Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 38
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Zaburi—Yaliyomo

      • Sala ya mtu aliyetubu anayeteseka

        • “Nimesononeka na kushuka moyo kupita kiasi” (6)

        • Yehova huwasikia wale wanaomngojea (15)

        • “Nilihangaishwa na dhambi yangu” (18)

Zaburi 38:1

Marejeo

  • +Yer 10:24

Zaburi 38:2

Marejeo

  • +Zb 32:4

Zaburi 38:3

Marejeo

  • +Zb 6:2; 41:4; 51:8

Zaburi 38:4

Marejeo

  • +Ezr 9:6; Zb 40:12

Zaburi 38:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Viuno vyangu vimejaa moto.”

Marejeo

  • +Zb 38:3

Zaburi 38:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ningurume.”

Zaburi 38:10

Marejeo

  • +Zb 6:7

Zaburi 38:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yangu.”

Marejeo

  • +2Sa 16:7; Zb 62:4

Zaburi 38:13

Marejeo

  • +2Sa 16:11
  • +Zb 39:2, 9

Zaburi 38:15

Marejeo

  • +2Sa 16:12; Zb 123:2
  • +Zb 138:3

Zaburi 38:17

Marejeo

  • +Zb 77:2

Zaburi 38:18

Marejeo

  • +Zb 32:5
  • +Zb 51:3

Zaburi 38:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wako hai.”

  • *

    Au labda, “Lakini wale ambao ni maadui wangu bila sababu ni wengi.”

Zaburi 38:21

Marejeo

  • +Zb 22:11; 35:22

Zaburi 38:22

Marejeo

  • +Zb 27:1; 62:2; Isa 12:2

Jumla

Zab. 38:1Yer 10:24
Zab. 38:2Zb 32:4
Zab. 38:3Zb 6:2; 41:4; 51:8
Zab. 38:4Ezr 9:6; Zb 40:12
Zab. 38:7Zb 38:3
Zab. 38:10Zb 6:7
Zab. 38:122Sa 16:7; Zb 62:4
Zab. 38:132Sa 16:11
Zab. 38:13Zb 39:2, 9
Zab. 38:152Sa 16:12; Zb 123:2
Zab. 38:15Zb 138:3
Zab. 38:17Zb 77:2
Zab. 38:18Zb 32:5
Zab. 38:18Zb 51:3
Zab. 38:21Zb 22:11; 35:22
Zab. 38:22Zb 27:1; 62:2; Isa 12:2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Zaburi 38:1-22

Zaburi

Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.

38 Ee Yehova, usinikaripie kwa hasira yako,

Wala usinirekebishe kwa ghadhabu yako.+

 2 Kwa maana mishale yako imenichoma ndani kabisa,

Na mkono wako unanikandamiza chini.+

 3 Mwili wangu wote ni mgonjwa kwa sababu ya hasira yako kali.

Hakuna amani katika mifupa yangu kwa sababu ya dhambi yangu.+

 4 Kwa maana dhambi zangu zimetanda juu ya kichwa changu;+

Kama mzigo mzito, ni nzito sana siwezi kuzibeba.

 5 Vidonda vyangu vinanuka na vina usaha

Kwa sababu ya upumbavu wangu.

 6 Nimesononeka na kushuka moyo kupita kiasi;

Ninatembea huku na huku mchana kutwa kwa huzuni.

 7 Ninaungua ndani ya mwili wangu;*

Mwili wangu wote ni mgonjwa.+

 8 Nimekufa ganzi na kupondeka kabisa;

Moyo wangu wenye maumivu makali unanifanya nilie kwa sauti kubwa.*

 9 Ee Yehova, unajua mambo yote ninayotamani,

Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa machoni pako.

10 Moyo wangu unadundadunda, nguvu zangu zimetoweka,

Na nuru ya macho yangu imetoweka.+

11 Rafiki zangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,

Na rafiki zangu wa karibu wanasimama mbali.

12 Wale wanaotafuta uhai wangu* wanatega mitego;

Wale wanaojaribu kunidhuru wanazungumza kuhusu kuniangamiza;+

Wananong’onezana uwongo mchana kutwa.

13 Lakini kama kiziwi, sikuwasikiliza;+

Na kama bubu, sikufumbua kinywa changu.+

14 Nimekuwa kama mtu asiyeweza kusikia,

Ambaye kinywa chake hakina lolote la kujitetea.

15 Kwa maana nilikungojea wewe, Ee Yehova,+

Nawe ukanijibu, Ee Yehova Mungu wangu.+

16 Kwa maana nilisema: “Acha wasinicheke

Wala kujikweza juu yangu mguu wangu ukiteleza.”

17 Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,

Na maumivu yangu yalikuwa pamoja nami daima.+

18 Niliungama kosa langu;+

Nilihangaishwa na dhambi yangu.+

19 Lakini maadui wangu wana juhudi* na ni hodari,*

Wale wanaonichukia bila sababu wameongezeka sana.

20 Walinilipa uovu kwa mema niliyotenda;

Walinipinga kwa sababu ya kufuatia mambo mema.

21 Usiniache, Ee Yehova.

Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami.+

22 Njoo haraka unisaidie,

Ee Yehova, wokovu wangu.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki