Ayubu
30 “Sasa wananicheka+
—Wanaume wenye umri mdogo kuliko mimi,
Ambao baba zao ningekataa
Kuwaweka pamoja na mbwa waliolinda kondoo wangu.
2 Nguvu za mikono yao zilikuwa na faida gani kwangu?
Nguvu zao zimekwisha.
3 Wamedhoofika kwa sababu ya umaskini na njaa;
Wanaguguna ardhi iliyokauka
Ambayo ilikuwa tayari imeharibiwa na kuachwa ukiwa.
4 Wanakusanya mmea wenye chumvi kutoka vichakani;
Chakula chao ni mizizi ya miretemu.
5 Wanafukuzwa kutoka katika jamii;+
Watu wanawapigia kelele kama wanavyompigia kelele mwizi.
6 Wanaishi kwenye miteremko ya mabonde,*
Kwenye mashimo ardhini na katika miamba.
7 Wanalia kwa sauti kutoka vichakani
Na kujikunyata pamoja katikati ya upupu.
8 Kama wana wa watu wapumbavu na wasio na jina,
Wamefukuzwa* kutoka nchini.
12 Wanainuka upande wangu wa kulia kama umati;
Wananikimbiza
Na kuweka vizuizi vya maangamizi kwenye njia yangu.
14 Wanakuja kana kwamba wanapita kwenye ufa mpana ukutani;
Wanamiminika ndani katikati ya magofu.
15 Hofu inanilemea;
Heshima yangu inapeperushwa mbali kama upepo,
Na wokovu wangu unatoweka kama wingu.
18 Kwa nguvu nyingi vazi langu limechakazwa;*
Hunikaba kama ukosi wa vazi langu.
19 Mungu ameniangusha chini kwenye matope;
Nimebaki mavumbi na majivu tu.
20 Ninakulilia unisaidie, lakini hunijibu;+
Ninasimama, lakini unaniangalia tu.
21 Umenigeukia kwa ukatili;+
Kwa nguvu zote za mkono wako, unanishambulia.
22 Unaniinua juu na kunipeperusha katika upepo;
Kisha unanitupa huku na huku katika dhoruba.*
23 Kwa maana ninajua kwamba utanishusha katika kifo,
Katika nyumba ambamo watu wote walio hai watakutana.
25 Je, sijawalilia wale ambao wamekabili nyakati ngumu?*
Je, sijawahuzunikia maskini?+
26 Ingawa nilitumaini mema, mabaya yalikuja;
Nilitarajia nuru, lakini giza likaja.
27 Msukosuko uliokuwa ndani yangu haukukoma;
Siku za mateso zilinikabili.
28 Ninatembeatembea kwa huzuni;+ hakuna mwangaza wa jua.
Ninasimama na kulilia msaada katika kusanyiko.
29 Nimekuwa ndugu ya mbwamwitu
Na rafiki ya mabinti wa mbuni.+
31 Kinubi changu kinatumika kwa ajili ya maombolezo tu,
Na zumari* yangu kwa ajili ya sauti ya kilio.