Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Malaki 3
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Malaki—Yaliyomo

      • Bwana wa kweli aja kutakasa hekalu lake (1-5)

        • Mjumbe wa agano (1)

      • Washauriwa wamrudie Yehova (6-12)

        • Yehova habadiliki (6)

        • “Nirudieni, nami nitawarudia” (7)

        • ‘Leteni sehemu yote ya kumi, na Yehova atawamwagia baraka’ (10)

      • Mwadilifu na mwovu (13-18)

        • Majina yaandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Mungu (16)

        • Tofauti kati ya mwadilifu na mwovu (18)

Malaki 3:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “atatayarisha.”

Marejeo

  • +Mt 3:1-3; 11:7, 10; Mk 1:2-4; Lu 1:76; Yoh 1:6, 23; 3:28
  • +Zb 11:4

Malaki 3:2

Marejeo

  • +Isa 1:25; Yer 2:22

Malaki 3:3

Marejeo

  • +Zb 66:10; Met 25:4; Zek 13:9

Malaki 3:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “itamridhisha.”

Marejeo

  • +2Nya 7:1

Malaki 3:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mwepesi.”

  • *

    Tnn., “mtoto asiye na baba.”

  • *

    Au “wanaomnyima haki.”

Marejeo

  • +Kum 18:10, 12
  • +Kut 20:7
  • +Met 14:31; Yak 5:4
  • +Kum 24:17; Isa 1:17; Yak 1:27
  • +Kut 23:9; Zek 7:10

Malaki 3:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sijabadilika.”

Marejeo

  • +Isa 43:10; 46:4; Yak 1:17

Malaki 3:7

Marejeo

  • +Kum 9:7; Mdo 7:51
  • +Yer 3:12; Zek 1:3; Yak 4:8

Malaki 3:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Kwa laana mnanilaani.”

Malaki 3:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sehemu zote za.”

Marejeo

  • +Law 27:30; Kum 14:28
  • +2Nya 31:11; Ne 12:44; 13:10
  • +Kum 28:12
  • +Law 26:10; 2Nya 31:10; Met 3:9, 10

Malaki 3:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana ni pigo la wadudu.

Marejeo

  • +Kum 11:14; Zek 8:12

Malaki 3:12

Marejeo

  • +Isa 61:9

Malaki 3:13

Marejeo

  • +Mal 1:6

Malaki 3:14

Marejeo

  • +Ayu 21:14, 15; Zb 73:13, 14; Isa 58:3; Sef 1:12

Malaki 3:15

Marejeo

  • +Yer 12:1

Malaki 3:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanaolifikiria.” Au labda, “wanaolithamini.”

Marejeo

  • +Zb 56:8; 69:28
  • +Isa 26:8

Malaki 3:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mali ninayothamini sana.”

Marejeo

  • +Yer 31:33
  • +Isa 62:3; 1Pe 2:9
  • +Zb 103:13

Malaki 3:18

Marejeo

  • +Zb 58:10, 11

Jumla

Mal. 3:1Mt 3:1-3; 11:7, 10; Mk 1:2-4; Lu 1:76; Yoh 1:6, 23; 3:28
Mal. 3:1Zb 11:4
Mal. 3:2Isa 1:25; Yer 2:22
Mal. 3:3Zb 66:10; Met 25:4; Zek 13:9
Mal. 3:42Nya 7:1
Mal. 3:5Kum 18:10, 12
Mal. 3:5Kut 20:7
Mal. 3:5Met 14:31; Yak 5:4
Mal. 3:5Kum 24:17; Isa 1:17; Yak 1:27
Mal. 3:5Kut 23:9; Zek 7:10
Mal. 3:6Isa 43:10; 46:4; Yak 1:17
Mal. 3:7Kum 9:7; Mdo 7:51
Mal. 3:7Yer 3:12; Zek 1:3; Yak 4:8
Mal. 3:10Law 27:30; Kum 14:28
Mal. 3:102Nya 31:11; Ne 12:44; 13:10
Mal. 3:10Kum 28:12
Mal. 3:10Law 26:10; 2Nya 31:10; Met 3:9, 10
Mal. 3:11Kum 11:14; Zek 8:12
Mal. 3:12Isa 61:9
Mal. 3:13Mal 1:6
Mal. 3:14Ayu 21:14, 15; Zb 73:13, 14; Isa 58:3; Sef 1:12
Mal. 3:15Yer 12:1
Mal. 3:16Zb 56:8; 69:28
Mal. 3:16Isa 26:8
Mal. 3:17Yer 31:33
Mal. 3:17Isa 62:3; 1Pe 2:9
Mal. 3:17Zb 103:13
Mal. 3:18Zb 58:10, 11
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Malaki 3:1-18

Malaki

3 “Tazama! Ninamtuma mjumbe wangu, naye atafungua* njia mbele yangu.+ Na ghafla Bwana wa kweli, mnayemtafuta, atakuja katika hekalu lake;+ na mjumbe wa agano atakuja, mnayependezwa naye. Tazama! Kwa hakika atakuja,” asema Yehova wa majeshi.

2 “Lakini ni nani atakayestahimili siku atakayokuja, na ni nani atakayeweza kusimama atakapotokea? Kwa maana atakuwa kama moto wa msafishaji wa madini na kama sabuni+ ya wafuaji wa nguo. 3 Naye ataketi kama msafishaji na mtakasaji wa fedha,+ naye atawatakasa wana wa Lawi; atawasafisha kama dhahabu na kama fedha, nao hakika watakuwa watu wanaomtolea Yehova zawadi kwa uadilifu. 4 Na kwa kweli zawadi ya Yuda na Yerusalemu itampendeza* Yehova, kama ilivyokuwa katika siku za kale na kama ilivyokuwa katika miaka ya zamani za kale.+

5 “Nitawakaribia ili niwahukumu, nami nitakuwa shahidi asiyesita* dhidi ya walozi,+ dhidi ya wazinzi, dhidi ya watu wanaotoa viapo vya uwongo,+ dhidi ya wale wanaomlaghai kibarua,+ mjane, na yatima,*+ na dhidi ya wale wanaokataa kumsaidia* mgeni.+ Watu hao hawaniogopi,” asema Yehova wa majeshi.

6 “Kwa maana mimi ni Yehova; sibadiliki.*+ Nanyi ni wana wa Yakobo; bado hamjaangamia. 7 Tangu siku za mababu zenu mmegeuka na kuacha masharti yangu nanyi hamjayashika.+ Nirudieni, nami nitawarudia,”+ asema Yehova wa majeshi.

Lakini mnauliza: “Tukurudie jinsi gani?”

8 “Je, mwanadamu anaweza kumwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia.”

Nanyi mnauliza: “Tumekuibia jinsi gani?”

“Katika sehemu za kumi na michango. 9 Kwa hakika mmelaaniwa,* kwa maana mnaniibia—naam, taifa zima linafanya hivyo. 10 Leteni ghalani sehemu yote ya* kumi,+ ili kuwe na chakula nyumbani mwangu;+ tafadhali, nijaribuni kwa njia hii,” asema Yehova wa majeshi, “mwone kama sitawafungulia malango ya mbinguni ya mafuriko+ na kuwamwagia baraka hivi kwamba hamtakosa chochote.”+

11 “Na kwa ajili yenu nitamkemea yule anayenyafua,* naye hataharibu mazao ya nchi yenu, wala mzabibu wa shamba lenu hautakosa matunda,”+ asema Yehova wa majeshi.

12 “Mataifa yote yatalazimika kuwatangaza ninyi kuwa wenye furaha,+ kwa maana mtakuwa nchi ya kupendeza,” asema Yehova wa majeshi.

13 “Maneno yenu dhidi yangu yamekuwa makali,” asema Yehova.

Nanyi mnauliza: “Ni katika njia gani tumesema maneno makali dhidi yako miongoni mwetu?”+

14 “Mnasema, ‘Hakuna faida yoyote ya kumtumikia Mungu.+ Tumefaidikaje kwa kutimiza wajibu wetu kwake na kutembea kwa huzuni mbele za Yehova wa majeshi? 15 Sasa tunawaona watu wenye kimbelembele kuwa wenye furaha. Pia, watu wanaotenda maovu wanafanikiwa.+ Wanathubutu kumjaribu Mungu, nao hawaadhibiwi.’”

16 Wakati huo wale wanaomwogopa Yehova walizungumza kila mmoja na mwenzake, na Yehova akaendelea kuwakazia uangalifu na kusikiliza. Na kitabu cha kumbukumbu kikaandikwa mbele zake+ kwa ajili ya wale wanaomwogopa Yehova na wale wanaolitafakari* jina lake.+

17 “Nao watakuwa wangu,”+ asema Yehova wa majeshi, “siku nitakayotokeza mali ya pekee.*+ Nitawahurumia, kama mwanamume anavyomhurumia mwana wake anayemtumikia.+ 18 Nanyi mtaona tena tofauti kati ya mtu mwadilifu na mtu mwovu,+ kati ya yule anayemtumikia Mungu na yule asiyemtumikia.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki