-
Kumbukumbu la Torati 30:1-3Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
30 “Maneno haya yote yatakapotimia kwenu, baraka na laana ambayo nimeweka mbele yenu,+ nanyi myakumbuke*+ katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu atawatawanya,+ 2 nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu+ na kuisikiliza sauti yake kulingana na yote ninayowaamuru leo, ninyi na wana wenu, kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote,+ 3 ndipo Yehova Mungu wenu atakapowarudisha mateka wenu+ na kuwaonyesha ninyi rehema+ na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu aliwatawanya.+
-
-
Isaya 66:20Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
20 Watawaleta ndugu zenu wote kutoka katika mataifa yote+ wawe zawadi kwa Yehova, wakiwa juu ya farasi, ndani ya magari ya vita, ndani ya magari ya kukokotwa yaliyofunikwa, juu ya nyumbu, juu ya ngamia wenye kasi, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu, Yerusalemu,” asema Yehova, “kama watu wa Israeli wanavyoleta zawadi zao ndani ya nyumba ya Yehova zikiwa katika chombo safi.”
-
-
Ezekieli 36:24Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
24 Nitawatoa kutoka kwa mataifa na kuwakusanya kutoka katika nchi zote na kuwaleta katika nchi yenu.+
-
-
Mika 2:12Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
12 Kwa hakika nitawakusanya ninyi nyote, enyi watu wa Yakobo;
Kwa kweli nitawakusanya pamoja wale wanaobaki wa Israeli.+
-