Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 43
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Watu wakataa kutii kisha waenda Misri (1-7)

      • Neno la Yehova kwa Yeremia nchini Misri (8-13)

Yeremia 43:2

Marejeo

  • +Yer 41:16; 42:1-3

Yeremia 43:3

Marejeo

  • +Yer 36:4; 45:1
  • +Yer 38:4, 6

Yeremia 43:5

Marejeo

  • +Yer 40:11, 12

Yeremia 43:6

Marejeo

  • +Yer 39:10
  • +2Fa 25:22
  • +2Nya 34:20, 21; Yer 26:24
  • +2Fa 22:8

Yeremia 43:7

Marejeo

  • +Yer 2:14, 16; 44:1; Eze 30:4, 18

Yeremia 43:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.

Marejeo

  • +Yer 25:9; 27:6; Eze 29:19, 20
  • +Da 2:21; 5:18

Yeremia 43:11

Marejeo

  • +Yer 25:17, 19; 46:13; Eze 29:19; 30:4, 18
  • +Yer 44:13; Eze 5:12

Yeremia 43:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “atayawasha moto mahekalu ya.”

  • *

    Au “bila madhara.”

Marejeo

  • +Yer 46:25

Yeremia 43:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “minara ya.”

  • *

    Au “Nyumba (Hekalu la) ya Jua,” yaani, Heliopolisi.

  • *

    Au “mahekalu ya.”

Jumla

Yer. 43:2Yer 41:16; 42:1-3
Yer. 43:3Yer 36:4; 45:1
Yer. 43:3Yer 38:4, 6
Yer. 43:5Yer 40:11, 12
Yer. 43:6Yer 39:10
Yer. 43:62Fa 25:22
Yer. 43:62Nya 34:20, 21; Yer 26:24
Yer. 43:62Fa 22:8
Yer. 43:7Yer 2:14, 16; 44:1; Eze 30:4, 18
Yer. 43:10Yer 25:9; 27:6; Eze 29:19, 20
Yer. 43:10Da 2:21; 5:18
Yer. 43:11Yer 25:17, 19; 46:13; Eze 29:19; 30:4, 18
Yer. 43:11Yer 44:13; Eze 5:12
Yer. 43:12Yer 46:25
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 43:1-13

Yeremia

43 Yeremia alipomaliza kuwaambia watu wote maneno hayo yote kutoka kwa Yehova Mungu wao, kila neno ambalo Yehova Mungu wao alikuwa amemtuma awaambie, 2 Azaria mwana wa Hoshaya, Yohanani+ mwana wa Karea, na watu wote wenye kimbelembele wakamwambia Yeremia: “Unasema uwongo! Yehova Mungu wetu hakukutuma useme, ‘Msiende kukaa Misri.’ 3 Lakini Baruku+ mwana wa Neria anakuchochea dhidi yetu ili kututia mikononi mwa Wakaldayo, ili watuue au kutupeleka uhamishoni Babiloni.”+

4 Basi Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa jeshi na watu wote hawakuitii sauti ya Yehova kwamba wabaki katika nchi ya Yuda. 5 Badala yake, Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa jeshi wakawachukua watu wote wa Yuda waliobaki ambao walikuwa wamerudi kuishi katika nchi ya Yuda kutoka katika mataifa yote ambako walikuwa wametawanywa.+ 6 Wakawachukua wanaume, wanawake, watoto, mabinti wa mfalme, na kila mtu ambaye Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi alikuwa amemwacha pamoja na Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ na pia nabii Yeremia na Baruku mwana wa Neria. 7 Nao wakaingia nchini Misri, kwa maana hawakuitii sauti ya Yehova, wakaenda mpaka Tahpanhesi.+

8 Kisha neno la Yehova likamjia Yeremia huko Tahpanhesi likisema: 9 “Beba mkononi mwako mawe makubwa, nawe uyafiche katika saruji kwenye ngazi ya matofali iliyo kwenye mlango wa nyumba ya Farao huko Tahpanhesi, huku wanaume Wayahudi wakitazama. 10 Kisha uwaambie, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Tazameni, ninamwita Nebukadneza* mfalme wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitakiweka kiti chake cha ufalme juu ya mawe haya ambayo nimeyaficha, naye atalitandaza hema lake la kifalme juu yake.+ 11 Naye ataingia na kuipiga nchi ya Misri.+ Yeyote aliyekusudiwa kufa kwa ugonjwa hatari atakufa kwa ugonjwa hatari, na yeyote aliyekusudiwa kwenda utekwani ataenda utekwani, na yeyote aliyekusudiwa kufa kwa upanga atakufa kwa upanga.+ 12 Nami nitaziwasha moto nyumba za* miungu ya Misri,+ naye ataiteketeza na kuichukua mateka. Atajifunika kwa nchi ya Misri kama mchungaji anavyojifunika kwa vazi lake, naye ataondoka huko kwa amani.* 13 Naye atazivunja vipandevipande nguzo za* Beth-shemeshi* katika nchi ya Misri, naye ataziteketeza kwa moto nyumba za* miungu ya Misri.”’”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki