Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 14:1-5
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 14 Wakati huo Herode, mtawala wa wilaya,* akasikia habari kumhusu Yesu.+ 2 Akawaambia watumishi wake: “Huyu ni Yohana Mbatizaji. Alifufuliwa kutoka kwa wafu na ndiyo sababu anafanya matendo yenye nguvu.”+ 3 Herode* alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo ndugu yake.+ 4 Kwa maana Yohana alikuwa akimwambia: “Si halali kwako kuwa na mwanamke huyo.”+ 5 Hata hivyo, ingawa Herode alitaka kumuua, aliuogopa umati, kwa sababu walimwona kuwa nabii.+

  • Luka 9:7-9
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 7 Basi Herode* mtawala wa wilaya* aliposikia kuhusu mambo yaliyokuwa yakitukia, akashikwa na wasiwasi sana kwa sababu watu walikuwa wakisema Yohana alikuwa amefufuliwa kutoka kwa wafu,+ 8 lakini wengine walikuwa wakisema Eliya alikuwa ametokea, na wengine mmoja wa manabii wa kale alikuwa amefufuliwa.+ 9 Herode akasema: “Yohana nilimkata kichwa.+ Basi, ni nani huyu ninayesikia habari hizi kumhusu?” Kwa hiyo alitamani kumwona.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki