-
Kumbukumbu la Torati 15:7, 8Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 “Ikiwa mmoja wa ndugu zenu atakuwa maskini miongoni mwenu katika mojawapo ya majiji yaliyo katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, msiifanye mioyo yenu iwe migumu au kumfumbia mkono ndugu yenu maskini.+ 8 Kwa maana mnapaswa kumfumbulia mkono wenu kwa ukarimu+ na kufanya yote mwezayo kumkopesha* chochote anachohitaji au alichopungukiwa.
-
-
Methali 28:27Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
27 Yeyote anayewapa maskini hatakosa chochote,+
Lakini yule anayewafumbia macho atapata laana nyingi.
-