Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 16
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Yeremia hapaswi kuoa, kuomboleza, wala kusherehekea (1-9)

      • Adhabu, kisha kurudishwa (10-21)

Yeremia 16:4

Marejeo

  • +Yer 15:2
  • +Zb 79:2, 3; Isa 5:25; Yer 7:33; 9:22; 36:30
  • +Eze 5:12

Yeremia 16:5

Marejeo

  • +Eze 24:16, 17
  • +Kum 31:17; Isa 27:11; 63:10

Yeremia 16:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Desturi za kipagani za kuomboleza ambazo inaelekea zilifanywa katika nchi ya Israeli iliyoasi imani.

Yeremia 16:9

Marejeo

  • +Isa 24:7, 8; Yer 7:34; Ufu 18:23

Yeremia 16:10

Marejeo

  • +Yer 5:19

Yeremia 16:11

Marejeo

  • +Amu 2:12
  • +Yer 8:1, 2
  • +Da 9:11; Amo 2:4

Yeremia 16:12

Marejeo

  • +Yer 7:26
  • +Ne 9:29; Yer 6:28

Yeremia 16:13

Marejeo

  • +2Nya 7:20; Yer 15:14; 17:4
  • +Kum 4:27, 28; 28:36

Yeremia 16:14

Marejeo

  • +Kut 20:2; Yer 23:7, 8

Yeremia 16:15

Marejeo

  • +Kum 30:1-3; Yer 3:18; 24:6; 30:3; 32:37; Amo 9:14

Yeremia 16:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “yanatazama njia zao zote.”

Yeremia 16:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “maiti za.”

Marejeo

  • +Isa 40:2
  • +Law 26:30; Zb 106:38

Yeremia 16:19

Marejeo

  • +Yer 17:17
  • +Yer 10:5, 14

Yeremia 16:20

Marejeo

  • +Zb 115:4; Yer 2:11; 1Ko 8:4

Jumla

Yer. 16:4Yer 15:2
Yer. 16:4Zb 79:2, 3; Isa 5:25; Yer 7:33; 9:22; 36:30
Yer. 16:4Eze 5:12
Yer. 16:5Eze 24:16, 17
Yer. 16:5Kum 31:17; Isa 27:11; 63:10
Yer. 16:9Isa 24:7, 8; Yer 7:34; Ufu 18:23
Yer. 16:10Yer 5:19
Yer. 16:11Amu 2:12
Yer. 16:11Yer 8:1, 2
Yer. 16:11Da 9:11; Amo 2:4
Yer. 16:12Yer 7:26
Yer. 16:12Ne 9:29; Yer 6:28
Yer. 16:132Nya 7:20; Yer 15:14; 17:4
Yer. 16:13Kum 4:27, 28; 28:36
Yer. 16:14Kut 20:2; Yer 23:7, 8
Yer. 16:15Kum 30:1-3; Yer 3:18; 24:6; 30:3; 32:37; Amo 9:14
Yer. 16:18Isa 40:2
Yer. 16:18Law 26:30; Zb 106:38
Yer. 16:19Yer 17:17
Yer. 16:19Yer 10:5, 14
Yer. 16:20Zb 115:4; Yer 2:11; 1Ko 8:4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 16:1-21

Yeremia

16 Na neno la Yehova likanijia tena, likisema: 2 “Usioe mke, wala usiwe na wana na mabinti mahali hapa. 3 Kwa maana Yehova anasema hivi kuhusu wana na mabinti wanaozaliwa hapa na kuhusu mama zao wanaowazaa na kuhusu baba zao wanaowazaa katika nchi hii: 4 ‘Watakufa kwa magonjwa hatari,+ lakini hakuna atakayewaombolezea wala kuwazika; watakuwa kama mbolea kwenye ardhi.+ Wataangamia kwa upanga na kwa njaa kali,+ na maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa duniani.’

 5 “Kwa maana Yehova anasema hivi:

‘Usiingie katika nyumba ambamo waombolezaji wanafanya karamu,

Wala usiende kuomboleza au kuwapa pole,’+

‘Kwa maana nimewaondolea watu hawa amani yangu,’ asema Yehova,

‘Pamoja na upendo wangu mshikamanifu na rehema.+

 6 Wakubwa kwa wadogo watakufa katika nchi hii.

Hawatazikwa,

Hakuna mtu atakayewaombolezea,

Wala hakuna mtu atakayejikatakata wala kujitia upara kwa ajili yao.*

 7 Na hakuna mtu atakayewapa chakula wale wanaoomboleza,

Ili kuwafariji baada ya kufiwa;

Wala hakuna yeyote atakayewapa kikombe cha faraja

Ili wanywe kwa sababu ya kumpoteza baba yao au mama yao.

 8 Nawe usiingie katika nyumba ya karamu

Kuketi pamoja nao ili kula na kunywa.’

9 “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Mahali hapa, katika siku zenu na mbele ya macho yenu wenyewe, nitazikomesha sauti za furaha na shangwe, sauti ya bwana harusi na sauti ya bibi harusi.’+

10 “Utakapowaambia watu hawa maneno haya yote, watakuuliza, ‘Kwa nini Yehova amesema kwamba tutapatwa na msiba wote huu mkubwa? Tumemtendea Yehova Mungu wetu kosa gani na dhambi gani?’+ 11 Utawajibu, ‘“Kwa sababu mababu zenu waliniacha,”+ asema Yehova, “nao waliendelea kuifuata miungu mingine na kuiabudu na kuiinamia.+ Lakini waliniacha mimi, nao hawakuishika sheria yangu.+ 12 Nanyi mmetenda mambo mabaya zaidi kuliko mababu zenu,+ na kila mmoja wenu anaufuata ukaidi wa moyo wake mwovu badala ya kunitii.+ 13 Basi nitawatupa nje ya nchi hii mpaka kwenye nchi ambayo wala ninyi wala mababu zenu hawakuijua,+ na huko mtalazimika kuiabudu miungu mingine mchana na usiku,+ kwa sababu sitawaonyesha kibali.”’

14 “‘Hata hivyo, siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘wakati ambapo hawatasema tena: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, aliyewatoa watu wa Israeli nchini Misri!”+ 15 badala yake watasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, aliyewatoa watu wa Israeli katika nchi ya kaskazini na katika nchi zote ambako alikuwa amewatawanya!” nami nitawarudisha katika nchi yao, niliyowapa mababu zao.’+

16 ‘Tazama, ninawaita wavuvi wengi,’ asema Yehova,

‘Nao watawavua.

Na baada ya hapo nitawaita wawindaji wengi,

Nao watawawinda kwenye kila mlima na kila kilima

Na kutoka kwenye mipasuko ya majabali.

17 Kwa maana macho yangu yanaona kila kitu wanachofanya.*

Hawajafichwa kutoka mbele zangu,

Wala kosa lao halijafichwa kutoka mbele ya macho yangu.

18 Kwanza, nitalipa kiwango kamili kinachostahili kosa lao na dhambi yao,+

Kwa maana wameitia unajisi nchi yangu kwa mifano isiyo hai ya* sanamu zao zinazochukiza

Nao wameujaza urithi wangu mambo yao yanayochukiza.’”+

19 Ee Yehova, nguvu zangu na ngome yangu,

Kimbilio langu katika siku ya taabu,+

Mataifa yatakuja kwako kutoka kwenye miisho ya dunia,

Nayo yatasema: “Mababu zetu walirithi uwongo mtupu,

Ubatili na vitu visivyofaa kitu ambavyo havina faida yoyote.”+

20 Je, mwanadamu anaweza kujitengenezea miungu

Wakati kwa kweli hiyo si miungu?+

21 “Basi nitawafanya wajue,

Wakati huu nitawafanya wajue nguvu zangu na uwezo wangu,

Nao watalazimika kujua kwamba jina langu ni Yehova.”

Tanzanian sign language publications (2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki