Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 28
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Ayubu aonyesha tofauti iliyopo kati ya hazina za dunia na hekima (1-28)

        • Jitihada za wanadamu za kuchimba madini (1-11)

        • Hekima ina thamani kuliko lulu (18)

        • Kumwogopa Yehova ndiyo hekima ya kweli (28)

Ayubu 28:1

Marejeo

  • +Met 17:3; Mal 3:3

Ayubu 28:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “humwagwa.”

Marejeo

  • +Kum 8:7, 9

Ayubu 28:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana kwamba maneno haya yanahusu uchimbaji wa madini.

Ayubu 28:10

Marejeo

  • +2Fa 20:20; 2Nya 32:30

Ayubu 28:12

Marejeo

  • +Met 2:6; Yak 1:5
  • +Ayu 28:28

Ayubu 28:13

Marejeo

  • +Met 3:15

Ayubu 28:14

Marejeo

  • +Ro 11:34

Ayubu 28:15

Marejeo

  • +Met 3:13, 14

Ayubu 28:16

Marejeo

  • +Isa 13:12

Ayubu 28:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “iliyosafishwa.”

Marejeo

  • +Met 16:16

Ayubu 28:18

Marejeo

  • +Met 8:11; 20:15

Ayubu 28:19

Marejeo

  • +Kut 28:15, 17

Ayubu 28:20

Marejeo

  • +Ayu 28:12

Ayubu 28:21

Marejeo

  • +Mhu 8:17; 1Ko 2:8, 11

Ayubu 28:23

Marejeo

  • +Yak 1:5

Ayubu 28:24

Marejeo

  • +Met 15:3; Zek 4:10; 1Pe 3:12

Ayubu 28:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “uzito.”

Marejeo

  • +Zb 148:8; Mhu 1:6
  • +Ayu 5:10; 26:8; 37:10; Zb 135:7; Met 30:4; Isa 40:12

Ayubu 28:26

Marejeo

  • +Zek 10:1
  • +Ayu 38:25

Ayubu 28:28

Marejeo

  • +Kum 4:6; Zb 111:10; Met 9:10; Mhu 12:13; Ro 1:20
  • +Met 3:7

Jumla

Ayu. 28:1Met 17:3; Mal 3:3
Ayu. 28:2Kum 8:7, 9
Ayu. 28:102Fa 20:20; 2Nya 32:30
Ayu. 28:12Met 2:6; Yak 1:5
Ayu. 28:12Ayu 28:28
Ayu. 28:13Met 3:15
Ayu. 28:14Ro 11:34
Ayu. 28:15Met 3:13, 14
Ayu. 28:16Isa 13:12
Ayu. 28:17Met 16:16
Ayu. 28:18Met 8:11; 20:15
Ayu. 28:19Kut 28:15, 17
Ayu. 28:20Ayu 28:12
Ayu. 28:21Mhu 8:17; 1Ko 2:8, 11
Ayu. 28:23Yak 1:5
Ayu. 28:24Met 15:3; Zek 4:10; 1Pe 3:12
Ayu. 28:25Zb 148:8; Mhu 1:6
Ayu. 28:25Ayu 5:10; 26:8; 37:10; Zb 135:7; Met 30:4; Isa 40:12
Ayu. 28:26Zek 10:1
Ayu. 28:26Ayu 38:25
Ayu. 28:28Kum 4:6; Zb 111:10; Met 9:10; Mhu 12:13; Ro 1:20
Ayu. 28:28Met 3:7
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 28:1-28

Ayubu

28 “Kuna mahali pa kuchimba fedha

Na mahali pa dhahabu wanayosafisha;+

 2 Chuma hutolewa ardhini,

Na shaba huyeyushwa* kutoka katika miamba.+

 3 Mwanadamu hulishinda giza;

Huchunguza kwa kina katika utusitusi na giza,

Akitafuta mawe yenye madini.

 4 Huzamisha bomba mbali na makao ya watu,

Mahali paliposahauliwa, mbali na mahali ambapo watu wanatembea;

Wanaume fulani hushuka wakining’inia kwa kamba.

 5 Chakula hukua juu ardhini;

Lakini chini, kuna msukosuko kama wa moto.*

 6 Katika mawe hayo kuna yakuti,

Na vumbi lake lina dhahabu.

 7 Hakuna ndege awindaye anayejua njia ya kufika huko;

Jicho la mwewe mweusi halijaiona.

 8 Hakuna mnyama yeyote wa mwituni mwenye fahari aliyeikanyaga;

Mwanasimba hajazunguka huko.

 9 Mwanadamu hugonga mwamba mgumu kwa mkono wake;

Huipindua milima kwenye misingi yake.

10 Huchimba mitaro ya maji+ kwenye mwamba;

Macho yake huona kila kitu chenye thamani.

11 Huziba chemchemi za mito

Na kufichua vitu vilivyofichwa.

12 Lakini hekima—inaweza kupatikana wapi,+

Na kiko wapi chanzo cha uelewaji?+

13 Hakuna mwanadamu anayetambua thamani yake,+

Nayo haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.

14 Vilindi vya maji vinasema, ‘Haimo ndani yangu!’

Nayo bahari inasema, ‘Haiko pamoja nami!’+

15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi;

Wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.+

16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri+

Wala kwa madini ya shohamu na yakuti yasiyopatikana kwa urahisi.

17 Dhahabu na kioo haviwezi kulinganishwa nayo;

Wala haiwezi kubadilishwa kwa chombo cha dhahabu bora.*+

18 Marijani na fuwele hazistahili kutajwa,+

Kwa maana mfuko uliojaa hekima una thamani kuliko mfuko uliojaa lulu.

19 Topazi+ ya Kushi haiwezi kulinganishwa nayo;

Haiwezi kununuliwa hata kwa dhahabu safi.

20 Lakini hekima hutoka wapi,

Na kiko wapi chanzo cha uelewaji?+

21 Imefichwa kutoka machoni pa kila kiumbe aliye hai+

Na kufichwa kutoka kwa ndege wa angani.

22 Maangamizi na kifo husema,

‘Masikio yetu yamesikia tu habari zake.’

23 Mungu anaelewa njia ya kuipata;

Yeye peke yake ndiye anayejua inakokaa,+

24 Kwa maana yeye hutazama mpaka kwenye miisho ya dunia,

Naye huona kila kitu chini ya mbingu.+

25 Alipoupa upepo nguvu*+

Na kuyapima maji,+

26 Alipoiwekea mvua sheria+

Na njia kwa ajili ya mawingu ya dhoruba yenye ngurumo,+

27 Kisha akaiona hekima na kuifafanua;

Aliiimarisha na kuijaribu.

28 Naye akamwambia mwanadamu:

‘Tazama! Kumwogopa Yehova—hiyo ndiyo hekima,+

Na kuepuka uovu ni uelewaji.’”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki