Zaburi
96 Mwimbieni Yehova wimbo mpya.+
Mwimbieni Yehova, dunia yote!+
2 Mwimbieni Yehova; lisifuni jina lake.
Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+
3 Tangazeni utukufu wake miongoni mwa mataifa,
Kazi zake zinazostaajabisha miongoni mwa mataifa yote.+
4 Yehova ni mkuu na anastahili kusifiwa kuliko wote.
Anaogopesha kuliko miungu mingine yote.
7 Mpeni Yehova anachostahili, enyi familia za mataifa,
Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
8 Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili;+
Leteni zawadi na mwingie katika nyua zake.
10 Tangazeni miongoni mwa mataifa: “Yehova amekuwa Mfalme!+
Dunia imeimarishwa kabisa, haiwezi kusogezwa.*
Atayahukumu* mataifa kwa haki.”+
11 Mbingu na zishangilie, dunia na iwe na shangwe;
Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza;+
12 Mashamba na vitu vyote vilivyomo na vishangilie.+