Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matendo 18
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Matendo—Yaliyomo

      • Huduma ya Paulo huko Korintho (1-17)

      • Kurudi Antiokia ya Siria (18-22)

      • Paulo aenda Galatia na Frigia (23)

      • Apolo mwenye ufasaha asaidiwa (24-28)

Matendo 18:2

Marejeo

  • +Mdo 18:24, 26; 1Ko 16:19; 2Ti 4:19

Matendo 18:3

Marejeo

  • +Mdo 20:34; 1Ko 4:11, 12; 9:15; 1Th 2:9; 2Th 3:8, 10

Matendo 18:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Alikuwa akijadiliana nao.”

Marejeo

  • +Mt 4:23
  • +Mdo 17:2

Matendo 18:5

Marejeo

  • +Mdo 15:27; 17:14
  • +Mdo 16:1, 2; 1Th 3:6
  • +Mdo 17:2, 3; 28:23

Matendo 18:6

Marejeo

  • +Mt 10:14
  • +Eze 33:4
  • +Mdo 20:26
  • +Mdo 13:46; 28:28; Ro 1:16

Matendo 18:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, sinagogi.

Matendo 18:8

Marejeo

  • +1Ko 1:14

Matendo 18:10

Marejeo

  • +Mt 28:20

Matendo 18:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Gavana Mroma aliyetawala mkoa. Angalia Kamusi.

Matendo 18:15

Marejeo

  • +Mdo 23:29; 25:19

Matendo 18:17

Marejeo

  • +1Ko 1:1

Matendo 18:18

Marejeo

  • +Ro 16:1

Matendo 18:19

Marejeo

  • +Mdo 17:2

Matendo 18:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Matendo 18:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana alienda Yerusalemu.

Marejeo

  • +Mdo 15:36

Matendo 18:23

Marejeo

  • +Mdo 16:6
  • +Mdo 14:21, 22; 15:32

Matendo 18:24

Marejeo

  • +Mdo 19:1; 1Ko 1:12; 3:5, 6

Matendo 18:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “amefundishwa kwa mdomo.”

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Matendo 18:26

Marejeo

  • +Ro 16:3; 1Ko 16:19

Matendo 18:28

Marejeo

  • +Kum 18:15; Zb 16:10; Isa 7:14; Mik 5:2

Jumla

Mdo. 18:2Mdo 18:24, 26; 1Ko 16:19; 2Ti 4:19
Mdo. 18:3Mdo 20:34; 1Ko 4:11, 12; 9:15; 1Th 2:9; 2Th 3:8, 10
Mdo. 18:4Mt 4:23
Mdo. 18:4Mdo 17:2
Mdo. 18:5Mdo 15:27; 17:14
Mdo. 18:5Mdo 16:1, 2; 1Th 3:6
Mdo. 18:5Mdo 17:2, 3; 28:23
Mdo. 18:6Mt 10:14
Mdo. 18:6Eze 33:4
Mdo. 18:6Mdo 20:26
Mdo. 18:6Mdo 13:46; 28:28; Ro 1:16
Mdo. 18:81Ko 1:14
Mdo. 18:10Mt 28:20
Mdo. 18:15Mdo 23:29; 25:19
Mdo. 18:171Ko 1:1
Mdo. 18:18Ro 16:1
Mdo. 18:19Mdo 17:2
Mdo. 18:22Mdo 15:36
Mdo. 18:23Mdo 16:6
Mdo. 18:23Mdo 14:21, 22; 15:32
Mdo. 18:24Mdo 19:1; 1Ko 1:12; 3:5, 6
Mdo. 18:26Ro 16:3; 1Ko 16:19
Mdo. 18:28Kum 18:15; Zb 16:10; Isa 7:14; Mik 5:2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Matendo 18:1-28

Matendo ya Mitume

18 Baada ya hayo, akatoka Athene na kwenda Korintho. 2 Naye akamkuta Myahudi aliyeitwa Akila,+ mzaliwa wa Ponto aliyekuwa amekuja hivi karibuni kutoka Italia na Prisila mke wake, kwa sababu Klaudio alikuwa ameagiza Wayahudi wote waondoke Roma. Basi akaenda kwao, 3 na kwa sababu walifanya kazi ileile, akakaa nyumbani kwao na kufanya kazi pamoja nao,+ kwa maana kazi yao ilikuwa ya kutengeneza mahema. 4 Alikuwa akitoa hotuba* katika sinagogi+ kila sabato+ na kuwashawishi Wayahudi na Wagiriki.

5 Basi, Sila+ na Timotheo+ waliposhuka kutoka Makedonia, Paulo akaanza kushughulika sana na lile neno, akiwatolea Wayahudi ushahidi ili kuthibitisha kwamba Yesu ndiye Kristo.+ 6 Lakini walipoendelea kumpinga na kumtukana, akayakung’uta mavazi yake+ na kuwaambia: “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu wenyewe.+ Mimi ni safi.+ Kuanzia sasa nitaenda kwa watu wa mataifa.”+ 7 Basi akatoka humo* na kuingia katika nyumba ya mwanamume aliyeitwa Titio Yusto, mwabudu wa Mungu, ambaye nyumba yake ilikuwa imeshikana na sinagogi. 8 Lakini Krispo,+ ofisa msimamizi wa sinagogi akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake. Na Wakorintho wengi waliosikia wakaanza kuamini na kubatizwa. 9 Isitoshe, Bwana akamwambia Paulo katika maono usiku: “Usiogope, bali endelea kusema na usinyamaze, 10 kwa sababu niko pamoja nawe+ na hakuna mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana nina watu wengi katika jiji hili.” 11 Basi akakaa huko kwa mwaka mmoja na miezi sita, akifundisha neno la Mungu kati yao.

12 Galio alipokuwa liwali* wa Akaya, Wayahudi wakaungana, wakamshambulia Paulo na kumpeleka kwenye kiti cha hukumu, 13 wakisema: “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kwa njia iliyo kinyume cha sheria.” 14 Lakini Paulo alipokuwa karibu kuzungumza, Galio akawaambia Wayahudi: “Enyi Wayahudi, kama kweli lingekuwa kosa fulani au uhalifu mkubwa, ningekuwa na sababu ya kuwasikiliza kwa subira. 15 Lakini kama mnabishania maneno na majina na sheria yenu,+ amueni wenyewe. Mimi sitaki kuwa mwamuzi wa mambo hayo.” 16 Ndipo akawafukuza kutoka mbele ya kiti cha hukumu. 17 Basi wote wakamkamata Sosthene,+ ofisa msimamizi wa sinagogi na kuanza kumpiga mbele ya kiti cha hukumu. Lakini Galio hakujihusisha kamwe na mambo hayo.

18 Hata hivyo, baada ya kukaa siku kadhaa, Paulo aliwaaga akina ndugu naye akasafiri baharini kwenda Siria, pamoja na Prisila na Akila. Alikuwa amekata nywele zake huko Kenkrea,+ kwa sababu alikuwa ameweka nadhiri. 19 Basi wakafika Efeso, akawaacha huko; lakini yeye akaingia ndani ya sinagogi na kujadiliana na Wayahudi.+ 20 Ingawa waliendelea kumsihi akae kwa muda mrefu zaidi, hakukubali 21 bali aliwaaga na kuwaambia: “Nitarudi kwenu tena, Yehova* akipenda.” Naye akasafiri baharini kutoka Efeso 22 na kushuka mpaka Kaisaria. Akapanda kwenda na kulisalimia kutaniko,* kisha akashuka kwenda Antiokia.+

23 Baada ya kukaa huko kwa muda fulani, akaondoka na kwenda sehemu mbalimbali katika nchi ya Galatia na Frigia,+ akiwaimarisha wanafunzi wote.+

24 Sasa Myahudi aliyeitwa Apolo,+ mzaliwa wa Aleksandria akafika Efeso; alikuwa mwanamume mwenye ufasaha na ujuzi mwingi wa Maandiko. 25 Mwanamume huyu alikuwa amefundishwa* njia ya Yehova,* na akiwa amewaka roho, alikuwa akizungumza na kufundisha kwa usahihi kumhusu Yesu, lakini alifahamu ubatizo wa Yohana tu. 26 Akaanza kuzungumza kwa ujasiri katika sinagogi, nao Prisila na Akila+ walipomsikia, wakamchukua na kumfafanulia kwa usahihi zaidi njia ya Mungu. 27 Pia, kwa sababu alitaka kuvuka kwenda Akaya, akina ndugu wakawaandikia wanafunzi wakiwahimiza wamkaribishe kwa fadhili. Basi alipofika huko, akawasaidia sana wale ambao kupitia fadhili zisizostahiliwa za Mungu walikuwa wameamini; 28 kwa maana alithibitisha kikamili hadharani na kwa juhudi nyingi kwamba Wayahudi walikuwa wamekosea, na kuwaonyesha kwa Maandiko kuwa Yesu ndiye Kristo.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki