Zaburi
74 Ee Mungu, kwa nini umetukataa milele?+
Kwa nini hasira yako inawaka* dhidi ya kundi la malisho yako?+
Ukumbuke Mlima Sayuni, mahali unapokaa.+
3 Zielekeze hatua zako kwenye magofu ya kudumu.+
Adui ameharibu kila kitu mahali patakatifu.+
4 Maadui wako walinguruma ndani ya mahali pako pa mkutano.*+
Wameweka bendera zao wenyewe ziwe ishara humo.
5 Walikuwa kama watu wanaotumia mashoka kufyeka msitu wenye miti mingi.
6 Walivunjavunja michongo yake yote+ kwa mashoka na fito za chuma.
7 Walichoma moto mahali pako patakatifu.+
Walichafua hema la ibada lenye jina lako, wakaliangusha chini.
8 Wao pamoja na uzao wao wamesema mioyoni mwao:
“Sehemu zote za Mungu za mikutano* zilizo nchini ni lazima ziteketezwe.”
9 Hatuoni ishara yoyote;
Hakuna tena nabii yeyote,
Na hakuna yeyote miongoni mwetu anayejua hali hii itaendelea hadi lini.
10 Ee Mungu, mpinzani ataendelea kudhihaki mpaka lini?+
Je, adui ataendelea kulidharau jina lako milele?+
11 Kwa nini unauzuia mkono wako, mkono wako wa kuume?+
Uchomoe kifuani mwako* na kuwaangamiza?
12 Lakini Mungu ni Mfalme wangu tangu zamani za kale,
Yeye anayefanya matendo ya wokovu duniani.+
13 Uliitibua bahari kwa nguvu zako;+
Uliviponda vichwa vya wanyama wakubwa sana wa baharini.
14 Uliviponda vichwa vya Lewiathani;*
Ukawapa watu wamle kama chakula chao, wale wanaokaa jangwani.
16 Mchana ni wako, na usiku pia.
18 Kumbuka dhihaka za adui, Ee Yehova,
Jinsi taifa pumbavu linavyodharau jina lako.+
19 Usiwape wanyama wa mwituni uhai wa* njiwa tetere wako.
Usiusahau milele uhai wa watu wako wanaoteseka.
20 Likumbuke lile agano,
Kwa maana sehemu za dunia zenye giza zimejaa makao ya ukatili.
21 Mtu aliyepondwa na asigeuke na kwenda zake akiwa amekata tamaa;+
Watu wa hali ya chini na maskini na walisifu jina lako.+
22 Inuka, Ee Mungu, na utetee kesi yako.
Kumbuka jinsi wapumbavu wanavyokudhihaki mchana kutwa.+
23 Usisahau mambo ambayo maadui wako wanasema.
Kelele za wale wanaokuasi zinapanda juu daima.