | BIBLIA INAZUNGUMUZIA HABARI GANI?

Habari Njema kwa Watu Wote

Ufufuo wa Yesu uliwafanya wanafunzi wake wawe na usadikisho mwingi na bidii nyingi. Mutume Paulo hasa alisafiri katika Asia Ndogo yote na Mediterania, akiunda makutaniko na kuwatia Wakristo nguvu ili wasimame imara wakati walikazwa kufanya mambo mabaya na wakati walipata upinzani mukali. Ijapokuwa matatizo hayo, Ukristo ulisonga mbele na kuenea kila mahali.

Paulo mwenyewe alitupwa katika gereza. Lakini, hata akiwa katika gereza, aliandikia makutaniko ya Kikristo barua zenye kutia moyo na zenye kuwa na mashauri mazuri. Aliwaonya juu ya hatari kubwa zaidi, ni kusema, uasi-imani. Akiwa mwenye kuongozwa na roho ya Mungu, Paulo aliona mbele ya wakati kwamba “mbwa-mwitu wenye kukandamiza” na wenye kusema “mambo yaliyopotoka” wangeingia katikati yao na “kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.”​—Matendo 20:29, 30.

Mwishoni mwa miaka kati ya 1 na 100, uasi-imani huo ulikuwa umeanza. Karibu na wakati huo Yesu aliyefufuliwa alimupatia mutume Yohana Ufunuo, ishara ya mambo ya wakati unaokuja. Kama vile Yohana alivyoandika wakati huo, iwe wapinzani ao walimu wa uongo hawangeweza kumuzuia Mungu kutimiza kabisa kusudi lake la mwanzoni kwa ajili ya dunia na wanadamu. “Kila taifa na kabila na luga na watu” watasikia habari njema juu ya Ufalme wa Mungu. (Ufunuo 14:6) Paradiso itarudishwa duniani, na kila mutu anayetaka kufanya mapenzi ya Mungu ataishi katika Paradiso hiyo!

Hiyo ni “habari njema” kwako, sivyo? Ikiwa jibu lako ni ndiyo, jifunze mambo mengi zaidi juu ya ujumbe wa Mungu kwa wanadamu ulio katika Biblia na namna ujumbe huo unavyoweza kukufaidi leo na pia wakati unaokuja.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Unaweza kusoma Biblia katika luga karibu 50 kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org. Kwenye adresi hiyo, unaweza pia kusoma broshua Biblia​—Ina Ujumbe Gani? na Habari Njema Inayotoka kwa Mungu! na pia kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Unaweza kusoma kwenye adresi hiyohiyo vichapo vingine vinavyozungumuzia sababu gani unaweza kuamini Biblia, na namna gani tunaweza kutumia mashauri ya Biblia yanayofaa katika familia yetu na katika maisha yetu ya kipekee. Ao ili kuelewa mengi zaidi, unaweza kumuuliza Shahidi yeyote wa Yehova.

​—Habari hii inategemea Matendo, Waefeso, Wafilipi, Wakolosai, Filemoni, 1 Yohana, Ufunuo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine