Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 21
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Ayubu ajibu (1-34)

        • ‘Kwa nini waovu wanafanikiwa?’ (7-13)

        • Afichua hila za “wafariji” wake (27-34)

Ayubu 21:3

Marejeo

  • +Ayu 16:10, 20; 17:2; Ebr 11:36

Ayubu 21:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “roho yangu isingekosa.”

Ayubu 21:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuwa na nguvu.”

Marejeo

  • +Hab 1:3, 13
  • +Ayu 12:6; Zb 37:7; 73:3, 12; Yer 12:1

Ayubu 21:9

Marejeo

  • +Zb 73:3, 5

Ayubu 21:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “filimbi.”

Marejeo

  • +Isa 5:12; 22:13; Amo 6:4, 5

Ayubu 21:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “haraka,” yaani, wanakufa upesi bila maumivu.

  • *

    Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Ayubu 21:14

Marejeo

  • +Zb 10:4, 11; 73:3, 11

Ayubu 21:15

Marejeo

  • +Kut 5:2; Zb 10:4; Ho. 13:6
  • +Mal 3:14

Ayubu 21:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Mashauri; Njama za waovu ziko mbali nami.”

Marejeo

  • +Lu 12:19, 20
  • +Zb 1:1

Ayubu 21:17

Marejeo

  • +Met 13:9; 20:20; 24:20

Ayubu 21:19

Marejeo

  • +Zb 11:6; Isa 26:11

Ayubu 21:20

Marejeo

  • +Zb 75:8; Isa 51:17; Yer 25:15; Ufu 14:10

Ayubu 21:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “imegawanywa mara mbili.”

Marejeo

  • +Zb 55:23

Ayubu 21:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kumfundisha Mungu jambo lolote.”

Marejeo

  • +Isa 40:13, 14; Ro 11:34; 1Ko 2:16
  • +Isa 40:23

Ayubu 21:23

Marejeo

  • +Zb 49:17; Lu 12:19, 20
  • +Zb 73:12, 19; Mt 24:38, 39

Ayubu 21:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “umajimaji ulio mifupani haujakauka.”

Ayubu 21:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “akiwa na uchungu nafsini.”

Ayubu 21:26

Marejeo

  • +Ayu 3:19; Mhu 9:2
  • +Ayu 24:20

Ayubu 21:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “ili kunitendea kikatili.”

Marejeo

  • +Zb 59:3

Ayubu 21:28

Marejeo

  • +Ayu 20:5, 7

Ayubu 21:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ishara zao.”

Ayubu 21:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “korongoni.”

  • *

    Tnn., “Naye atawakokota wanadamu wote wamfuate.”

Marejeo

  • +Ayu 3:17
  • +Ro 5:12

Ayubu 21:34

Marejeo

  • +Ayu 16:2, 3

Jumla

Ayu. 21:3Ayu 16:10, 20; 17:2; Ebr 11:36
Ayu. 21:7Hab 1:3, 13
Ayu. 21:7Ayu 12:6; Zb 37:7; 73:3, 12; Yer 12:1
Ayu. 21:9Zb 73:3, 5
Ayu. 21:12Isa 5:12; 22:13; Amo 6:4, 5
Ayu. 21:14Zb 10:4, 11; 73:3, 11
Ayu. 21:15Kut 5:2; Zb 10:4; Ho. 13:6
Ayu. 21:15Mal 3:14
Ayu. 21:16Lu 12:19, 20
Ayu. 21:16Zb 1:1
Ayu. 21:17Met 13:9; 20:20; 24:20
Ayu. 21:19Zb 11:6; Isa 26:11
Ayu. 21:20Zb 75:8; Isa 51:17; Yer 25:15; Ufu 14:10
Ayu. 21:21Zb 55:23
Ayu. 21:22Isa 40:13, 14; Ro 11:34; 1Ko 2:16
Ayu. 21:22Isa 40:23
Ayu. 21:23Zb 49:17; Lu 12:19, 20
Ayu. 21:23Zb 73:12, 19; Mt 24:38, 39
Ayu. 21:26Ayu 3:19; Mhu 9:2
Ayu. 21:26Ayu 24:20
Ayu. 21:27Zb 59:3
Ayu. 21:28Ayu 20:5, 7
Ayu. 21:33Ayu 3:17
Ayu. 21:33Ro 5:12
Ayu. 21:34Ayu 16:2, 3
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 21:1-34

Ayubu

21 Ayubu akajibu:

 2 “Sikilizeni kwa makini ninayosema;

Na hii iwe faraja mnayonipa.

 3 Nivumilieni ninapozungumza;

Nikimaliza kuzungumza, mnaweza kunidhihaki.+

 4 Je, ninamlalamikia mwanadamu?

Ikiwa ndivyo, je, nisingekosa* subira?

 5 Niangalieni na kunikodolea macho kwa mshangao;

Funikeni kinywa chenu kwa mkono wenu.

 6 Ninapofikiria jambo hilo, nashikwa na wasiwasi,

Na mwili wangu wote unatetemeka.

 7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi,+

Wanazeeka, na kutajirika?*+

 8 Huwaona watoto wao sikuzote,

Nao huendelea kuishi na kuwaona wazao wao.

 9 Nyumba zao zina usalama, hawana hofu yoyote,+

Na Mungu hawaadhibu kwa fimbo yake.

10 Ng’ombe dume wao hawashindwi kuzalisha;

Ng’ombe wao huzaa na mimba haziharibiki.

11 Wavulana wao hukimbia nje kama kondoo,

Na watoto wao hurukaruka huku na huku.

12 Wao huimba kwa tari na kinubi

Na kushangilia wanaposikia sauti ya zumari.*+

13 Huishi siku zao wakiwa wameridhika

Nao hushuka kwa amani* Kaburini.*

14 Lakini wanamwambia Mungu wa kweli, ‘Tuache!

Hatutamani kuzijua njia zako.+

15 Mweza-Yote ni nani ili tumtumikie?+

Tutapata faida gani tukimfahamu?’+

16 Lakini ninajua kwamba hawaudhibiti ufanisi wao wenyewe.+

Mawazo ya waovu yako mbali nami.*+

17 Ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa?+

Ni mara ngapi wanapopatwa na msiba?

Ni mara ngapi Mungu huwaangamiza kwa hasira yake?

18 Je, kuna wakati wowote wanapopeperushwa na upepo kama majani makavu

Na kama makapi yanayopeperushwa mbali na upepo wa dhoruba?

19 Mungu atawawekea watoto wa mtu mwovu adhabu ya mtu huyo.

Lakini Mungu na amlipe ili apate kujua hilo.+

20 Macho yake mwenyewe na yaone maangamizi yake,

Na anywe mwenyewe ghadhabu ya Mweza-Yote.+

21 Kwa maana, kwa nini ahangaikie kitakachoipata nyumba yake baada ya kifo chake

Ikiwa idadi ya miezi yake imepunguzwa?*+

22 Je, kuna yeyote anayeweza kumfundisha Mungu ujuzi,*+

Wakati Yeye ndiye anayewahukumu hata walio juu zaidi?+

23 Kuna mtu anayekufa akiwa na nguvu zake zote+

Akiwa amestarehe kabisa na bila mahangaiko,+

24 Wakati mapaja yake yamenenepa kwa mafuta

Na mifupa yake ikiwa na nguvu.*

25 Lakini mtu mwingine hufa akiwa ametaabika sana,*

Akiwa hajaonja kamwe vitu vyema.

26 Wote watalala mavumbini,+

Na mabuu yatawafunika wote wawili.+

27 Tazama! Ninajua vizuri mambo mnayofikiria

Na njama mnazopanga ili kunidhuru.*+

28 Kwa maana mnasema, ‘Iko wapi nyumba ya yule mtu maarufu,

Na liko wapi hema alimoishi yule mtu mwovu?’+

29 Je, hamjawauliza wasafiri?

Je, hamchunguzi kwa makini mambo waliyoona,*

30 Kwamba mtu mwovu huokolewa katika siku ya msiba

Na kuokolewa katika siku ya ghadhabu?

31 Ni nani atakayemuuliza kuhusu njia yake,

Na ni nani atakayemlipa kwa sababu ya mambo aliyotenda?

32 Anapopelekwa kaburini,

Kaburi lake litalindwa.

33 Mabonge ya udongo wa bondeni* yatakuwa matamu kwake,+

Na wanadamu wote humfuata*+

Kama idadi isiyohesabika ya waliomtangulia.

34 Basi kwa nini mnipe faraja isiyo na maana?+

Majibu yenu hayana lolote isipokuwa udanganyifu!”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki