Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 30
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Ayubu aeleza jinsi maisha yake yalivyobadilika (1-31)

        • Adhihakiwa na watu wasiofaa kitu (1-15)

        • Yaonekana ni kama Mungu hamsaidii (20, 21)

        • “Ngozi yangu imekuwa nyeusi” (30)

Ayubu 30:1

Marejeo

  • +Ayu 12:4

Ayubu 30:5

Marejeo

  • +Mwa 4:12; Zb 109:10; Da 4:25

Ayubu 30:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “makorongo.”

Ayubu 30:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Wamepigwa mijeledi na kufukuzwa.”

Ayubu 30:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “methali; msemo kwao.”

Marejeo

  • +Zb 69:12; Omb 3:14
  • +Ayu 17:6

Ayubu 30:10

Marejeo

  • +Ayu 19:13
  • +Hes 12:14; Kum 25:9; Isa 50:6; Mt 27:30

Ayubu 30:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “amelegeza kamba ya upinde wangu.”

  • *

    Tnn., “Wanatupilia mbali lijamu.”

Ayubu 30:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Na hakuna yeyote anayewasaidia.”

Marejeo

  • +Ayu 16:2; Zb 69:26

Ayubu 30:16

Marejeo

  • +Zb 22:14
  • +Ayu 10:15

Ayubu 30:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Mifupa yangu inatobolewa.”

Marejeo

  • +Zb 6:2
  • +Ayu 2:8, 13; 7:4

Ayubu 30:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Mateso yangu makali yanauharibu mwili wangu.”

Ayubu 30:20

Marejeo

  • +Ayu 19:7; Zb 22:2

Ayubu 30:21

Marejeo

  • +Ayu 7:20; 19:6

Ayubu 30:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “unaniyeyusha kwa kishindo.”

Ayubu 30:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kushambulia rundo la magofu.”

Marejeo

  • +Ayu 13:25

Ayubu 30:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “walio na siku ngumu?”

Marejeo

  • +Met 14:21, 31; 19:17

Ayubu 30:28

Marejeo

  • +Zb 38:6; 42:9; 43:2

Ayubu 30:29

Marejeo

  • +Mik 1:8

Ayubu 30:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “homa.”

Marejeo

  • +Ayu 7:5; Omb 4:8

Ayubu 30:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “filimbi.”

Jumla

Ayu. 30:1Ayu 12:4
Ayu. 30:5Mwa 4:12; Zb 109:10; Da 4:25
Ayu. 30:9Zb 69:12; Omb 3:14
Ayu. 30:9Ayu 17:6
Ayu. 30:10Ayu 19:13
Ayu. 30:10Hes 12:14; Kum 25:9; Isa 50:6; Mt 27:30
Ayu. 30:13Ayu 16:2; Zb 69:26
Ayu. 30:16Zb 22:14
Ayu. 30:16Ayu 10:15
Ayu. 30:17Zb 6:2
Ayu. 30:17Ayu 2:8, 13; 7:4
Ayu. 30:20Ayu 19:7; Zb 22:2
Ayu. 30:21Ayu 7:20; 19:6
Ayu. 30:24Ayu 13:25
Ayu. 30:25Met 14:21, 31; 19:17
Ayu. 30:28Zb 38:6; 42:9; 43:2
Ayu. 30:29Mik 1:8
Ayu. 30:30Ayu 7:5; Omb 4:8
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 30:1-31

Ayubu

30 “Sasa wananicheka+

—Wanaume wenye umri mdogo kuliko mimi,

Ambao baba zao ningekataa

Kuwaweka pamoja na mbwa waliolinda kondoo wangu.

 2 Nguvu za mikono yao zilikuwa na faida gani kwangu?

Nguvu zao zimekwisha.

 3 Wamedhoofika kwa sababu ya umaskini na njaa;

Wanaguguna ardhi iliyokauka

Ambayo ilikuwa tayari imeharibiwa na kuachwa ukiwa.

 4 Wanakusanya mmea wenye chumvi kutoka vichakani;

Chakula chao ni mizizi ya miretemu.

 5 Wanafukuzwa kutoka katika jamii;+

Watu wanawapigia kelele kama wanavyompigia kelele mwizi.

 6 Wanaishi kwenye miteremko ya mabonde,*

Kwenye mashimo ardhini na katika miamba.

 7 Wanalia kwa sauti kutoka vichakani

Na kujikunyata pamoja katikati ya upupu.

 8 Kama wana wa watu wapumbavu na wasio na jina,

Wamefukuzwa* kutoka nchini.

 9 Lakini sasa wananidhihaki hata katika nyimbo zao;+

Nimekuwa kitu cha kudharauliwa nao.*+

10 Wananichukia na kukaa mbali nami;+

Hawasiti kunitemea mate usoni.+

11 Kwa sababu Mungu amenidhoofisha* na kuninyenyekeza,

Wanafanya watakavyo* mbele zangu.

12 Wanainuka upande wangu wa kulia kama umati;

Wananikimbiza

Na kuweka vizuizi vya maangamizi kwenye njia yangu.

13 Wanaharibu barabara zangu

Na kuzidisha msiba wangu,+

Na hakuna yeyote anayewazuia.*

14 Wanakuja kana kwamba wanapita kwenye ufa mpana ukutani;

Wanamiminika ndani katikati ya magofu.

15 Hofu inanilemea;

Heshima yangu inapeperushwa mbali kama upepo,

Na wokovu wangu unatoweka kama wingu.

16 Sasa uhai wangu unatoweka taratibu;+

Siku za mateso+ zinashikamana nami.

17 Maumivu yanatoboa mifupa yangu* usiku;+

Na maumivu yanayonitafuna hayaishi kamwe.+

18 Kwa nguvu nyingi vazi langu limechakazwa;*

Hunikaba kama ukosi wa vazi langu.

19 Mungu ameniangusha chini kwenye matope;

Nimebaki mavumbi na majivu tu.

20 Ninakulilia unisaidie, lakini hunijibu;+

Ninasimama, lakini unaniangalia tu.

21 Umenigeukia kwa ukatili;+

Kwa nguvu zote za mkono wako, unanishambulia.

22 Unaniinua juu na kunipeperusha katika upepo;

Kisha unanitupa huku na huku katika dhoruba.*

23 Kwa maana ninajua kwamba utanishusha katika kifo,

Katika nyumba ambamo watu wote walio hai watakutana.

24 Lakini hakuna yeyote anayeweza kumshambulia mtu anayetaabika*+

Anapolilia msaada wakati wa msiba.

25 Je, sijawalilia wale ambao wamekabili nyakati ngumu?*

Je, sijawahuzunikia maskini?+

26 Ingawa nilitumaini mema, mabaya yalikuja;

Nilitarajia nuru, lakini giza likaja.

27 Msukosuko uliokuwa ndani yangu haukukoma;

Siku za mateso zilinikabili.

28 Ninatembeatembea kwa huzuni;+ hakuna mwangaza wa jua.

Ninasimama na kulilia msaada katika kusanyiko.

29 Nimekuwa ndugu ya mbwamwitu

Na rafiki ya mabinti wa mbuni.+

30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi na imebambuka;+

Mifupa yangu inaungua kwa sababu ya joto.*

31 Kinubi changu kinatumika kwa ajili ya maombolezo tu,

Na zumari* yangu kwa ajili ya sauti ya kilio.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki