Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 32
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Kutoka—Yaliyomo

      • Ibada ya ndama wa dhahabu (1-35)

        • Musa asikia uimbaji usio wa kawaida (17, 18)

        • Musa ayavunjavunja mabamba ya sheria (19)

        • Walawi wabaki washikamanifu kwa Yehova (26-29)

Kutoka 32:1

Marejeo

  • +Kut 24:18; Kum 9:9
  • +Mdo 7:40

Kutoka 32:2

Marejeo

  • +Kut 12:35, 36

Kutoka 32:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Marejeo

  • +Kum 9:16; Isa 46:6; Mdo 7:41
  • +Kut 20:4; Ne 9:18; Zb 106:19, 20

Kutoka 32:6

Marejeo

  • +1Ko 10:7

Kutoka 32:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wamejichafua.”

Marejeo

  • +Kum 4:15-18

Kutoka 32:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Marejeo

  • +Kut 18:20; 20:3

Kutoka 32:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wana shingo ngumu.”

Marejeo

  • +Kut 34:9; Kum 9:6; Mdo 7:51

Kutoka 32:10

Marejeo

  • +Hes 14:12; Kum 9:14

Kutoka 32:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “akautuliza uso wa.”

Marejeo

  • +Zb 106:23
  • +Kum 9:18, 19

Kutoka 32:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ughairi kuhusu.”

Marejeo

  • +Kum 9:28

Kutoka 32:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mbegu.”

Marejeo

  • +Mwa 22:15-17; 35:10, 11; Ebr 6:13, 14
  • +Mwa 13:14, 15; 26:3, 4

Kutoka 32:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kughairi kuhusu.”

Marejeo

  • +Zb 106:45

Kutoka 32:15

Marejeo

  • +Kut 40:20; Kum 5:22
  • +Kum 9:15

Kutoka 32:16

Marejeo

  • +Kut 31:18; Kum 9:10

Kutoka 32:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “tendo la kishujaa.”

Kutoka 32:19

Marejeo

  • +Ne 9:18; Zb 106:19, 20; Mdo 7:41
  • +Kum 9:16, 17

Kutoka 32:20

Marejeo

  • +Kum 7:25
  • +Kum 9:21

Kutoka 32:22

Marejeo

  • +Kut 15:24; 16:2; 17:2; Kum 9:7; 31:27

Kutoka 32:23

Marejeo

  • +Kut 32:1; Mdo 7:40

Kutoka 32:26

Marejeo

  • +Yos 24:15; 2Fa 10:15

Kutoka 32:27

Marejeo

  • +Hes 25:5

Kutoka 32:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Ujazeni mkono wenu.”

Marejeo

  • +Hes 25:11; Kum 13:6-9
  • +Kum 33:8, 9

Kutoka 32:30

Marejeo

  • +Hes 16:47; 21:7; Kum 9:18

Kutoka 32:31

Marejeo

  • +Kut 20:23

Kutoka 32:32

Marejeo

  • +Hes 14:19
  • +Flp 4:3; Ufu 3:5

Kutoka 32:34

Marejeo

  • +Kut 23:20; 33:2

Jumla

Kut. 32:1Kut 24:18; Kum 9:9
Kut. 32:1Mdo 7:40
Kut. 32:2Kut 12:35, 36
Kut. 32:4Kum 9:16; Isa 46:6; Mdo 7:41
Kut. 32:4Kut 20:4; Ne 9:18; Zb 106:19, 20
Kut. 32:61Ko 10:7
Kut. 32:7Kum 4:15-18
Kut. 32:8Kut 18:20; 20:3
Kut. 32:9Kut 34:9; Kum 9:6; Mdo 7:51
Kut. 32:10Hes 14:12; Kum 9:14
Kut. 32:11Zb 106:23
Kut. 32:11Kum 9:18, 19
Kut. 32:12Kum 9:28
Kut. 32:13Mwa 22:15-17; 35:10, 11; Ebr 6:13, 14
Kut. 32:13Mwa 13:14, 15; 26:3, 4
Kut. 32:14Zb 106:45
Kut. 32:15Kut 40:20; Kum 5:22
Kut. 32:15Kum 9:15
Kut. 32:16Kut 31:18; Kum 9:10
Kut. 32:19Ne 9:18; Zb 106:19, 20; Mdo 7:41
Kut. 32:19Kum 9:16, 17
Kut. 32:20Kum 7:25
Kut. 32:20Kum 9:21
Kut. 32:22Kut 15:24; 16:2; 17:2; Kum 9:7; 31:27
Kut. 32:23Kut 32:1; Mdo 7:40
Kut. 32:26Yos 24:15; 2Fa 10:15
Kut. 32:27Hes 25:5
Kut. 32:29Hes 25:11; Kum 13:6-9
Kut. 32:29Kum 33:8, 9
Kut. 32:30Hes 16:47; 21:7; Kum 9:18
Kut. 32:31Kut 20:23
Kut. 32:32Hes 14:19
Kut. 32:32Flp 4:3; Ufu 3:5
Kut. 32:34Kut 23:20; 33:2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Kutoka 32:1-35

Kutoka

32 Basi, watu wakaona kwamba Musa amekawia sana kushuka kutoka mlimani.+ Kwa hiyo wakakusanyika kumzunguka Haruni na kumwambia: “Haya, tutengenezee mungu atakayetuongoza+ kwa sababu hatujui lililompata huyu Musa, mtu aliyetuongoza kutoka katika nchi ya Misri.” 2 Ndipo Haruni akawaambia: “Chukueni vipuli vya dhahabu+ ambavyo wake zenu, wana wenu, na binti zenu wamevaa masikioni mniletee.” 3 Basi watu wote wakaanza kutoa vipuli vya dhahabu walivyokuwa wamevaa masikioni wakamletea Haruni. 4 Kisha akachukua dhahabu iliyokuwa kwenye vipuli hivyo, akatengeneza sanamu* ya ndama kwa kifaa cha kuchongea.+ Watu wakaanza kusema: “Huyu ndiye Mungu wenu, enyi Waisraeli, aliyewaongoza kutoka katika nchi ya Misri.”+

5 Haruni alipoona hilo, akajenga madhabahu mbele ya sanamu hiyo na kutangaza hivi: “Kesho kutakuwa na sherehe kwa ajili ya Yehova.” 6 Basi wakaamka mapema siku iliyofuata na kuanza kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika. Baada ya hayo watu wakaketi ili wale na kunywa. Kisha wakasimama ili wajitumbuize.+

7 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Nenda, shuka, kwa sababu watu wako uliowaongoza kutoka katika nchi ya Misri wametenda uovu.*+ 8 Wamegeuka haraka na kuacha njia niliyowaamuru wafuate.+ Wamejitengenezea sanamu* ya ndama, nao wanaendelea kuiinamia na kuitolea dhabihu wakisema, ‘Huyu ndiye Mungu wenu, enyi Waisraeli, aliyewaongoza kutoka katika nchi ya Misri.’” 9 Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Nimeona kwamba watu hawa ni wakaidi.*+ 10 Basi sasa, niache niwaangamize kabisa kwa hasira yangu inayowaka, na acha nikufanye wewe kuwa taifa kubwa.”+

11 Ndipo Musa akamsihi* Yehova Mungu wake+ akisema: “Ee Yehova, kwa nini uwaelekezee watu wako hasira yako inayowaka, baada ya kuwatoa katika nchi ya Misri kwa nguvu kuu na kwa mkono wenye nguvu?+ 12 Kwa nini Wamisri waseme, ‘Alikuwa na nia ovu alipowatoa Misri. Alitaka kuwaua milimani na kuwaangamiza kabisa kutoka duniani’?+ Acha hasira yako inayowaka na ufikirie upya* uamuzi wako wa kuwaletea watu wako msiba huu. 13 Wakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaka, na Israeli, uliowaapia kwa jina lako mwenyewe na kusema, ‘Nitaufanya uzao wenu uwe mwingi kama nyota za mbinguni,+ nami nitaupa uzao* wenu nchi yote hii niliyowaahidi, ili iwe miliki yao ya kudumu.’”+

