-
Kutoka 20:14Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 “Usifanye uzinzi.+
-
-
Mambo ya Walawi 20:10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
10 “‘Ifuatayo ni sheria kuhusu mwanamume anayefanya uzinzi na mke wa mwanamume mwingine: Mwanamume anayefanya uzinzi na mke wa mwenzake lazima auawe; mwanamume huyo na mwanamke aliyefanya naye uzinzi lazima wauawe.+
-
-
Kumbukumbu la Torati 22:22Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
22 “Mwanamume akipatikana akifanya ngono na mke wa mwanamume mwingine, ni lazima wote wawili wauawe pamoja, mwanamume huyo pamoja na mwanamke aliyefanya naye ngono.+ Kwa hiyo ni lazima mwondoe uovu katika Israeli.
-
-
Methali 6:29Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
29 Ndivyo ilivyo kwa mtu yeyote anayelala na mke wa jirani yake;
Hakuna yeyote anayemgusa mwanamke huyo atakayekosa kuadhibiwa.+
-