Methali
4 Mali haitakuwa* na faida yoyote siku ya ghadhabu,+
Lakini uadilifu ndio utakaookoa kutoka katika kifo.+
5 Uadilifu wa mtu asiye na lawama hukinyoosha kijia chake,
Lakini mwovu ataanguka kwa sababu ya uovu wake mwenyewe.+
7 Mtu mwovu anapokufa, tumaini lake hutokomea;
Na matarajio aliyokuwa nayo kwa kutegemea nguvu zake hutokomea pia.+
8 Mwadilifu huokolewa kutoka katika taabu,
Na mwovu huingia humo badala yake.+
10 Wema wa watu waadilifu hulifanya jiji lishangilie,
Na waovu wanapoangamia, kunakuwa na kelele za shangwe.+
12 Mtu yeyote asiye na busara* humdharau jirani yake,
Lakini mtu mwenye utambuzi wa kweli hukaa kimya.+
15 Yeyote anayemwekea dhamana ya mkopo* mtu asiyemjua hakika ataumia,+
Lakini yeyote anayeepuka* kumpa mkono ili kumdhamini atakuwa salama.
18 Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu,+
Lakini mtu anayepanda uadilifu hupata thawabu ya kweli.+
19 Anayetetea uadilifu kwa uthabiti atapata uzima,+
Lakini anayefuatia uovu anaelekea kwenye kifo.
21 Uwe na hakika kuhusu hili:* Mtu mwovu hatakosa kuadhibiwa,+
Lakini watoto wa mwadilifu wataponyoka.
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe
Ndivyo alivyo mwanamke mrembo anayekataa busara.
23 Tamaa ya waadilifu huongoza kwenye mema,+
Lakini tumaini la waovu huongoza kwenye ghadhabu.
24 Mtu mmoja hutoa kwa ukarimu* na kupata vitu vingi zaidi;+
Mtu mwingine huwanyima wengine wanachostahili, lakini anakuwa maskini.+
26 Watu watamlaani anayeficha nafaka,
Lakini watambariki anayeiuza.
27 Anayetafuta kwa bidii kutenda mema hutafuta kibali,+
Lakini anayetafuta uovu—kwa hakika atapatwa na uovu.+
29 Yeyote anayewaletea taabu* watu wa nyumbani mwake atarithi upepo,+
Na mpumbavu atakuwa mtumishi wa mtu mwenye hekima moyoni.
31 Ikiwa, kwa hakika, mtu mwadilifu duniani huthawabishwa,
Sembuse mwovu na mtenda dhambi!+