Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 15
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Kutoka—Yaliyomo

      • Musa na Waisraeli waimba wimbo wa ushindi (1-19)

      • Miriamu aimba akiwaitikia wanaume (20, 21)

      • Maji machungu yageuzwa kuwa matamu (22-27)

Kutoka 15:1

Marejeo

  • +Amu 5:1; 2Sa 22:1; Ufu 15:3
  • +Kut 9:16; 18:10, 11; Zb 106:11, 12
  • +Kut 15:21; Zb 136:15

Kutoka 15:2

Maelezo ya Chini

  • *

    “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Marejeo

  • +Isa 12:2
  • +2Sa 22:47; Isa 25:1
  • +Kut 3:15
  • +Zb 83:18; 148:13

Kutoka 15:3

Marejeo

  • +Zb 24:8
  • +Kut 6:3; Isa 42:8

Kutoka 15:4

Marejeo

  • +Kut 14:27
  • +Kut 14:6, 7

Kutoka 15:5

Marejeo

  • +Ne 9:10, 11

Kutoka 15:6

Marejeo

  • +Zb 60:5; 89:13

Kutoka 15:7

Marejeo

  • +Isa 37:23

Kutoka 15:9

Marejeo

  • +Kut 14:5, 9

Kutoka 15:10

Marejeo

  • +Kut 14:21, 28

Kutoka 15:11

Marejeo

  • +Kum 3:24; 2Sa 7:22
  • +Isa 6:3
  • +Kut 11:9

Kutoka 15:12

Marejeo

  • +Zb 78:53; Ebr 11:29

Kutoka 15:13

Marejeo

  • +Zb 106:10

Kutoka 15:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “uchungu wa kuzaa.”

Marejeo

  • +Hes 14:13, 14

Kutoka 15:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Shehe alikuwa mkuu wa kabila.

  • *

    Au “watawala wa mabavu.”

Marejeo

  • +Hes 22:1, 3
  • +Yos 2:9-11; 5:1

Kutoka 15:16

Marejeo

  • +Kum 11:25
  • +2Sa 7:23; Isa 43:1
  • +Hes 20:14, 17; 21:21, 22

Kutoka 15:17

Marejeo

  • +Zb 80:8

Kutoka 15:18

Marejeo

  • +Zb 10:16

Kutoka 15:19

Marejeo

  • +Kut 14:23
  • +Kut 14:28
  • +Kut 14:22

Kutoka 15:21

Marejeo

  • +Kut 9:16; 18:11
  • +Kut 14:27, 28; Zb 106:11, 12

Kutoka 15:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Uchungu.”

Marejeo

  • +Hes 33:8

Kutoka 15:24

Marejeo

  • +Kut 16:2, 3; 17:3; 1Ko 10:6, 10

Kutoka 15:25

Marejeo

  • +Kut 17:4
  • +Kut 16:4; Kum 8:2

Kutoka 15:26

Marejeo

  • +Kum 28:1
  • +Kum 7:12, 15
  • +Kut 23:25; Zb 103:3

Jumla

Kut. 15:1Amu 5:1; 2Sa 22:1; Ufu 15:3
Kut. 15:1Kut 9:16; 18:10, 11; Zb 106:11, 12
Kut. 15:1Kut 15:21; Zb 136:15
Kut. 15:2Isa 12:2
Kut. 15:22Sa 22:47; Isa 25:1
Kut. 15:2Kut 3:15
Kut. 15:2Zb 83:18; 148:13
Kut. 15:3Zb 24:8
Kut. 15:3Kut 6:3; Isa 42:8
Kut. 15:4Kut 14:27
Kut. 15:4Kut 14:6, 7
Kut. 15:5Ne 9:10, 11
Kut. 15:6Zb 60:5; 89:13
Kut. 15:7Isa 37:23
Kut. 15:9Kut 14:5, 9
Kut. 15:10Kut 14:21, 28
Kut. 15:11Kum 3:24; 2Sa 7:22
Kut. 15:11Isa 6:3
Kut. 15:11Kut 11:9
Kut. 15:12Zb 78:53; Ebr 11:29
Kut. 15:13Zb 106:10
Kut. 15:14Hes 14:13, 14
Kut. 15:15Hes 22:1, 3
Kut. 15:15Yos 2:9-11; 5:1
Kut. 15:16Kum 11:25
Kut. 15:162Sa 7:23; Isa 43:1
Kut. 15:16Hes 20:14, 17; 21:21, 22
Kut. 15:17Zb 80:8
Kut. 15:18Zb 10:16
Kut. 15:19Kut 14:23
Kut. 15:19Kut 14:28
Kut. 15:19Kut 14:22
Kut. 15:21Kut 9:16; 18:11
Kut. 15:21Kut 14:27, 28; Zb 106:11, 12
Kut. 15:23Hes 33:8
Kut. 15:24Kut 16:2, 3; 17:3; 1Ko 10:6, 10
Kut. 15:25Kut 17:4
Kut. 15:25Kut 16:4; Kum 8:2
Kut. 15:26Kum 28:1
Kut. 15:26Kum 7:12, 15
Kut. 15:26Kut 23:25; Zb 103:3
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Kutoka 15:1-27

Kutoka

15 Wakati huo Musa na Waisraeli wakamwimbia Yehova wimbo huu:+

“Acheni nimwimbie Yehova, kwa maana amekwezwa sana.+

Farasi na mpandaji wake amewavurumisha baharini.+

 2 Nguvu zangu na uwezo wangu ni Yah,* kwa maana amekuwa wokovu wangu.+

Huyu ni Mungu wangu, nitamsifu;+ Mungu wa baba yangu,+ nitamkweza.+

 3 Yehova ni shujaa mwenye nguvu.+ Yehova ndilo jina lake.+

 4 Ametupa baharini magari ya vita ya Farao na jeshi lake,+

Na mashujaa wake bora kabisa wamezama katika Bahari Nyekundu.+

 5 Mawimbi makubwa yaliwafunika; wakazama vilindini kama jiwe.+

 6 Mkono wako wa kuume, Ee Yehova, una nguvu nyingi;+

Mkono wako wa kuume, Ee Yehova, unaweza kumvunjavunja adui.

 7 Katika fahari yako kuu unaweza kuwaangusha chini wale wanaoinuka juu dhidi yako;+

Unaituma hasira yako inayowaka, nayo inawala kama majani makavu.

 8 Kwa pumzi moja kutoka katika mianzi ya pua yako maji yalikusanyika pamoja;

Yalisimama tuli, yakazuia mafuriko;

Mawimbi makubwa yaligandamana katikati ya bahari.

 9 Adui alisema, ‘Nitawafuatia! Nitawafikia!

Nitagawanya nyara mpaka nitakapotosheka!

Nitauchomoa upanga wangu! Mkono wangu utawatiisha!’+

10 Ulipuliza bahari kwa pumzi yako, ikawafunika;+

Walizama kama madini ya risasi katika maji makuu.

11 Ni nani kati ya miungu aliye kama wewe, Ee Yehova?+

Ni nani aliye kama wewe, unayejidhihirisha mwenyewe kuwa mkuu katika utakatifu?+

Wewe unayestahili kuogopwa kwa nyimbo za sifa, Wewe unayetenda mambo yanayostaajabisha.+

12 Uliunyoosha mkono wako wa kuume, dunia ikawameza kabisa.+

13 Kwa upendo wako mshikamanifu umewaongoza watu uliowakomboa;+

Kwa nguvu zako utawaongoza kwenye makao yako matakatifu.

14 Ni lazima mataifa yasikie;+ yatatetemeka;

Wakaaji wa Ufilisti watashikwa na maumivu makali.*

15 Wakati huo mashehe* wa Edomu wataogopa sana,

Na watawala wenye nguvu* wa Moabu watatetemeka.+

Wakaaji wote wa Kanaani watavunjika moyo.+

16 Watashikwa na woga na hofu.+

Kwa sababu ya ukuu wa mkono wako watatulia kama jiwe

Mpaka watu wako watakapopita, Ee Yehova,

Mpaka watu uliowatokeza+ watakapopita.+

17 Utawaleta na kuwapanda kwenye mlima wa urithi wako,+

Mahali pa kudumu ulipotayarisha pawe makao yako, Ee Yehova,

Mahali patakatifu, Ee Yehova, ambapo umepajenga imara kwa mikono yako.

18 Yehova atatawala akiwa mfalme milele na milele.+

19 Farasi wa Farao na magari yake ya vita na askari wake wapanda farasi walipoingia baharini,+

Ndipo Yehova alipoyarudisha maji ya bahari yakawafunika,+

Lakini Waisraeli walitembea kwenye nchi kavu katikati ya bahari.”+

20 Kisha nabii Miriamu, dada ya Haruni, akachukua tari, na wanawake wote wakamfuata wakiwa na matari yao wakicheza dansi. 21 Miriamu akaimba hivi akiwaitikia wanaume:

“Mwimbieni Yehova, kwa maana amekwezwa sana.+

Farasi na mpandaji wake amewavurumisha baharini.”+

22 Baadaye Musa akawaongoza Waisraeli kutoka katika Bahari Nyekundu, wakaenda katika nyika ya Shuri na kusafiri kwa siku tatu nyikani, lakini hawakupata maji. 23 Wakafika Mara,*+ lakini hawakuweza kunywa maji ya Mara kwa sababu yalikuwa machungu. Ndiyo sababu alipaita mahali hapo Mara. 24 Basi watu wakaanza kumnung’unikia Musa,+ wakisema: “Tutakunywa nini?” 25 Musa akamlilia Yehova,+ naye Yehova akamwelekeza kwenye mti fulani. Alipoutupa ndani ya maji hayo, yakawa matamu.

Huko Mungu akawawekea sharti na msingi wa hukumu, na huko Mungu akawajaribu.+ 26 Alisema: “Ikiwa mtaisikiliza kwa makini sauti yangu mimi, Yehova Mungu wenu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu na kusikiliza kwa makini amri zangu na kushika masharti yangu yote,+ sitawaletea ugonjwa wowote ambao niliwaletea Wamisri,+ kwa sababu mimi, Yehova, ninawaponya.”+

27 Baada ya hapo wakafika Elimu, mahali palipokuwa na chemchemi 12 za maji na mitende 70. Kwa hiyo wakapiga kambi hapo kando ya maji.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki