Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 66
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Ibada ya kweli na ibada ya uwongo (1-6)

      • Sayuni na wanawe (7-17)

      • Watu wakusanyika Yerusalemu ili kuabudu (18-24)

Isaya 66:1

Marejeo

  • +Mt 5:34, 35
  • +2Nya 6:18; Mdo 17:24
  • +1Nya 28:2; Mdo 7:48-50

Isaya 66:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “anayelihangaikia.”

Marejeo

  • +Isa 40:26
  • +2Fa 22:18, 19; Lu 18:14

Isaya 66:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “yule anayeisifu sanamu.”

  • *

    Au “Na nafsi zao zinapenda.”

Marejeo

  • +Isa 1:11
  • +Law 11:27
  • +Kum 14:8
  • +Law 2:1, 2
  • +Isa 1:13

Isaya 66:4

Marejeo

  • +Kum 28:15
  • +Yer 7:13
  • +2Fa 21:9; Isa 65:3

Isaya 66:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mnaolihangaikia.”

Marejeo

  • +Isa 5:18, 19; 29:13
  • +Isa 65:13, 14; Yer 17:13, 18

Isaya 66:7

Marejeo

  • +Isa 54:1

Isaya 66:10

Marejeo

  • +Isa 44:23
  • +Zb 137:6

Isaya 66:12

Marejeo

  • +Isa 9:7
  • +Isa 60:3; Hag 2:7

Isaya 66:13

Marejeo

  • +Isa 51:3
  • +Isa 44:28; 65:18, 19

Isaya 66:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nguvu za Yehova zitajulikana.”

Marejeo

  • +Isa 59:18

Isaya 66:15

Marejeo

  • +Kum 4:24
  • +Zb 50:3; Yer 25:32, 33
  • +2Th 1:7, 8

Isaya 66:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanadamu wote.”

Isaya 66:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, bustani za pekee zilizotumiwa kwa ajili ya ibada ya sanamu.

Marejeo

  • +Isa 1:29; 65:3
  • +Law 11:7, 8; Isa 65:4
  • +Law 11:29

Isaya 66:19

Marejeo

  • +Mwa 10:4
  • +Mwa 10:6, 13
  • +Mwa 10:2; Eze 27:12, 13
  • +Isa 60:3; Mal 1:11

Isaya 66:20

Marejeo

  • +Kum 30:1-3; Isa 11:16; 43:6; 60:4, 9

Isaya 66:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mbegu yenu.”

Marejeo

  • +Isa 65:17, 18; 2Pe 3:13; Ufu 21:1
  • +Isa 65:23; Yer 31:35, 36

Isaya 66:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Wanadamu wote.”

  • *

    Au “kuabudu.”

Marejeo

  • +Zb 86:9; Zek 14:16; Mal 1:11

Isaya 66:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wote wenye mwili.”

Marejeo

  • +Isa 34:10; Mt 25:41; Mk 9:47, 48; 2Th 1:9

Jumla

Isa. 66:1Mt 5:34, 35
Isa. 66:12Nya 6:18; Mdo 17:24
Isa. 66:11Nya 28:2; Mdo 7:48-50
Isa. 66:2Isa 40:26
Isa. 66:22Fa 22:18, 19; Lu 18:14
Isa. 66:3Isa 1:11
Isa. 66:3Law 11:27
Isa. 66:3Kum 14:8
Isa. 66:3Law 2:1, 2
Isa. 66:3Isa 1:13
Isa. 66:4Kum 28:15
Isa. 66:4Yer 7:13
Isa. 66:42Fa 21:9; Isa 65:3
Isa. 66:5Isa 5:18, 19; 29:13
Isa. 66:5Isa 65:13, 14; Yer 17:13, 18
Isa. 66:7Isa 54:1
Isa. 66:10Isa 44:23
Isa. 66:10Zb 137:6
Isa. 66:12Isa 9:7
Isa. 66:12Isa 60:3; Hag 2:7
Isa. 66:13Isa 51:3
Isa. 66:13Isa 44:28; 65:18, 19
Isa. 66:14Isa 59:18
Isa. 66:15Kum 4:24
Isa. 66:15Zb 50:3; Yer 25:32, 33
Isa. 66:152Th 1:7, 8
Isa. 66:17Isa 1:29; 65:3
Isa. 66:17Law 11:7, 8; Isa 65:4
Isa. 66:17Law 11:29
Isa. 66:19Mwa 10:4
Isa. 66:19Mwa 10:6, 13
Isa. 66:19Mwa 10:2; Eze 27:12, 13
Isa. 66:19Isa 60:3; Mal 1:11
Isa. 66:20Kum 30:1-3; Isa 11:16; 43:6; 60:4, 9
Isa. 66:22Isa 65:17, 18; 2Pe 3:13; Ufu 21:1
Isa. 66:22Isa 65:23; Yer 31:35, 36
Isa. 66:23Zb 86:9; Zek 14:16; Mal 1:11
Isa. 66:24Isa 34:10; Mt 25:41; Mk 9:47, 48; 2Th 1:9
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 66:1-24

Isaya

66 Yehova anasema hivi:

“Mbingu ni kiti changu cha ufalme, na dunia ni kiti cha miguu yangu.+

Hivyo basi, iko wapi nyumba mnayoweza kunijengea,+

Na pako wapi mahali pangu pa kupumzikia?”+

 2 “Sasa mkono wangu mwenyewe uliumba vitu hivi vyote,

Na vitu vyote vilikuja kuwapo kwa njia hiyo,” asema Yehova.+

“Basi, nitamtazama huyu,

Yule aliye mnyenyekevu na aliyevunjika rohoni na anayelitetemekea* neno langu.+

 3 Anayemchinja ng’ombe dume ni kama yule anayemuua mwanadamu.+

Anayemchinja kondoo ni kama yule anayevunja shingo ya mbwa.+

Anayetoa zawadi—kama damu ya nguruwe!+

Anayetoa toleo la ubani la ukumbusho+ ni kama yule anayebariki kwa maneno ya uchawi.*+

Wamechagua njia zao wenyewe,

Nao wanapenda* mambo yanayochukiza.

 4 Basi nitachagua njia za kuwaadhibu,+

Nami nitawaletea mambo yaleyale wanayoogopa sana.

Kwa sababu nilipoita, hakuna aliyejibu;

Nilipozungumza, hakuna aliyesikiliza.+

Waliendelea kutenda maovu machoni pangu,

Nao wakachagua kufanya mambo yaliyonichukiza.”+

 5 Sikieni neno la Yehova, ninyi mnaolitetemekea* neno lake:

“Ndugu zenu wanaowachukia na kuwatenga kwa sababu ya jina langu, walisema, ‘Yehova na atukuzwe!’+

Lakini atatokea na kuwaletea shangwe,

Nao ndio watakaoaibishwa.”+

 6 Kuna sauti ya ghasia kutoka jijini, sauti kutoka hekaluni!

Ni sauti ya Yehova akiwalipa maadui wake kile wanachostahili.

 7 Kabla hajawa na uchungu wa kuzaa, alizaa.+

Kabla ya kushikwa na uchungu wa kuzaa, alijifungua mtoto wa kiume.

 8 Ni nani amewahi kusikia jambo kama hilo?

Ni nani ameona mambo kama hayo?

Je, nchi itazaliwa katika siku moja?

Au, je, taifa lote litazaliwa mara moja?

Hata hivyo, mara tu Sayuni aliposhikwa na uchungu wa kuzaa, aliwazaa wanawe.

 9 “Je, nimfanye mtoto akaribie kuzaliwa kisha nifanye asizaliwe?” asema Yehova.

“Au, je, nisababishe afikie hatua ya kuzaliwa kisha nifunge tumbo la uzazi?” asema Mungu wako.

10 Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi pamoja naye,+ ninyi nyote mnaompenda.+

Furahini sana pamoja naye, ninyi nyote mnaomwombolezea,

11 Kwa maana mtanyonya na kushiba kabisa maziwa ya titi lake la faraja,

Nanyi mtakunywa sana na kufurahia utukufu wake mwingi.

12 Kwa maana Yehova anasema hivi:

“Tazama, ninampa amani kama mto+

Na utukufu wa mataifa kama mto unaofurika.+

Mtanyonya na kubebwa kiunoni,

Nanyi mtachezeshwa kwenye magoti yake.

13 Kama mama anavyomfariji mwanawe,

Ndivyo nitakavyoendelea kuwafariji;+

Nanyi mtafarijiwa kwa sababu ya Yerusalemu.+

14 Mtaona jambo hilo, na moyo wenu utashangilia,

Mifupa yenu itanawiri kama majani mabichi.

Na mkono wa Yehova utajulikana* kwa watumishi wake,

Lakini atawashutumu maadui wake.”+

15 “Kwa maana Yehova atakuja kama moto,+

Na magari yake ya vita kama upepo wa dhoruba,+

Ili kulipa kwa hasira kali,

Ili kukemea kwa miali ya moto.+

16 Kwa maana Yehova atatekeleza hukumu kwa moto,

Naam, kwa upanga wake, dhidi ya wote wenye mwili;*

Na watakaouawa na Yehova watakuwa wengi.

17 “Wale wanaojitakasa na kujisafisha ili waingie kwenye bustani*+ wakimfuata yule aliye katikati, wale wanaokula nyama ya nguruwe+ na vitu vinavyochukiza na panya,+ wote watafikia mwisho wao pamoja,” asema Yehova. 18 “Kwa kuwa ninajua kazi zao na mawazo yao, ninakuja kuwakusanya watu wa mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.”

19 “Nitaweka ishara miongoni mwao, nami nitawapeleka baadhi ya wale wanaoponyoka waende kwa mataifa—waende Tarshishi,+ Pulu, na Ludi,+ wale wanaouvuta upinde, waende Tubali na Yavani,+ na kwenye visiwa vilivyo mbali sana—mataifa ambayo hayajasikia habari kunihusu wala kuuona utukufu wangu; nao watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.+ 20 Watawaleta ndugu zenu wote kutoka katika mataifa yote+ wawe zawadi kwa Yehova, wakiwa juu ya farasi, ndani ya magari ya vita, ndani ya magari ya kukokotwa yaliyofunikwa, juu ya nyumbu, juu ya ngamia wenye kasi, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu, Yerusalemu,” asema Yehova, “kama watu wa Israeli wanavyoleta zawadi zao ndani ya nyumba ya Yehova zikiwa katika chombo safi.”

21 “Pia nitawachukua baadhi yao wawe makuhani na Walawi,” asema Yehova.

22 “Kwa maana kama vile mbingu mpya na dunia mpya+ ninazoumba zitakavyoendelea kusimama mbele zangu,” asema Yehova, “ndivyo uzao wenu* na jina lenu litakavyoendelea kudumu.”+

23 “Na kutoka mwezi mpya mpaka mwezi mpya na kutoka sabato mpaka sabato,

Wote wenye mwili* wataingia ili kuinama chini* mbele zangu,”+ asema Yehova.

24 “Nao watatoka nje na kuzitazama maiti za watu walioniasi;

Kwa maana funza walio juu yao hawatakufa,

Na moto wao hautazimwa,+

Nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa watu wote.”*

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki