Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 39
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Kutoka—Yaliyomo

      • Kutengeneza mavazi ya kuhani (1)

      • Efodi (2-7)

      • Kifuko cha kifuani (8-21)

      • Joho lisilo na mikono (22-26)

      • Mavazi mengine ya kuhani (27-29)

      • Bamba la dhahabu (30, 31)

      • Musa akagua hema la ibada (32-43)

Kutoka 39:1

Marejeo

  • +Kut 35:23
  • +Kut 28:4, 5; 29:5; 35:10, 19

Kutoka 39:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaelekea ni Bezaleli.

Marejeo

  • +Kut 28:6-8; Law 8:7

Kutoka 39:5

Marejeo

  • +Kut 29:5

Kutoka 39:6

Marejeo

  • +Kut 28:9, 10

Kutoka 39:7

Marejeo

  • +Kut 28:12

Kutoka 39:8

Marejeo

  • +Law 8:8
  • +Kut 28:15-21

Kutoka 39:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, upana wa kiganja cha mkono kuanzia kidole gumba hadi kidole kidogo, karibu sentimita 22.2 (inchi 8.75). Angalia Nyongeza B14.

Kutoka 39:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Jiwe la thamani ambalo halijulikani, huenda ni jiwe la kaharabu, hayasinthi, opali, au tumalini.

Kutoka 39:15

Marejeo

  • +Kut 28:22-25

Kutoka 39:19

Marejeo

  • +Kut 28:26-28

Kutoka 39:22

Marejeo

  • +Kut 28:31-35

Kutoka 39:27

Marejeo

  • +Kut 28:39, 40

Kutoka 39:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nguo za ndani.”

Marejeo

  • +Kut 28:4
  • +Kut 29:8, 9
  • +Kut 28:42

Kutoka 39:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “taji takatifu.”

Marejeo

  • +Kut 28:36, 37; Law 8:9

Kutoka 39:32

Marejeo

  • +Kut 25:40; Ebr 8:5

Kutoka 39:33

Marejeo

  • +Kut 36:8, 14
  • +Kut 36:18
  • +Kut 36:20
  • +Kut 36:31
  • +Kut 36:24

Kutoka 39:34

Marejeo

  • +Kut 36:19
  • +Kut 36:35

Kutoka 39:35

Marejeo

  • +Kut 37:1, 4
  • +Kut 37:6

Kutoka 39:36

Marejeo

  • +Kut 37:10, 16

Kutoka 39:37

Marejeo

  • +Kut 37:17, 23
  • +Kut 25:38
  • +Kut 35:27, 28

Kutoka 39:38

Marejeo

  • +Kut 37:25
  • +Kut 37:29
  • +Kut 30:34, 35
  • +Kut 36:37

Kutoka 39:39

Marejeo

  • +Kut 38:1, 4
  • +Kut 38:6
  • +Kut 38:30
  • +Kut 30:18; 38:8

Kutoka 39:40

Marejeo

  • +Kut 38:9-11
  • +Kut 38:18
  • +Kut 38:20

Kutoka 39:41

Marejeo

  • +Kut 28:3

Kutoka 39:42

Marejeo

  • +Kut 35:10; 36:1

Jumla

Kut. 39:1Kut 35:23
Kut. 39:1Kut 28:4, 5; 29:5; 35:10, 19
Kut. 39:2Kut 28:6-8; Law 8:7
Kut. 39:5Kut 29:5
Kut. 39:6Kut 28:9, 10
Kut. 39:7Kut 28:12
Kut. 39:8Law 8:8
Kut. 39:8Kut 28:15-21
Kut. 39:15Kut 28:22-25
Kut. 39:19Kut 28:26-28
Kut. 39:22Kut 28:31-35
Kut. 39:27Kut 28:39, 40
Kut. 39:28Kut 28:4
Kut. 39:28Kut 29:8, 9
Kut. 39:28Kut 28:42
Kut. 39:30Kut 28:36, 37; Law 8:9
Kut. 39:32Kut 25:40; Ebr 8:5
Kut. 39:33Kut 36:8, 14
Kut. 39:33Kut 36:18
Kut. 39:33Kut 36:20
Kut. 39:33Kut 36:31
Kut. 39:33Kut 36:24
Kut. 39:34Kut 36:19
Kut. 39:34Kut 36:35
Kut. 39:35Kut 37:1, 4
Kut. 39:35Kut 37:6
Kut. 39:36Kut 37:10, 16
Kut. 39:37Kut 37:17, 23
Kut. 39:37Kut 25:38
Kut. 39:37Kut 35:27, 28
Kut. 39:38Kut 37:25
Kut. 39:38Kut 37:29
Kut. 39:38Kut 30:34, 35
Kut. 39:38Kut 36:37
Kut. 39:39Kut 38:1, 4
Kut. 39:39Kut 38:6
Kut. 39:39Kut 38:30
Kut. 39:39Kut 30:18; 38:8
Kut. 39:40Kut 38:9-11
Kut. 39:40Kut 38:18
Kut. 39:40Kut 38:20
Kut. 39:41Kut 28:3
Kut. 39:42Kut 35:10; 36:1
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Kutoka 39:1-43

Kutoka

39 Walitumia zile nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, na kitambaa cha rangi nyekundu+ kufuma kwa ustadi mavazi ya kuhudumu mahali patakatifu. Walimtengenezea Haruni mavazi matakatifu+ kama Yehova alivyomwamuru Musa.

2 Alitengeneza* efodi+ kwa dhahabu, nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu, na kitani bora kilichosokotwa. 3 Walitengeneza mabamba membamba ya dhahabu kwa kutumia nyundo, naye akayakata yakawa nyuzi nyembamba ili zifumwe pamoja na zile nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu, na kitani bora, akatarizi efodi. 4 Wakatengeneza vipande vya mabegani vilivyoungana, navyo vikaunganishwa kwenye miisho miwili ya efodi. 5 Mshipi uliofumwa unaoshikilia kwa nguvu efodi ulitengenezwa kwa vitu hivyohivyo,+ yaani, dhahabu, nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu, na kitani bora kilichosokotwa, kama Yehova alivyomwamuru Musa.

6 Kisha wakatia mawe ya shohamu katika vifuko vya dhahabu na kuchonga majina ya wana wa Israeli kwenye mawe hayo, kama mtu anavyochonga muhuri.+ 7 Akayaweka mawe hayo kwenye vipande vya mabegani vya efodi, ili yawe mawe ya ukumbusho kwa wana wa Israeli,+ kama Yehova alivyomwamuru Musa. 8 Kisha akatengeneza kifuko cha kifuani+ na kukitarizi. Akakitengeneza kama efodi kwa kutumia dhahabu, nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu, na kitani bora kilichosokotwa.+ 9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba kilipokunjwa mara mbili. Walikitengeneza kifuko hicho cha kifuani kikiwa na urefu wa shubiri moja* na upana wa shubiri moja kinapokunjwa mara mbili. 10 Wakaweka kwenye kifuko hicho mawe yaliyopangwa katika safu nne. Safu ya kwanza ilikuwa na zabarijadi, topazi, na zumaridi. 11 Safu ya pili ilikuwa na feruzi, yakuti, na yaspi. 12 Safu ya tatu ilikuwa na jiwe la leshemi,* akiki, na amethisti. 13 Safu ya nne ilikuwa na krisolito, shohamu, na yashefi. Mawe hayo yaliwekwa kwenye vifuko vya dhahabu. 14 Yalilingana na majina 12 ya wana wa Israeli, na majina hayo yalichongwa kama muhuri, na kila jina liliwakilisha mojawapo ya makabila 12 ya wana wa Israeli.

15 Kisha wakakitengenezea kifuko cha kifuani minyororo iliyosokotwa, kama kamba za dhahabu safi.+ 16 Halafu wakatengeneza vifuko viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu na kuzitia kwenye pembe mbili za juu za kifuko hicho. 17 Baada ya hayo wakatia zile kamba mbili za dhahabu katika pete mbili zilizo kwenye pembe hizo. 18 Kisha wakatia ncha mbili za hizo kamba mbili katika vile vifuko viwili vya mabegani na kuzifunga ncha hizo kwenye vipande viwili vya efodi, sehemu ya mbele. 19 Halafu wakatengeneza pete mbili za dhahabu na kuziweka kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani, upande wa efodi.+ 20 Kisha wakatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu upande wa mbele wa efodi, chini ya vipande viwili vya mabegani vya efodi, karibu na mahali inapoungana, juu ya mshipi uliofumwa wa efodi. 21 Hatimaye, wakafunga pete za kifuko cha kifuani pamoja na pete za efodi kwa kamba ya bluu, ili kifuko cha kifuani kibaki mahali pake kwenye efodi, juu ya mshipi uliofumwa, kama Yehova alivyomwamuru Musa.

22 Kisha akafuma joho lisilo na mikono la efodi kwa nyuzi za bluu peke yake.+ 23 Lilikuwa na nafasi ya kupitishia kichwa katikati sehemu ya juu. Sehemu hiyo ilikuwa na ukingo kuizunguka kama wa koti la vita, ili isiraruke. 24 Halafu wakatengeneza kwenye upindo wa joho hilo makomamanga ya nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, na kitambaa cha rangi nyekundu; vitu vyote hivyo vilisokotwa pamoja. 25 Walitengeneza kengele za dhahabu safi na kuzitia kati ya makomamanga kwenye upindo wote wa joho hilo lisilo na mikono; 26 walitia kengele kisha komamanga, kengele kisha komamanga kwenye upindo wote wa joho hilo lisilo na mikono lililotumiwa kuhudumu, kama Yehova alivyomwamuru Musa.

27 Pia walifuma kanzu za kitani bora kwa ajili ya Haruni na wanawe,+ 28 na pia kilemba+ cha kitani bora, kofia maridadi za kitani bora,+ suruali fupi*+ za kitani bora kilichosokotwa, 29 na ukumbuu uliofumwa kwa kitani bora kilichosokotwa, nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, na kitambaa cha rangi nyekundu, kama Yehova alivyomwamuru Musa.

30 Hatimaye, walitengeneza kwa dhahabu safi bamba linalong’aa, yaani, ile ishara takatifu ya wakfu,* na kuchonga maneno haya juu yake kama muhuri unavyochongwa: “Utakatifu ni wa Yehova.”+ 31 Wakalifunga bamba hilo kwa kamba ya bluu ili waliweke juu ya kilemba, kama Yehova alivyomwamuru Musa.

32 Basi wakakamilisha kazi yote ya hema la ibada, yaani, hema la mkutano; Waisraeli walifanya kila jambo ambalo Yehova alimwamuru Musa.+ Hivyo ndivyo walivyofanya.

33 Wakamletea Musa hema la ibada+ pamoja na vifaa vyake vyote: vibanio vyake,+ viunzi vyake,+ fito zake,+ nguzo zake na vikalio vyake;+ 34 kifuniko chake cha ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu,+ kifuniko chake cha ngozi za sili, na pazia lake;+ 35 sanduku la ushahidi pamoja na fito zake+ na kifuniko chake;+ 36 meza, vyombo vyake vyote+ na mikate ya wonyesho; 37 kinara cha taa cha dhahabu safi, taa zake,+ safu zake za taa, na vyombo vyake vyote+ na mafuta kwa ajili ya taa hizo;+ 38 madhabahu+ ya dhahabu, mafuta yanayotumiwa kutia mafuta,+ uvumba uliotiwa manukato,+ pazia la mlango+ wa hema; 39 madhabahu ya shaba+ na wavu wake wa shaba, fito zake,+ vyombo vyake vyote,+ beseni na kinara chake;+ 40 mapazia ya ua yanayoning’inia, nguzo zake na vikalio vyake,+ pazia la mlango+ wa ua, kamba na vigingi vya hema+ na vifaa vyote vya utumishi wa hema la ibada, yaani, hema la mkutano; 41 yale mavazi yaliyofumwa kwa ustadi ya kuhudumu mahali patakatifu, mavazi matakatifu ya kuhani Haruni,+ na mavazi ya wanawe ya kutumikia wakiwa makuhani.

42 Waisraeli walifanya kazi yote kama Yehova alivyomwamuru Musa.+ 43 Musa alipokagua kazi yao yote, aliona kwamba walikuwa wameifanya kama Yehova alivyoamuru; basi Musa akawabariki.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki