MUSEMWA WA BIBLIA
Tumikisha “Zawadi ya Kiroho” Yenye Uko Nayo
Siye bote tunatiwa moyo wakati tunapitisha wakati pamoya na bandugu na badada. Lakini haitoshe tu kupitisha wakati pamoya. Kuko mambo ingine yenye tunaweza kufanya juu ya kutiana moyo zaidi. Biblia inaita ule uwezo wa kutiana moyo na kutiana nguvu katika imani, “zawadi ya kiroho.” (Ro. 1:11, 12) Tunaweza kufanya nini ingine juu ya kutiana moyo?
Tia bengine moyo kupitia maneno yako. Kwa mufano, wakati unatoa maelezo ku mikutano, usizungumuzie sana maisha yako na mawazo yako, lakini uzungumuzie mambo yenye unajifunza kutoka kwa Yehova, Neno yake Biblia, na watu wake. Wakati unazungumuza na ndugu na dada, zungumuzia mambo yenye inatia moyo.
Utie bengine moyo kupitia maamuzi na matendo yako. Kwa mufano, wakati unaamua kuendelea na utumishi wa wakati wote hata kama haiko mwepesi, ile inatia bengine moyo. Tena bengine banatiwa moyo wakati banaona unajikaza kufika ku mikutano ya katikati ya juma, hata kama uko na matatizo ya afya ao unachoka sana kwa sababu ya kazi yako.
Maneno yako na matendo yako inatiaka moyo ndugu na dada? Unakubali zawadi za kiroho zenye ndugu na dada banakutolea?