14 Basi Yehova akaanza kufikiria upya* msiba ambao alikuwa amesema atawaletea watu wake.+

15 Kisha Musa akageuka na kushuka kutoka mlimani akiwa amebeba yale mabamba mawili ya Ushahidi+ mikononi mwake.+ Mabamba hayo yalikuwa yameandikwa pande zote mbili; upande wa mbele na wa nyuma. 16 Mabamba hayo yalitengenezwa na Mungu, na maandishi yake yalikuwa maandishi ya Mungu yalichongwa kwenye mabamba hayo.+ 17 Yoshua alipoanza kusikia sauti za watu wakipiga kelele, akamwambia Musa: “Kuna kelele za vita kambini.” 18 Lakini Musa akasema:

“Si sauti za watu wanaoimba kwa sababu ya ushindi,*

Wala si sauti za watu wanaolia kwa sababu ya kushindwa;

Ninasikia sauti za uimbaji wa aina nyingine.”

19 Mara tu Musa alipoikaribia kambi na kuona ile sanamu ya ndama+ na watu wakicheza dansi, akaanza kuwaka hasira, naye akayatupa chini yale mabamba mawili yaliyokuwa mikononi mwake, yakavunjika-vunjika chini ya mlima.+ 20 Akaichukua sanamu ya ndama waliyokuwa wametengeneza, akaiteketeza na kuipondaponda ikawa ungaunga;+ kisha akaunyunyiza juu ya maji na kuwalazimisha Waisraeli wayanywe.+ 21 Musa akamuuliza Haruni: “Watu hawa walikufanya nini hivi kwamba ukasababisha watende dhambi kubwa hivi?” 22 Haruni akajibu: “Usikasirike, bwana wangu. Unajua vizuri kwamba watu hawa wana mwelekeo wa kutenda maovu.+ 23 Basi waliniambia, ‘Tutengenezee mungu atakayetuongoza, kwa sababu hatujui lililompata huyu Musa, mtu aliyetuongoza kutoka katika nchi ya Misri.’+ 24 Basi nikawaambia, ‘Mtu yeyote aliye na dhahabu aitoe na kunipa.’ Kisha nikaitupa motoni na ndama huyu akatokea.”

25 Musa akaona kwamba watu wanafanya watakavyo, kwa sababu Haruni aliwaacha wafanye watakavyo, hivi kwamba wakajiletea aibu mbele ya wapinzani wao. 26 Kisha Musa akasimama kwenye lango la kambi na kusema: “Ni nani aliye upande wa Yehova? Njooni kwangu!”+ Ndipo Walawi wote wakakusanyika kumzunguka. 27 Basi Musa akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli amesema, ‘Kila mmoja wenu na ajifunge upanga wake na kupita kotekote kambini, kutoka lango mpaka lango, amuue ndugu yake, jirani yake, na rafiki yake wa karibu.’”+ 28 Walawi wakafanya kama Musa alivyowaambia. Kwa hiyo wanaume 3,000 hivi waliuawa siku hiyo. 29 Kisha Musa akawaambia: “Jitakaseni* leo kwa ajili ya Yehova, kwa maana kila mmoja wenu amemshambulia mwana wake mwenyewe na ndugu yake mwenyewe;+ atawabariki leo.”+

30 Siku iliyofuata, Musa akawaambia watu: “Mlitenda dhambi kubwa sana, na sasa nitapanda kwenda kwa Yehova ili nione ikiwa ninaweza kuomba msamaha kwa ajili ya dhambi yenu.”+ 31 Kwa hiyo Musa akarudi kwa Yehova na kumwambia: “Watu hawa wametenda dhambi kubwa sana! Walijitengenezea mungu wa dhahabu!+ 32 Lakini sasa ukipenda, wasamehe dhambi yao;+ la sivyo, tafadhali nifute katika kitabu chako ulichoandika.”+ 33 Hata hivyo, Yehova akamwambia Musa: “Yeyote aliyenitendea dhambi, nitamfuta katika kitabu changu. 34 Nenda sasa, waongoze watu kwenda mahali nilipokuambia. Tazama! Malaika wangu atakutangulia,+ na siku ya kuwaadhibu itakapofika, nitawaadhibu kwa sababu ya dhambi yao.” 35 Ndipo Yehova akaanza kuwaletea watu pigo kwa sababu walikuwa wametengeneza sanamu ya ndama, sanamu ambayo Haruni alitengeneza.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki