-
Kutoka 35:21Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
21 Basi kila mtu ambaye moyo wake ulimsukuma+ na kila mtu aliyechochewa na roho yake akaja na kumletea Yehova mchango ili utumiwe katika kazi ya hema la mkutano, yaani, katika utumishi wake wote, na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
-
-
1 Mambo ya Nyakati 29:9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
9 Watu walishangilia kwa sababu walitoa matoleo hayo ya hiari, kwa maana walimtolea Yehova matoleo hayo ya hiari kwa moyo kamili,+ na Mfalme Daudi pia alishangilia sana.
-
-
Ezra 7:14-16Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 Kwa maana umetumwa na mfalme na washauri wake saba ili kuchunguza kama watu walio Yuda na Yerusalemu wanafuata Sheria ya Mungu wako uliyo nayo,* 15 na kuchukua fedha na dhahabu ambayo mfalme na washauri wake wamemtolea kwa hiari Mungu wa Israeli, ambaye makao yake yako Yerusalemu, 16 pamoja na fedha na dhahabu yote ambayo utapokea* katika mkoa wote* wa Babiloni, na pia zawadi ambazo watu na makuhani hutoa kwa hiari kwa ajili ya nyumba ya Mungu wao iliyo Yerusalemu.+
-