-
Mathayo 14:1-5Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 Wakati huo Herode, mtawala wa wilaya,* akasikia habari kumhusu Yesu.+ 2 Akawaambia watumishi wake: “Huyu ni Yohana Mbatizaji. Alifufuliwa kutoka kwa wafu na ndiyo sababu anafanya matendo yenye nguvu.”+ 3 Herode* alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo ndugu yake.+ 4 Kwa maana Yohana alikuwa akimwambia: “Si halali kwako kuwa na mwanamke huyo.”+ 5 Hata hivyo, ingawa Herode alitaka kumuua, aliuogopa umati, kwa sababu walimwona kuwa nabii.+
-
-
Luka 9:7-9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 Basi Herode* mtawala wa wilaya* aliposikia kuhusu mambo yaliyokuwa yakitukia, akashikwa na wasiwasi sana kwa sababu watu walikuwa wakisema Yohana alikuwa amefufuliwa kutoka kwa wafu,+ 8 lakini wengine walikuwa wakisema Eliya alikuwa ametokea, na wengine mmoja wa manabii wa kale alikuwa amefufuliwa.+ 9 Herode akasema: “Yohana nilimkata kichwa.+ Basi, ni nani huyu ninayesikia habari hizi kumhusu?” Kwa hiyo alitamani kumwona.+
-