-
Kutoka 3:11, 12Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
11 Hata hivyo, Musa akamwambia Mungu wa kweli: “Mimi ni nani hata niende kwa Farao na kuwatoa Waisraeli nchini Misri?” 12 Mungu akamwambia: “Nitathibitika kuwa pamoja nawe,+ na hii ndiyo ishara itakayoonyesha kwamba ni mimi niliyekutuma: Baada ya kuwatoa Waisraeli nchini Misri, ninyi mtanitumikia* mimi, Mungu wa kweli, kwenye mlima huu.”+
-
-
Matendo 18:9, 10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
9 Isitoshe, Bwana akamwambia Paulo katika maono usiku: “Usiogope, bali endelea kusema na usinyamaze, 10 kwa sababu niko pamoja nawe+ na hakuna mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana nina watu wengi katika jiji hili.”
-