Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Luka 17
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Luka—Yaliyomo

      • Kukwazika, msamaha, na imani (1-6)

      • Watumwa wasiofaa kitu (7-10)

      • Watu kumi wenye ukoma waponywa (11-19)

      • Kuja kwa Ufalme wa Mungu (20-37)

        • “Ufalme wa Mungu uko katikati yenu.” (21)

        • “Mkumbukeni mke wa Loti” (32)

Luka 17:2

Marejeo

  • +Mt 18:6; Mk 9:42

Luka 17:3

Marejeo

  • +Met 17:10
  • +Law 19:17; Mt 18:15

Luka 17:4

Marejeo

  • +Isa 55:7; Mt 6:12; 18:21, 22; Kol 3:13; 1Pe 4:8

Luka 17:5

Marejeo

  • +Mk 9:23, 24; Ebr 12:2

Luka 17:6

Marejeo

  • +Mt 17:20; 21:21; Mk 11:23

Luka 17:10

Marejeo

  • +1Ko 9:16

Luka 17:12

Marejeo

  • +Law 13:45, 46

Luka 17:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “tuonyeshe rehema!”

Luka 17:14

Marejeo

  • +Law 14:2-4; Kum 24:8; Mt 8:3, 4; Lu 5:13, 14
  • +2Fa 5:1, 14

Luka 17:16

Marejeo

  • +2Fa 17:24; Yoh 4:9

Luka 17:19

Marejeo

  • +Mt 9:22; Mk 5:34; Lu 7:50

Luka 17:20

Marejeo

  • +Mt 24:3

Luka 17:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “uko miongoni mwenu.”

Marejeo

  • +Mt 12:28; 21:5

Luka 17:23

Marejeo

  • +Mt 24:23; Mk 13:21; Lu 21:8; 1Yo 4:1

Luka 17:24

Marejeo

  • +Da 7:13
  • +Mt 24:27

Luka 17:25

Marejeo

  • +Mk 8:31; 9:31; Lu 9:22

Luka 17:26

Marejeo

  • +Mwa 6:5
  • +Mt 24:37-39

Luka 17:27

Marejeo

  • +Mwa 7:7
  • +Mwa 7:17, 21

Luka 17:28

Marejeo

  • +Mwa 19:15

Luka 17:29

Marejeo

  • +Mwa 19:24, 25

Luka 17:30

Marejeo

  • +1Ko 1:7; 2Th 1:7, 8

Luka 17:32

Marejeo

  • +Mwa 19:17, 26

Luka 17:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yake.”

Marejeo

  • +Mt 10:39; 16:25; Mk 8:35; Lu 9:24; Yoh 12:25

Luka 17:34

Marejeo

  • +Mt 24:40, 41

Luka 17:36

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A3.

Luka 17:37

Marejeo

  • +Mt 24:28

Jumla

Luka 17:2Mt 18:6; Mk 9:42
Luka 17:3Met 17:10
Luka 17:3Law 19:17; Mt 18:15
Luka 17:4Isa 55:7; Mt 6:12; 18:21, 22; Kol 3:13; 1Pe 4:8
Luka 17:5Mk 9:23, 24; Ebr 12:2
Luka 17:6Mt 17:20; 21:21; Mk 11:23
Luka 17:101Ko 9:16
Luka 17:12Law 13:45, 46
Luka 17:14Law 14:2-4; Kum 24:8; Mt 8:3, 4; Lu 5:13, 14
Luka 17:142Fa 5:1, 14
Luka 17:162Fa 17:24; Yoh 4:9
Luka 17:19Mt 9:22; Mk 5:34; Lu 7:50
Luka 17:20Mt 24:3
Luka 17:21Mt 12:28; 21:5
Luka 17:23Mt 24:23; Mk 13:21; Lu 21:8; 1Yo 4:1
Luka 17:24Da 7:13
Luka 17:24Mt 24:27
Luka 17:25Mk 8:31; 9:31; Lu 9:22
Luka 17:26Mwa 6:5
Luka 17:26Mt 24:37-39
Luka 17:27Mwa 7:7
Luka 17:27Mwa 7:17, 21
Luka 17:28Mwa 19:15
Luka 17:29Mwa 19:24, 25
Luka 17:301Ko 1:7; 2Th 1:7, 8
Luka 17:32Mwa 19:17, 26
Luka 17:33Mt 10:39; 16:25; Mk 8:35; Lu 9:24; Yoh 12:25
Luka 17:34Mt 24:40, 41
Luka 17:37Mt 24:28
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Luka 17:1-37

Kulingana na Luka

17 Ndipo akawaambia wanafunzi wake: “Lazima vikwazo vije. Hata hivyo, ole wake mtu atakayevisababisha! 2 Ingekuwa afadhali kwake kama angefungiwa shingoni jiwe la kusagia kisha atupwe baharini kuliko amkwaze mmoja wa hawa wadogo.+ 3 Jiangalieni ninyi wenyewe. Ndugu yako akitenda dhambi mkemee,+ na akitubu, msamehe.+ 4 Hata akikutendea dhambi mara saba kwa siku, naye anarudi kwako mara saba akisema, ‘ninatubu,’ unapaswa kumsamehe.”+

5 Mitume wakamwambia Bwana: “Tusaidie tuwe na imani zaidi.”+ 6 Bwana akasema: “Kama mngekuwa na imani inayolingana na mbegu ya haradali, mngeuambia mti huu wa mforsadi, ‘Ng’oka ukapandwe baharini!’ nao ungewatii.+

7 “Ni nani kati yenu aliye na mtumwa anayelima shamba au kuchunga wanyama, ambaye akirudi kutoka shambani, atamwambia ‘Njoo upesi, keti ule chakula’? 8 Hapana. Badala yake atamwambia, ‘Nitayarishie chakula cha jioni, na ujifunge vazi la kazi ili unihudumie mpaka nitakapomaliza kula na kunywa, kisha unaweza kula na kunywa.’ 9 Je, utamshukuru mtumwa huyo kwa sababu alifanya mambo uliyomwagiza? 10 Vivyo hivyo, baada ya kufanya mambo mliyoagizwa, semeni: ‘Sisi ni watumwa wasiofaa kitu. Tumefanya kile tulichopaswa kufanya.’”+

11 Alipokuwa akienda Yerusalemu, alipita kati ya Samaria na Galilaya. 12 Alipokuwa akiingia katika kijiji fulani alikutana na wanaume kumi wenye ukoma, lakini walisimama mbali naye.+ 13 Kisha wakasema kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwalimu, tuhurumie!”* 14 Alipowaona, akawaambia: “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.”+ Basi walipokuwa wakienda wakatakaswa.+ 15 Mmoja wao alipoona amepona, akarudi akimtukuza Mungu kwa sauti kubwa. 16 Akaanguka kifudifudi miguuni pa Yesu na kumshukuru. Isitoshe, alikuwa Msamaria.+ 17 Yesu akauliza: “Wote kumi walitakaswa, sivyo? Basi, wako wapi wale wengine tisa? 18 Je, hakuna mwingine aliyerudi ili kumtukuza Mungu isipokuwa mtu huyu wa taifa lingine?” 19 Kisha akamwambia: “Simama uende; imani yako imekuponya.”+

20 Mafarisayo walipomuuliza Ufalme wa Mungu utakuja lini,+ aliwajibu: “Ufalme wa Mungu hautakuja ukionekana waziwazi; 21 wala watu hawatasema, ‘Tazama! uko hapa!’ au, ‘Uko pale!’ Kwa maana tazama! Ufalme wa Mungu uko katikati yenu.”*+

22 Kisha akawaambia wanafunzi: “Siku zitafika ambapo mtatamani kuona moja kati ya siku za Mwana wa binadamu lakini hamtaiona. 23 Na watu watawaambia, ‘Angalia pale!’ au, ‘Angalia hapa!’ Msiende wala msiwafuate.+ 24 Kwa maana kama radi inavyong’aa kutoka sehemu moja ya mbingu mpaka sehemu nyingine, ndivyo Mwana wa binadamu+ atakavyokuwa katika siku yake.+ 25 Hata hivyo, kwanza lazima apatwe na mateso mengi na kukataliwa na kizazi hiki.+ 26 Isitoshe, kama ilivyokuwa katika siku za Noa,+ ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa binadamu:+ 27 walikuwa wakila, walikuwa wakinywa, wanaume walikuwa wakioa na wanawake wakiolewa, mpaka siku ambayo Noa aliingia ndani ya safina,+ na Gharika ikaja na kuwaangamiza wote.+ 28 Vivyo hivyo, kama ilivyokuwa katika siku za Loti:+ walikuwa wakila, walikuwa wakinywa, walikuwa wakinunua, walikuwa wakiuza, walikuwa wakipanda, na walikuwa wakijenga. 29 Lakini siku ambayo Loti alitoka Sodoma, kulinyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni na wote wakaangamizwa.+ 30 Ndivyo itakavyokuwa siku ambayo Mwana wa binadamu atafunuliwa.+

31 “Siku hiyo mtu aliye kwenye paa la nyumba asishuke kuchukua mali iliyo ndani ya nyumba yake, vivyo hivyo mtu aliye shambani, asirudi kwenye vitu vilivyo nyuma. 32 Mkumbukeni mke wa Loti.+ 33 Yeyote anayetaka kuuokoa uhai wake* ataupoteza, lakini yeyote anayeupoteza atauokoa.+ 34 Ninawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atachukuliwa, lakini mwingine ataachwa.+⁠ 35 Wanawake wawili watakuwa wakisaga kwenye jiwe moja la kusagia; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.” 36* —— 37 Basi wakamuuliza: “Wapi, Bwana?” Akawajibu: “Mahali palipo na mzoga, hapo ndipo tai watakapokusanyika.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki