25 Mungu alimtoa kuwa dhabihu ya upatanisho*+ kupitia imani katika damu yake.+ Ilikuwa hivyo ili kuonyesha uadilifu wake mwenyewe, kwa sababu Mungu kwa uvumilivu* wake alikuwa akizisamehe dhambi zilizofanywa wakati uliopita.
17 Kwa hiyo alipaswa kuwa kama “ndugu” zake katika mambo yote,+ ili awe kuhani mkuu mwenye rehema na mwaminifu katika mambo yanayohusiana na Mungu, ili atoe dhabihu ya upatanisho*+ kwa ajili ya dhambi za watu.+
26 La sivyo, ingekuwa lazima ateseke mara nyingi tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu. Lakini sasa amejifunua mara moja kwa wakati wote kwenye umalizio wa mifumo ya mambo* ili kuondoa dhambi kupitia dhabihu yake mwenyewe.+