Zaburi
Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.
38 Ee Yehova, usinikaripie kwa hasira yako,
Wala usinirekebishe kwa ghadhabu yako.+
2 Kwa maana mishale yako imenichoma ndani kabisa,
Na mkono wako unanikandamiza chini.+
3 Mwili wangu wote ni mgonjwa kwa sababu ya hasira yako kali.
Hakuna amani katika mifupa yangu kwa sababu ya dhambi yangu.+
4 Kwa maana dhambi zangu zimetanda juu ya kichwa changu;+
Kama mzigo mzito, ni nzito sana siwezi kuzibeba.
5 Vidonda vyangu vinanuka na vina usaha
Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6 Nimesononeka na kushuka moyo kupita kiasi;
Ninatembea huku na huku mchana kutwa kwa huzuni.
8 Nimekufa ganzi na kupondeka kabisa;
Moyo wangu wenye maumivu makali unanifanya nilie kwa sauti kubwa.*
9 Ee Yehova, unajua mambo yote ninayotamani,
Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa machoni pako.
10 Moyo wangu unadundadunda, nguvu zangu zimetoweka,
Na nuru ya macho yangu imetoweka.+
11 Rafiki zangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,
Na rafiki zangu wa karibu wanasimama mbali.
12 Wale wanaotafuta uhai wangu* wanatega mitego;
Wale wanaojaribu kunidhuru wanazungumza kuhusu kuniangamiza;+
Wananong’onezana uwongo mchana kutwa.
14 Nimekuwa kama mtu asiyeweza kusikia,
Ambaye kinywa chake hakina lolote la kujitetea.
16 Kwa maana nilisema: “Acha wasinicheke
Wala kujikweza juu yangu mguu wangu ukiteleza.”
17 Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,
Na maumivu yangu yalikuwa pamoja nami daima.+
20 Walinilipa uovu kwa mema niliyotenda;
Walinipinga kwa sababu ya kufuatia mambo mema.
21 Usiniache, Ee Yehova.
Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami.+
22 Njoo haraka unisaidie,
Ee Yehova, wokovu wangu.+