Zaburi
Wimbo wa Safari za Kupanda.
121 Ninayainua macho yangu nitazame milimani.+
Msaada wangu utatoka wapi?
2 Msaada wangu hutoka kwa Yehova,+
Muumba wa mbingu na dunia.
3 Hataruhusu kamwe mguu wako uteleze.*+
Yeye anayekulinda hatasinzia kamwe.
4 Tazama! Hatasinzia kamwe wala kulala usingizi,
Yeye anayelinda Israeli.+
5 Yehova anakulinda.
Yehova ni kivuli+ kwenye mkono wako wa kulia.+
7 Yehova atakulinda dhidi ya madhara yote.+
8 Yehova atakulinda katika mambo yote unayofanya*
Kuanzia sasa mpaka milele.