Methali
10 Methali za Sulemani.+
Mwana mwenye hekima humfanya baba yake ashangilie,+
Lakini mwana mpumbavu ni huzuni kwa mama yake.
2 Hazina zilizopatikana kwa uovu hazitakuwa na faida yoyote,
Lakini uadilifu ndio unaookoa kutoka katika kifo.+
3 Yehova hatamwacha mwadilifu akae njaa,+
Lakini atawanyima waovu wanachotamani.
5 Mwana anayetenda kwa ufahamu hukusanya mazao wakati wa kiangazi,
Lakini mwana anayetenda kwa aibu analala usingizi mzito wakati wa mavuno.+
6 Baraka ziko juu ya kichwa cha mwadilifu,+
Lakini kinywa cha mwovu hufunika ukatili.
8 Mwenye hekima moyoni atakubali mafundisho,*+
Lakini mtu anayezungumza maneno ya upumbavu atakanyagiwa chini.+
10 Anayekonyeza jicho lake kwa hila husababisha huzuni,+
Na yule anayezungumza maneno ya upumbavu atakanyagiwa chini.+
12 Chuki ndiyo inayochochea ugomvi,
Lakini upendo hufunika makosa yote.+
13 Hekima hupatikana kwenye midomo ya mtu mwenye utambuzi,+
Lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa mtu asiye na busara.*+
15 Mali ya* tajiri ni jiji lake lenye ngome.
Ufukara wa maskini ndio unaowaangamiza.+
16 Kazi ya mwadilifu huongoza kwenye uzima;
Lakini mazao ya mwovu huongoza kwenye dhambi.+
17 Anayetii nidhamu ni kijia kinachoelekea kwenye uzima,*
Lakini anayepuuza karipio huwapotosha wengine.
19 Maneno yanapokuwa mengi, makosa hayawezi kuepukwa,+
Lakini yeyote anayedhibiti midomo yake anatenda kwa busara.+
20 Ulimi wa mwadilifu ni kama fedha bora kabisa,+
Lakini moyo wa mwovu una thamani ndogo.
23 Kutenda mambo ya aibu ni kama mchezo kwa mpumbavu,
Lakini hekima ni ya mtu mwenye utambuzi.+
24 Anachoogopa mwovu kitamjia;
Lakini tamaa ya mwadilifu itatoshelezwa.+
26 Kama siki kwenye meno na moshi machoni,
Ndivyo alivyo mtu mvivu kwa yule anayemtuma.*
31 Kinywa cha mwadilifu huzaa* hekima,
Lakini ulimi uliopotoka utaangamizwa.
32 Midomo ya mwadilifu inajua mambo yanayopendeza,
Lakini kinywa cha waovu kimepotoka.