Zaburi
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.* Alipomkimbia Sauli na kuingia pangoni.+
57 Nionyeshe kibali, Ee Mungu, nionyeshe kibali,
Kwa maana ninakukimbilia,+
Ninakimbilia kivuli cha mabawa yako mpaka matatizo haya yapite.+
2 Ninamlilia Mungu Aliye Juu Zaidi,
Mungu wa kweli, anayeyakomesha kwa ajili yangu.
3 Atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa.+
Atamtamausha yule anayejaribu kuning’ata. (Sela)
Mungu atatuma upendo wake mshikamanifu na uaminifu wake.+
4 Nimezungukwa na simba;+
Nimelazimika kulala miongoni mwa watu wanaotaka kuninyafua,
Ambao meno yao ni mikuki na mishale
Na ambao ulimi wao ni upanga mkali.+
5 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+
Wamechimba shimo mbele yangu,
Lakini wao wenyewe wameanguka ndani yake.+ (Sela)
7 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu,+
Moyo wangu uko imara.
Nitaimba na kupiga muziki.
8 Amka, utukufu wangu.
Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.
Nitayaamsha mapambazuko.+
10 Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkubwa, uko juu kama mbingu,+
Na uaminifu wako, unafika mpaka angani.
11 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+