Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+
3 Uliizuia ghadhabu yako yote;
Uliiacha hasira yako kali.+
5 Je, utatughadhibikia milele?+
Je, utaendelea kukasirika kizazi baada ya kizazi?
6 Je, hutatuhuisha tena
Ili watu wako washangilie kwa sababu yako?+
7 Ee Yehova, tutendee kwa upendo mshikamanifu,+
Nawe utupe wokovu wako.
8 Nitasikiliza jambo ambalo Mungu wa kweli Yehova anasema,
Kwa maana atawaambia watu wake kuhusu amani,+ washikamanifu wake,
Lakini wasianze tena kujiamini kupita kiasi.+
9 Kwa hakika wokovu wake uko karibu na wale wanaomwogopa,+
Ili utukufu wake ukae katika nchi yetu.
10 Upendo mshikamanifu utakutana na uaminifu;
Uadilifu utabusiana na amani.+
11 Uaminifu utachipuka duniani,
Na uadilifu utatazama chini kutoka mbinguni.+
13 Uadilifu utatembea mbele zake+
Na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.