Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Methali 25
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Methali—Yaliyomo

    • METHALI ZA SULEMANI ZILIZONAKILIWA NA WATU WA MFALME HEZEKIA (25:1–29:27)

        • Kutunza siri (9)

        • Maneno yaliyochaguliwa vizuri (11)

        • Kuheshimu faragha ya wengine (17)

        • Kukusanya makaa ya mawe juu ya kichwa cha adui (21, 22)

        • Habari njema ni kama maji baridi (25)

Methali 25:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “zilizonakiliwa na kukusanywa.”

Marejeo

  • +1Fa 4:29, 32; Mhu 12:9
  • +2Nya 29:1

Methali 25:2

Marejeo

  • +Kum 29:29; Ro 11:33

Methali 25:4

Marejeo

  • +Met 17:3

Methali 25:5

Marejeo

  • +1Fa 2:44, 46; Met 20:28; 29:14

Methali 25:6

Marejeo

  • +Met 27:2
  • +Zb 131:1

Methali 25:7

Marejeo

  • +Lu 14:8-10; 1Pe 5:5

Methali 25:8

Marejeo

  • +Met 18:17; Mt 5:25

Methali 25:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “usifunue siri za wengine.”

Marejeo

  • +Mt 18:15
  • +Met 11:13

Methali 25:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “uvumi unaodhuru ambao hauwezi.”

Methali 25:11

Marejeo

  • +Met 15:23; Isa 50:4

Methali 25:12

Marejeo

  • +Zb 141:5; Met 1:8, 9; 9:8

Methali 25:13

Marejeo

  • +Met 13:17

Methali 25:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kuhusu zawadi ya uwongo.”

Marejeo

  • +Mt 5:37

Methali 25:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mpole.”

Marejeo

  • +Mwa 32:4, 5; Met 15:1

Methali 25:16

Marejeo

  • +Met 25:27

Methali 25:18

Marejeo

  • +Kut 20:16

Methali 25:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “mtu mwenye hila.”

Methali 25:20

Marejeo

  • +Zb 137:3, 4

Methali 25:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “anayekuchukia.”

Marejeo

  • +Kut 23:5; 2Fa 6:21, 22; Met 24:17; Mt 5:44

Methali 25:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, kupunguza uadui wake na kuyeyusha ugumu wake.

Marejeo

  • +Ro 12:20

Methali 25:23

Marejeo

  • +Zb 101:5

Methali 25:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “msumbufu.”

Marejeo

  • +Met 21:9, 19; 27:15

Methali 25:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Met 15:30; Isa 52:7

Methali 25:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “anayekubaliana na.” Tnn., “anayepepesuka mbele ya.”

Methali 25:27

Marejeo

  • +Met 25:16
  • +Met 27:2; Yoh 5:44; Flp 2:3

Methali 25:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “asiyeweza kuizuia roho yake.”

Marejeo

  • +1Sa 20:33; Met 16:32; 22:24, 25; 29:11

Jumla

Met. 25:11Fa 4:29, 32; Mhu 12:9
Met. 25:12Nya 29:1
Met. 25:2Kum 29:29; Ro 11:33
Met. 25:4Met 17:3
Met. 25:51Fa 2:44, 46; Met 20:28; 29:14
Met. 25:6Met 27:2
Met. 25:6Zb 131:1
Met. 25:7Lu 14:8-10; 1Pe 5:5
Met. 25:8Met 18:17; Mt 5:25
Met. 25:9Mt 18:15
Met. 25:9Met 11:13
Met. 25:11Met 15:23; Isa 50:4
Met. 25:12Zb 141:5; Met 1:8, 9; 9:8
Met. 25:13Met 13:17
Met. 25:14Mt 5:37
Met. 25:15Mwa 32:4, 5; Met 15:1
Met. 25:16Met 25:27
Met. 25:18Kut 20:16
Met. 25:20Zb 137:3, 4
Met. 25:21Kut 23:5; 2Fa 6:21, 22; Met 24:17; Mt 5:44
Met. 25:22Ro 12:20
Met. 25:23Zb 101:5
Met. 25:24Met 21:9, 19; 27:15
Met. 25:25Met 15:30; Isa 52:7
Met. 25:27Met 25:16
Met. 25:27Met 27:2; Yoh 5:44; Flp 2:3
Met. 25:281Sa 20:33; Met 16:32; 22:24, 25; 29:11
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Methali 25:1-28

Methali

25 Hizi pia ni methali za Sulemani+ zilizonakiliwa* na watu wa Hezekia+ mfalme wa Yuda:

 2 Ni utukufu wa Mungu kutunza jambo likiwa siri,+

Na utukufu wa wafalme ni kulichunguza jambo kabisa.

 3 Kama mbingu zilivyo juu na kama dunia ilivyo na kina,

Ndivyo moyo wa wafalme usivyochunguzika.

 4 Ondoa takataka katika fedha,

Nayo itakuwa safi kabisa.+

 5 Mwondoe mtu mwovu mbele ya mfalme,

Na kiti chake cha ufalme kitaimarishwa kabisa katika uadilifu.+

 6 Usijiheshimu mwenyewe mbele ya mfalme,+

Wala usijiingize miongoni mwa watu mashuhuri,+

 7 Kwa maana ni afadhali yeye akuambie, “Njoo hapa juu,”

Kuliko akuaibishe mbele ya mkuu.+

 8 Usiharakishe kupeleka kesi mahakamani,

Kwa maana utafanya nini baadaye jirani yako akikuaibisha?+

 9 Suluhisha jambo hilo na jirani yako,+

Lakini usifunue uliyoambiwa sirini,*+

10 Ili anayesikiliza asikuaibishe

Nawe ueneze habari mbaya ambayo haiwezi* kubatilishwa.

11 Kama matofaa ya dhahabu yaliyonakshiwa kwenye vyombo vya fedha

Ndivyo lilivyo neno linalosemwa wakati unaofaa.+

12 Kama kipuli cha dhahabu na pambo la dhahabu bora

Ndivyo alivyo mkaripiaji mwenye hekima kwa sikio linalosikia.+

13 Kama baridi ya theluji siku ya mavuno

Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wanaomtuma,

Kwa maana yeye humburudisha bwana wake.+

14 Kama mawingu na upepo usioleta mvua

Ndivyo alivyo mtu anayejigamba kwamba atatoa zawadi lakini haitoi kamwe.*+

15 Kwa subira kamanda hushawishiwa,

Na ulimi laini* unaweza kuvunja mfupa.+

16 Ukipata asali, kula kiasi kinachokutosha,

Kwa maana ukiila kupita kiasi, huenda ukaitapika.+

17 Mguu wako na uwe haba katika nyumba ya jirani yako,

Ili asikuchoke na kukuchukia.

18 Kama rungu la vita na upanga na mshale mkali

Ndivyo alivyo mtu anayetoa ushahidi wa uwongo dhidi ya jirani yake.+

19 Kama jino lililovunjika au mguu unaochechemea

Ndivyo ilivyo kumtumaini mtu asiyetegemeka* nyakati za taabu.

20 Kama mtu anayevua nguo siku ya baridi

Na kama siki iliyomwagwa kwenye magadi

Ndivyo alivyo mtu anayeuimbia nyimbo moyo wenye huzuni.+

21 Ikiwa adui yako* ana njaa, mpe mkate ale;

Ikiwa ana kiu, mpe maji anywe,+

22 Kwa maana utakuwa unakusanya makaa ya mawe yanayowaka juu ya kichwa chake,*+

Na Yehova atakuthawabisha.

23 Upepo wa kaskazini huleta mvua,

Na ulimi unaopiga porojo huleta uso wenye hasira.+

24 Ni afadhali kuishi pembeni juu ya paa

Kuliko kuishi katika nyumba moja na mke mgomvi.*+

25 Kama maji baridi kwa nafsi* iliyochoka

Ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.+

26 Kama chemchemi yenye matope na kisima kilichochafuliwa

Ndivyo alivyo mtu mwadilifu anayekubali kumfuata* mtu mwovu.

27 Si vizuri kula asali nyingi mno,+

Wala si utukufu kujitafutia utukufu wako mwenyewe.+

28 Kama jiji lililobomolewa, lisilo na ukuta,

Ndivyo alivyo mtu asiyeweza kuidhibiti hasira yake.*+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki